Jamaa anamfuatilia mke wangu

Jamaa anamfuatilia mke wangu

Kama mkeo hamtwki na anakupenda wewe,basi andaeni mpango wa fumanizi ili umkanye akiwa uchi wa mnyama.Ila usimfanye kitu chochote.Mpe onyo tu.
 
Nina rafiki yangu alikupendana na mdada ambae ametoka kutengana na mwanaume wake.

Jamaa akaanza msumbua bi dada akiwa tayari anaishi na rafiki yangu. Rafiki yangu akawasiliana nae, jamaa akajitetea kuwa anafanya hivyo sababu anataka kujua hali ya watoto hakuna ubaya mwingine....

Mtoto wa kwanza ana miaka 6, wa pili ana mwaka na miezi. Jamaa akasubiria mtoto amalize muda wa kunyonya. Huku jamaa akisumbua sana. Mtoto alipotimiza miaka miwili na nusu, jamaa akaona huu ufala.

Jamaa alikuwa bado anaendelea kumsumbua bibie na kubembeleza. So jamaa akamwambia mwanamke awaandae watoto awapeleke kwa baba yao.

Wakaenda na house girl, jamaa akawapokea vizuri, yule dada akalala hapo hapo akiwa na watoto na house girl, walilala chumba tofauti na jamaa asubuhi jamaa akatoka na kwenda kazini akiahidi atarejea mchana mapema ili waketi na kuongea....

Alipoondoka tu yule bi dada akampa maagizo beki tatu kuwa awatazame watoto vizuri yeye anarejea. Akaondoka akarudi home kwake.

Jamaa kurejea anakuta bi dada hayupo na sim yake haipatikani, kumbe amebadili namba kabisa. Mshikaji akampigia mwanaume(aliomba namba kwa beki 3) alipoona hampati bi dada hewani.

Kumpigia jamaa na kujitambulisha jamaa akamwambia unataka nini, jamaa oooh mbona bibie amewaacha watoto na watoto wanahitaji malezi ya mama, akawambia ulikuwa unasumbua kutaka kujua kuhusu watoto. Haya hao hapo upo nao, usimsumbue tena huyu mwanamke sio mkeo tena, na kuhusu malezi hao watoto hawanyonyi tena ni wakubwa wanakula chakula cha kawaida.

So pambana na watoto wako ulee maana ulikuwa unasumbua kisa watoto haya hao hapo na wewe ni baba yao, lea damu yako. Kama hauwataki tuandikishiane kabisa na iwe ni makubaliano kuwa hautaki hao watoto tena, nitalea mimi, na tutarekodi hadi video ukikubaliana kabisa na haya masharti kuwa hautakuwa tena katika maisha yao.... La si hivyo, hao hapo lea watoto wako acha kusumbua mtu asiye kuhusu tena.....

Jamaa akawa wabaridi balaa...... Kurudisha watoto hawezi, kukaa nao bila mwanamke anaona amekomolewa...... Balaa akawa nalo....
Hapo alimpa dawa tena yakumwingia sawa sawa!
 
Mwambie mkeo ahamie kwa mzazi mwenzake asikuchoshe. Unampigania kwani ni shati hilo kuwa haliwezi kujitetea mwingine akitaka kulivaa? Achague kati yako au mzazi mwenzake wa awali. Mwambie kabisa ukigundua lolote ww unakuwa X maana huwezi kushindana na baba wa kwanza.
 
Ni single mother wa mtoto mmoja, jamaa anamfuatilia sana akitaka warudiane lakini mke wangu amekataa kabisa ila jamaa hakati tamaa. Alimtelekeza toka akiwa na mimba miaka mitano imepita ndio amerudi na kuanza kumsumbua huyu mke wangu.

Mimi kazi zangu ni za kusafiri kwahiyo muda mwingine nakuwa sipo nyumbani, hata baada ya mke wangu mimi kuzaa naye watoto jamaa bado tu hakomi

Nifanyeje?
Nipe simu ya huyo bwana nimkanye haraka sana
 
Mambo mengine yapo so easy hapo chukuwa line ya simu ya wife iweke kwenye simu yako. Chat na hilo jambazi nganganizi jifanye wewe ndio kama wife mpe appointment ya kukutana. Nenda na machali wako mkamateni mpeleke ghetto usimfire mpigeni mbrashi tu. Hatosumbua tena😉😂😂


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
Kwenye hilo zoezi mnialike na mie hata kushuhudia tu
 
Nunua bahasha weka weka mafuta yakiwa yameambatana na ujumbe unaosomeka "achana na mke wangu"
Halafu mtumie huyo jamaa
Wa hivyo wanahitaji vilainishi kweli??
 
Eenheee ulimfanyaje???!!!

Hata ivyo kizuri kula na mwenzio
 
Ni single mother wa mtoto mmoja, jamaa anamfuatilia sana akitaka warudiane lakini mke wangu amekataa kabisa ila jamaa hakati tamaa. Alimtelekeza toka akiwa na mimba miaka mitano imepita ndio amerudi na kuanza kumsumbua huyu mke wangu.

Mimi kazi zangu ni za kusafiri kwahiyo muda mwingine nakuwa sipo nyumbani, hata baada ya mke wangu mimi kuzaa naye watoto jamaa bado tu hakomi

Nifanyeje?
Alafu unakuta na hilo lijamaa lipo humu linakupimia
 
Mkuu vipi mpaka leo jamaa kakaza kumbembeleza huyo single mother wako ama bado uko kwenye hizo safari safari zako kama ulivyoziita
 
Back
Top Bottom