Jaji Warioba: Ripoti ya PAC ni dhaifu

Jaji Warioba: Ripoti ya PAC ni dhaifu

Khekhe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee nicheke mie yeye Warioba ripoti yake iko wapi? Yeye aendelee kula pesa za walipa kodi tu, alipokuwa waziri mkuu alifanya nini kama sio uzembe wa kutisha. Kama yeye angekuwa mfanyakazi anayejali maisha ya walipa kodi leo hii Kikwete asingekuwa pale. Udhoofu wake ndio uliowaleta hawa wezi wa mchana kweupe.

Warioba anasema ni dhaifu kwa sababu kuna watu wamelindwa akina Sada Mkuya na Abdalla kigoda wote hawa walipaswa kuwajibishwa
 
Mzee warioba naona kachanganyikiwa sasa, udhaifu wa ripoti ya PAC ukwap? na wakati wao wametohoa data za CAG? Hebu acheni kukatisha watu tamaa.
 
Mzee warioba naona kachanganyikiwa sasa, udhaifu wa ripoti ya PAC ukwap? na wakati wao wametohoa data za CAG? Hebu acheni kukatisha watu tamaa.

Ripoti inanza na "self censorship", eti Waziri Mkuu anaweza kuondolewa, lakini rais akiondolewa nchi itatikisika.

Watu wana mi nchi ina mi silaha ya nyuklia na wamemtoa rais kwa impeachment bila nchi kutikisika.

Ripoti ni dhaifu kwa sababu ilianza kujipiga risasi miguuni yenyewe kabla adui hajaanza kufyatua risasi zake.

Na hata Kikwete akiamua kuikalia bila kuifanyia kazi siwezi kushangaa sana.

Kilichotakiwa ilikuwa kuanzishwe an impeachment motion in parliament. Kikwete apigiwe kura ya impeachment.

Lakini Tanzania tunamuheshimu sana rais, hata anapolala kwenye usukani.
 
MZee hajakosea..Mimi nilioona kabisa report ilikuwa ikitushambulia watu fulani na kuacha fulani.Hiwezekani bank chache zikatajwa na kutaka zishambulia bila kuweka angalizo kwanini nyingine hazikuwekwa.Yule dada waziri wa fedha siamini kwanini kaachwa.Ila ni rahisi sana establish pattern ktk report ya Zitto na ukizingatia tabia yake tangu mwanzo hakuna ubishi huyu jamaa upuuzi hajaacha. KITENDO CHA ZITTO KUSUPPORT "PHRASE YA FISADI CHENGE " Niliona ubaya za zitto ktk kujifanya anajua kuwa kasuku,Baadae akachomekea kwa nidhamu mbaya kabisa kuwa sasa kachoka.Hapa ZItto alijua kuwa alichosema chenge kingekubalika Blindly na UKAWA then ingefikia kwa WEREMA NA PINDA basi mafisadi wangekuwa washindi na Zitto km kibaraka wao angekuwa shujaa.This boy was another kamikaze stuntman in the HOUSE.
 
Mkuu nakuhakikishia kuwa swala hilo haliwezekani chini ya wabunge wa CCM,

Hata kama suala haliwezekani, unafanya motion wananchi wanajua wabunge wako serious. Ipigwe kura watu tujue nani anamuendekeza Kikwete na nani anaangalia maslahi ya nchi.

Moreover, revolutions always look impossible before they happen and inevitable after they happen.
 
MZee hajakosea..Mimi nilioona kabisa report ilikuwa ikitushambulia watu fulani na kuacha fulani.Hiwezekani bank chache zikatajwa na kutaka zishambulia bila kuweka angalizo kwanini nyingine hazikuwekwa.Yule dada waziri wa fedha siamini kwanini kaachwa.Ila ni rahisi sana establish pattern ktk report ya Zitto na ukizingatia tabia yake tangu mwanzo hakuna ubishi huyu jamaa upuuzi hajaacha. KITENDO CHA ZITTO KUSUPPORT "PHRASE YA FISADI CHENGE " Niliona ubaya za zitto ktk kujifanya anajua kuwa kasuku,Baadae akachomekea kwa nidhamu mbaya kabisa kuwa sasa kachoka.Hapa ZItto alijua kuwa alichosema chenge kingekubalika Blindly na UKAWA then ingefikia kwa WEREMA NA PINDA basi mafisadi wangekuwa washindi na Zitto km kibaraka wao angekuwa shujaa.This boy was another kamikaze stuntman in the HOUSE.


Naona Mkuu kutajwa kwa maaskofu kumekuuma Sana.
 
Ripoti ingekuwa si dhaifu Kikwete angepigiwa kura ya impeachment bungeni.


Kwa msingi Wa report ile ya CAG ingekua ngumu tu...

ila Kama ingekwenda ile original iyobainisha mpaka wamiliki Wa Simba trust nchi ingewaka moto Bahati mbaya ilichakachuliwa Sana....
 
ni kweli Ripoti ya PAC ina udhaifu kwa sababu inaendeleza mambo yale yale ya akina mwakyembe,ya kuogopa kutaja baadhi ya watu eti nchi itatikisika.kwa uoga huo ndio maana mzimu IPTL unaendelea kulitafuna Taifa letu.
 
Mbona unamshambulia Sana Zitto wakati kamati ilikua na watu 24? Ile haikua ripoti za ya Zitto ni ya PAC
Kwa vile alijikusanyia sana sifa,na mara nyingi alitofautiana na wenzio,ktk final report bungeni.Mara nyingi wenzie walihitaji kujaribu Tumia lugha nzuri ili wasiguse hisia zake.
 
Waziri wa Fedha ambaye kwa uelewa wake finyu wa mambo ya kodi anataka kutoza kodi pesa za wizi, na saa zote ni kiguu na njia kupigia debe chama badala ya kufuatilia urudishwaji wa mabilioni ya Uswiss &529 million wakati hazina ikiwa haina kitu.

Hili nalo jipya......lkn kiukweli hata mimi nilishangaa Waziri wa fedha kutoguswa na hili sakata.
 
Jf ilikuwa na info za kutosha zenye uzito mkubwa kuliko ile ripoti.

Nashangaa ilikuwaje ripoti iwe shallow vile,ilhali hao hao akina Zitto walikuwa wakimwaga mambo mengi mitandaoni.

Anyway,ngoja tuone hicho kidogo walichokabidhi kitashughulikiwaje.

You never know,huenda alikuwa na shinikizo la kupunguza makali ya ripoti kutoka kwa members wa PAC wa chama tawala,manake mambo mengi mazito tuliyasikia wakati wa mjadala toka kwa akina Lissu,kuliko yaliyokuwemo kwenye ripoti,hii ikasababisha akina Lissu waonekane wapiga porojo tu,mfano ni malipo ya viroba hayakuelezewa kwa kina.

Zito huyu huyu ukimsoma mitandaoni ameandika mambo mazito sana ambayo baadhi hayamo kwenye ripoti.

Kwa nini ripoti za CAG na TAKUKURU ambazo ndio authority ya PAC report zinafichwafichwa?
 
attachment.php
 
Waziri wa Fedha ambaye kwa uelewa wake finyu wa mambo ya kodi anataka kutoza kodi pesa za wizi, na saa zote ni kiguu na njia kupigia debe chama badala ya kufuatilia urudishwaji wa mabilioni ya Uswiss &529 million wakati hazina ikiwa haina kitu.

Naona wanahangaika Sana kukopa fedha za mishahara wamesababisha NMB isitishe huduma ya mikopo kwa ajili ya kuwakopesha wao...

Nchi ipo kwenye hali mbaya Sana jamani tatizo watu wake wanawekeza ktk starehe kuliko kufikiri mambo ya nchi....

Inauma kuona watunga Sera wetu wakiwa vihiyo kiasi cha kushindwa hata kuelewa wanasimamia nini....

Much worse!!!!!
 
Mkuu lusungo tusishangae Kikwete atakapomaliza awamu yake ataacha deni la Taifa kati ya trillion 80 mpaka Trilioni 100 kulilipa hili deni itakuwa ni kazi ambayo haitawezekana na athari yake kwa Taifa itakuwa kubwa sana.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu lusungo tusishangae Kikwete atakapomaliza awamu yake ataacha deni la Taifa kati ya trillion 80 mpaka Trilioni 100 kulilipa hili deni itakuwa ni kazi ambayo haitawezekana na athari yake kwa Taifa itakuwa kubwa sana.


Kweli mkuu mkuu hali ni mbaya mno madeni yanaongezeka kila uchao...thamani ya shilingi inashuka kila siku....

Pathetic!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Naona wanahangaika Sana kukopa fedha za mishahara wamesababisha NMB isitishe huduma ya mikopo kwa ajili ya kuwakopesha wao...

Nchi ipo kwenye hali mbaya Sana jamani tatizo watu wake wanawekeza ktk starehe kuliko kufikiri mambo ya nchi....

Inauma kuona watunga Sera wetu wakiwa vihiyo kiasi cha kushindwa hata kuelewa wanasimamia nini....

Much worse!!!!!

Hali hii huzidi kuwa mbaya sana bongo pale marais wanapokuwa wanamalizia awamu zao.

Sijui kwa nini?!
 
Mkuu lusungo tusishangae Kikwete atakapomaliza awamu yake ataacha deni la Taifa kati ya trillion 80 mpaka Trilioni 100 kulilipa hili deni itakuwa ni kazi ambayo haitawezekana na athari yake kwa Taifa itakuwa kubwa sana.

Hatari aisee!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom