Jaji Warioba: Ripoti ya PAC ni dhaifu

Jaji Warioba: Ripoti ya PAC ni dhaifu

Hili nalo jipya......lkn kiukweli hata mimi nilishangaa Waziri wa fedha kutoguswa na hili sakata.

Na wewe "sada tulia" haya maneno aliyasema zito wakati sada mkuya alipochangia utumbo
 
Nilisema na ninarudia kusema kuwa kamati ya Bunge ya PAC haikuwa na weledi wa kuichambua na kuielewa ripoti ya CAG na wala hawakuwa na weledi wa kufanya uchunguzi wao wenyewe. Matokeo yake walichukua hoja za CAG wakachakachua ili kufikia malengo yao ya kisiasa. Maswali ambayo CAG alishindwa kuyajibu kwenye uchunguzi wake na kupendekeza uchunguzi zaidi PAC nao wameshindwa kuyajibu pia na badala yake wakayatafutia majibu yanayokidhi matakwa yao ya kisiasa.
 
Kwa maoni ya Warioba kunahitajika kufanywe ajwari ,ili Zito na wenzake wajipange upya ,na zaidi ipatikane suluhu ya kutoonewa mtu na kuachwa mtu ,kila mtu abebe mzigo wake kwa haki.

Mambo ya kutoana kafara ili wengine wasalimike wakati huo umepitwa ,haki itendeke vinginevyo Zito nae achunguzwe kwa kukwepa na kuwakwepa wengine kama alivyodai Mh.Warioba ,utamhusishaje Waziri mkuu kwamba mambo akiyajua wakati Wizara ya fedha nayo hukuitaja wala kuihusisha isipokuwa madagaa wachache wasio na mapezi ya kuwavukisha kina kikubwa chenye mawimbi.

Zito achunguzwe,inaonekana kuna watu amewalinda.

Zitto au kamati ya PAC yenye wajumbe 24? Naona issue anasukumiziwa mtu mmoja inakuwaje!!?
 
Raia Tanzania, leo jumanne trh 02/12/2014

WARIOBA: RIPOTI YA ZITO DHAIFU, NGELEJA KAHUSIKAJE ESCROW?

Waziri mkuu na makamu wa pili wa rais wa zamani, Jaji Joseph Warioba, amesema ripoti ya kamati ya bunge ya hesabu za serikali (PAC) chini ya Kabwe Zitto kuhusu akaunti ya tegeta Escrow ilikuwa dhaifu, yenye kuendeleza tabia ya kulindana.

Zaidi ya hapo, Jaji Warioba alisema kwa namna fulani Bunge la Jamhuri ya Muungano limeingilia uhuru wa mihimili mingine kutokana na maazimio yake.

Akizungumza na Raia Tanzania ofisini kwake jijini Dar es salaam, Jaji Warioba alisema ripoti ya PAC imeacha maswali kadhaa bila majibu.
"Wameacha maswali hayana majibu, la kwanza, taarifa ya kamati ya Hesabu za serikali (PAC), imeonyesha udhaifu katika maeneo mengi. Moja ni katika eneo linalohusu Wizara ya Nishati na Madini, pili ni yale yanayohusu Wizara ya fedha na tatu ni yale yanayohusu Wizara ya Viwanda na Biashara.

Alisema katika mjadala wa sakata la Escrow Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara hazikuguswa licha ya kwamba ndio wahusika wakuu wa hasara inayojulikana.

" Katika mawasiliano yote (kuhusu utoaji fedha Escrow) Waziri mkuu walimuingiza kwa kusema alikuwa akipata nakala za barua lakini wizara ya Fedha ilihusika katika mawasiliano na wameachwa" alisema Warioba.

Yafuatayo ni maelezo ya kina ya Jaji Warioba:

IPTL NI MZIGO

"Nataka nizungumzie mchakato wa Escrow, kwanza, IPTL imekuwa mzigo kwa nchi kwa muda mrefu tangu kampuni hiyo ilipoundwa, imekuwa na matatizo mengi. Katika kipindi hicho nchi imepoteza fedha nyingi kupitia kesi zilizotokana na IPTL ".

Nimesikia kwenye bunge kampuni moja ya wanasheria imelipwa sh.bilioni 62 lakini haikuwa peke yake, katika kesi hizo kulikuwa na gharama za TANESCO kwa kuwa walikuwa wakipeleka watu na kulikuwa na gharama za serikali, kwa hiyo fedha zilizotumika kwa migogoro hii ni nyingi.

"Katika utendaji wenyewe kulikuwa na matatizo, kwa hiyo nadhani ni jambo jema kwa sababu ya tatizo lililotokea lizungumzwe kwa undani ili kumaliza matatizo ya IPTL, tusiendelee nayo na gharama zake kwa nchi..
Kwa hiyo kulipeleka bungeni ilikuwa ni jambo zuri na limezungumzwa na ninaamini baada ya mchakato huu tutafika mahali tumalize matatizo ya IPTL na kuendelea na shughuli zingine za uchumi" alisema Warioba.

MAMBO MATATU MUHIMU

Warioba alisema hadi suala la IPTL linafikishwa bungeni na kisha kupatikana kwa maazimio ya Bunge kuna mambo matatu yameongoza mjadala:

La kwanza, ni wananchi, wananchi walikuwa na hamu ya kusikiliza mjadala Hui na kuona matokeo yake ni nini. Yalipokuwa yakitokea matatizo kama vile ya umeme, walikuwa wakilalamika kwa kuwa walitaka wafuatilie kwa ukaribu sana.

Hili kwa kiwango kikubwa naweza kusema ni kama vile imani ya wananchi kwa uongozi, hivyo kwa kila jambo linalotokea likiwahusu viongozi, wananchi wanakuwa makini kuona ni nini kitatokea. Hivyo bunge lilipokuwa likizungumza walijua kwamba wananchi wanatarajia kutatokea uamuzi mzito na si mazungumzo tu.

La pili, ni kwamba tunazungumza wakati huu ni kama wahisani wamesimamisha misaada kwa serikali na hata katika mjadala wengine walitaja hilo, kwamba limetuletea matatizo nchi sasa haipati misaada, kwa hiyo walipozungumza walijua kuwa wahisani walitaka waone matokeo ya hilo.

La tatu, nadhani ni siasa kwa kiwango kikubwa. Tunaingia katika kipindi cha uchaguzi, kwa hiyo vyama vinatafuta mambo ya kampeni kwa pande zote mbili, chama tawala na vyama vya upinzani. Nina hakika hili litaendelea kuwa jambo litakalozungumzwa wakati wa kampeni, kwa hiyo mazungumzo yote, huo ndo ulikuwa msingi wake.

FEDHA ZA ESCROW NI ZA NANI?

Mazungumzo yalivyokwenda utaona kubwa ambalo ndilo msingi wa uamuzi uliofanywa na bunge ni kuwa fedha za Escrow zilikuwa mali ya umma na ndivyo wananchi wamefanywa waamini hilo lakini hakuna palipothibitishwa kuwa ni za umma. Msingi wa Escrow ni kwamba pande hizi mbili hazikuwa zikikubaliana kuhusu capacity charge, hivyo kwa kuwa hawakuwa wakikubaliana waliona wawe na utaratibu, kwanza waendelee kushauriana wao wenyewe au kwenye mahakama ya nje; lakini kwa kipindi hicho kwa kuwa hawakuwa wakikubaliana, iliafikiwa kuwe na mpango wa kuweka fedha mpaka watakapofikia makubaliano. Katika kipindi chote hicho IPTL ilikuwa ikitoa huduma, kwa hiyo kwa vyovyote vile ilikuwa na haki ya kulipwa capacity charge watakapokubaliana.

Hivyo kilicho cha uhakika katika fedha zile ni kwamba, zipo za capacity charge, hawakufika mahali waseme ni kiasi gani, lakini kwa kuwa sasa wanakwenda kuchunguza nina hakika mwisho itaonekana sehemu kubwa ya fedha hizo zilikuwa ni za capacity charge", alisema warioba.

Hata hivyo, wananchi wamefanywa waamini kwamba fedha zote zilikuwa ni za umma, hilo ni mwelekeo wa kisiasa. Ni sawa wamefikia hapo, kama wameamua kwa msingi huo, wanasema kuna watu ni lazima wawajibike kwa hasara ambayo nchi imepata.

VIPORO VYA MASWALI

Jaji Warioba alisema mchakato huu wa IPTL na akaunti ya Escrow umeacha maswali kadhaa.:

" Wameacha maswali hayana majibu, la kwanza , taarifa ya kamati ya Hesabu za serikali (PAC), imeonyesha udhaifu katika maeneo mengi. Moja ni katika eneo linalohusu Wizara ya Nishati na Madini, pili ni yale yanayohusu Wizara ya ya Fedha na tatu ni yale yanahusu Wizara ya viwanda na biashara.

" Hasara inayotajwa kwa uhakika ilikuwa inahusu kodi inayotokana na mauzo ya hisa na hiyo si strictly ya Escrow ni kodi ya mauzo ya hisa , kwa namna ya capital gains tax na stamp duty. Wanaohusika hasa ni Wizara ya Fedha na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na pia wizara ya viwanda kwa maana ya Brela.

"Katika mjadala huu inaonekana kama wizara ya fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara hazikuguswa na huko ndiko yametokea matatizo ya hasara inayojulikana. Nimesoma taarifa ya PAC, wakifika kwenye wizara ya fedha, wanasema PAP kwa kushirikiana na maofisa wadogo wa TRA walofanya dhambi hii, sasa ni kama wanataka kuilinda Wizara ya Fedha. Katika mawasiliano yote Waziri Mkuu walimuingiza kwa kusema alikuwa akipata nakala za barua kakini Wizara ya Fedha ilihusika kabisa katika mawasiliano na wameachwa.

Brela wamefanya uzembe kwamba, unaweza kuandikisha kampuni na watu wakatia saini na majina hayapo, unaona kulikuwa na kasoro lakini haikuguswa. Kwa hiyo licha ya kuwa wameamua kuchagua watu waliohusika, inaonekana walikwenda mahali pamoja na huku kwingine wamewalinda.

Wamewalinda viongozi wa wizara ya fedha na Wizara ya Viwanda, wakati vitendo vilivyosababisha hasara ya kodi kupatikana vimetendwa katika wizara hizi. Nijachouliza hapa ni kwa nini hawakutajwa, kuna element ya kulindana.

La pili linaloonekana kwamba kuna kulindana ni kwamba, waliopokea fedha kutoka kwa Rugemalira (James) wote wametajwa. Akaunti ya Rugemalira imetajwa katika benki ya mkombozi na hao wametuhumiwa lakini wanaohusika na fedha zilizotolewa stanbic bank , ambazo kamati inasema zilichukuliwa kwenye mifuko ya rambo, lumbesa na kwenye magunia, hawakutaja ni nani alichukua.

"Kwa sababu kama wanajua zilichukuliwa kwa njia hiyo, lazima watakuwa wanajua ni nani alichukua. Hivyo ni kwa nini hao waliochukua upande huu hawakutajwa? Unaaanza kuwa na maswali kuwa hapa kuna dalili za kulindana na wameendelea hivyo na kutoa uamuzi.

"Umuzi ule ni kama wa mahakama, bunge limekaa na kuamua kwamba fedha hizi na hasa alizolipa Rugemalira zilikuwa chafu na wote waliopokea fedha hizo walizipokea zikiwa chafu, hivyo na wao waadhibiwe. Wana ushahidi gani? Hawakuwasikiliza wale watu. Unasema kuna askofu amepewa fedha umuhukumu kwamba alijua kuwa ni fedha chafu, kuna jaji hapa alipata fedha unasema alijua ni fedha chafu, kuna Waziri alichukua fedha unasema alijua kuwa ni chafu, lakini hawakuwasikiliza.

" Kwa hiyo, wamehukumu bila kuwasikiliza na wamependekeza hatua za kuchukua. Baadhi yao wamesema wachukuliwe hatua za kinidhamu na wengine walipe kodi. Najiuliza kama askofu amepewa fedha, unasimama kwenye bunge unasema ajiandae kulipa kodi, najiuliza hivi ni mara ya kwanza kwa wao na watu wengine kupata fedha za aina hii? Mbona viongozi hao hao wanatoa misaada tena mikubwa na mahali pengi, mamilioni hatujasikia wakisema waliopewa walipe kodi.

" Hivi tuna uhakika gani kwamba hizi site zinazochangwa ni halali? Kwanini hawa ndio walipe kodi lakini zinazotolewa na wanasiasa husemi zilipiwe kodi.
Nadhani bunge halikutumia madaraka yake sawasawa. Unamwambia rais aunde tume ya kuwachunguza majaji walipata fedha, anaunda tume kwa msingi gani?

"Kwa sababu sheria inasema yakiwapo malalamiko kuhusu jaji, rais ataunda tume. Sasa hapa bunge linampelekea malalamiko gani yatakayomfamya aunde tume. Bunge lina ushahidi gani kwa sababu halikuwasikiliza ili kusema kuna malalamiko? Hilo nadhani bunge limeingilia mambo yasiyolihusu, ingekuwa haki kwamba hujatamka hatua gani zichukuliwe wangepata maelezo kutoka kwa wote wanaohusika ndipo ubaini kama kuna shaka ndipo uchukue hatua.....

Na Ester Mvungi, Dar es salaam
 
Warioba ni mzee aliyekosa busara. Ila kwa hili kuna mahala namuunga mkono. Ile ripoti ya PAC ilikuwa inawalenga watu fulani. Ndo maana wakamuingiza na Maselle kwa makosa yasiyojulikana

Wewe ni sawa na kijana ambaye hata degree hana halafu anahoji elimu ya professor aliipataje
 
Mzee anaona kiki yake imechukuliwa na Zitto ana mind.
 
binafsi nilikuelewa na bado naamini,kwa yeyote asiyependa kujitoa akili,atakubali kuwa report ya zito ilikuwa ovyo na dhaifu sana.kwanza uandishi wake mbaya na uwasilishaji ulikuwa mbaya.report ilianghaika na watu ambao nadhani wangelikuwa mashahidi wakawa ndo wakosaji.wameachwa wahusika halisi pamoja na ukweli kwamba bado hakuna ushahidi wa kutosha dhidi ya makosa yaliyofanyika.pac inaundwa na watu wengi wenye average and low brain,wakaalika watu wa aina hyohyo.wenzetu kamatikama hzi zinakuwa na watu wenye akili ya kutosha.

Kwanini wizara ya fedha ,Msajili wa makampuni ..afisa wa Ikulu Mbena aliyeandika Barua ...wameachwa..au imechagua iliolenga kuwangusha
 
Na wewe "sada tulia" haya maneno aliyasema zito wakati sada mkuya alipochangia utumbo

Du so inamaana alimaanisha haya hayakugusi tulia..maana ni AJABU Sana waziri wa fedha katajwa Sana na ikidaiwa hadi kuna aliyekufa kwa Ajili Hiyo na ikitakiwa ijulikane nani alikuwa anakaimu wizara ..definitely alikuwa Saada
 
Mimi nafikiri sasa tunakoelekea ktk hii nchi yetu ni kuwa watu wanajaribu kuongea na kuwatete watu(watuhumiwa) kulingana na uhusiano wao(ukabila/kutoka mkoa mmoja au urafiki wa muda mrefu).Huwa namuheshimu na kumkubali sana mzee wangu Warioba.Mzee huyu ana IQ kubwa na uwelewa mpana sana. Ila kwa maoni yake haya naona kama ameteleza kidogo.
PAC wamefanya utafiti wamegundua kuwa kuna baadhi ya hela ya umma ktk Escrow akaunti,na hili limedhibitshwa na TRA wenyewe,CAG na naibu waziri wa Fedha.Hawa ni watu ambao wapo serikalini kwa sasa na wanajua vizuri michakato inavyoendelea serikalini.Sawa mzee Warioba alikuwa serikalini,ila kwa sasa hayupo serikalini,hivyo naamini hajui kila kitu kinachoendelea ktk serikali yetu kwa sasa.
Sasa naomba kumuuliza mzee Warioba,alifanya lini uchunguzi wake akabaini kuwa hazikuwa hela za umma?na kitu gani kimemfanya kusema kuwa RIPOTI ya PAC ILIKUWA DHAIFU?au kwa sababu hiyo ripoti haikuitaja wizara ya viwanda na biashara?.HAPANA nafikiri kuna sababu nyingine.Kwa mtu msomi kama mzee Warioba kamwe hawezi kusema kuwa RIPOTI YA KAMATI YA BUNGE ILIKUWA DHAIFU,labda uwe na maslahi na watuhumiwa.
Nomba kumuuliza tena mzee Warioba,mbona sikuwahi kumsikia sehemu yoyote kuikosoa ile kamati/tume ya akina Mwakyembe iliomng'oa Mzee Rowassa na baadhi ya mawaziri?Au ni kwa sababu hakukuwa na WAZIRI, AG,NA KATIBU MKUU WA WIZARA KUTOKA MARA?Na kwa nini ametumia nguvu kubwa kuikosoa RIPOTI YA PAC?,au ni sababu RIPOTI YA PAC kutaja ndugu zake kutoka MARA ?(AG anatoka Mara,Waziri wa Nishati anatoka Mara,na Katibu mkuu wa wizara ya nishati anatoka Mara).Jaji Warioba ana urafiki wa karibu sana na hawa watuhumiwa ndio maana ametumia energy kubwa kuiponda Ripoti ya PAC.
 
Mimi nafikiri sasa tunakoelekea ktk hii nchi yetu ni kuwa watu wanajaribu kuongea na kuwatete watu(watuhumiwa) kulingana na uhusiano wao(ukabila/kutoka mkoa mmoja au urafiki wa muda mrefu).Huwa namuheshimu na kumkubali sana mzee wangu Warioba.Mzee huyu ana IQ kubwa na uwelewa mpana sana. Ila kwa maoni yake haya naona kama ameteleza kidogo.
PAC wamefanya utafiti wamegundua kuwa kuna baadhi ya hela ya umma ktk Escrow akaunti,na hili limedhibitshwa na TRA wenyewe,CAG na naibu waziri wa Fedha.Hawa ni watu ambao wapo serikalini kwa sasa na wanajua vizuri michakato inavyoendelea serikalini.Sawa mzee Warioba alikuwa serikalini,ila kwa sasa hayupo serikalini,hivyo naamini hajui kila kitu kinachoendelea ktk serikali yetu kwa sasa.
Sasa naomba kumuuliza mzee Warioba,alifanya lini uchunguzi wake akabaini kuwa hazikuwa hela za umma?na kitu gani kimemfanya kusema kuwa RIPOTI ya PAC ILIKUWA DHAIFU?au kwa sababu hiyo ripoti haikuitaja wizara ya viwanda na biashara?.HAPANA nafikiri kuna sababu nyingine.Kwa mtu msomi kama mzee Warioba kamwe hawezi kusema kuwa RIPOTI YA KAMATI YA BUNGE ILIKUWA DHAIFU,labda uwe na maslahi na watuhumiwa.
Nomba kumuuliza tena mzee Warioba,mbona sikuwahi kumsikia sehemu yoyote kuikosoa ile kamati/tume ya akina Mwakyembe iliomng'oa Mzee Rowassa na baadhi ya mawaziri?Au ni kwa sababu hakukuwa na WAZIRI, AG,NA KATIBU MKUU WA WIZARA KUTOKA MARA?Na kwa nini ametumia nguvu kubwa kuikosoa RIPOTI YA PAC?,au ni sababu RIPOTI YA PAC kutaja ndugu zake kutoka MARA ?(AG anatoka Mara,Waziri wa Nishati anatoka Mara,na Katibu mkuu wa wizara ya nishati anatoka Mara).Jaji Warioba ana urafiki wa karibu sana na hawa watuhumiwa ndio maana ametumia energy kubwa kuiponda Ripoti ya PAC.

Watanzania tuna shida moja kubwa,Ya kusoma na kulielewa andishi.Hata mimi mbumbumbu wa masuala ya kiuchambuzi niliona udhaifu flani Kwenye ile ripoti ya PAC.Kushindwa kutàja majina ya wahusika waliochukua fedha Kwenye viroba;Kushindwa kuwataja Mawaziri kwenye wizara za Fedha na Viwanda ambazo nazo kwa kiasi kikubwa zinaonekana kuhusika katika uchotwaji wa fedha za ESCROW. So ni kweli ripoti hii imebezi kwenye kukandamizana kwa upande mmoja;Na kubebana kwa upande mwingine.
 
Hili nalo jipya......lkn kiukweli hata mimi nilishangaa Waziri wa fedha kutoguswa na hili sakata.
Hawajaligusa kwa sababu inatakiwa tutambue uchafu huu umefanyika wakati waziri wa fedha Dr Mgimwa akiwa tayari wamemlisha SUMU na akiwa mgonjwa na kupelekwa South Africa nikimaanisha mwezi Sept. - Dec 2013 kwa hiyo waziri kamili alikuwa Mgonjwa na aliyekuwepo ni huyu naibu Nkuya ambaye kiuhalisia na jinsi alivyo dhaifu nafikiri na inawezekana hakuhusishwa kabisa kwani hapo alipo ni boya tu hajui mbele wala nyuma.
 
Watanzania tuna shida moja kubwa,Ya kusoma na kulielewa andishi.Hata mimi mbumbumbu wa masuala ya kiuchambuzi niliona udhaifu flani Kwenye ile ripoti ya PAC.Kushindwa kutàja majina ya wahusika waliochukua fedha Kwenye viroba;Kushindwa kuwataja Mawaziri kwenye wizara za Fedha na Viwanda ambazo nazo kwa kiasi kikubwa zinaonekana kuhusika katika uchotwaji wa fedha za ESCROW. So ni kweli ripoti hii imebezi kwenye kukandamizana kwa upande mmoja;Na kubebana kwa upande mwingine.
Mkuu Kuitaja familia ya mkuu wa kaya kwa majina kuwa walichukua fedha kwenye magunia yahitaji moyo ndugu kwani unaweza kufanywa chochote na usipate mtetezi kwani watu wana kumbukumbu sana za yaliyomkuta Ulimboka na akina Kibanda na Dr Mvungi bila kumsahau Dr. Mgimwa
 
Raia Tanzania, leo jumanne trh 02/12/2014

WARIOBA: RIPOTI YA ZITO DHAIFU, NGELEJA KAHUSIKAJE ESCROW?

Waziri mkuu na makamu wa pili wa rais wa zamani, Jaji Joseph Warioba, amesema ripoti ya kamati ya bunge ya hesabu za serikali (PAC) chini ya Kabwe Zitto kuhusu akaunti ya tegeta Escrow ilikuwa dhaifu, yenye kuendeleza tabia ya kulindana.

Zaidi ya hapo, Jaji Warioba alisema kwa namna fulani Bunge la Jamhuri ya Muungano limeingilia uhuru wa mihimili mingine kutokana na maazimio yake.

Akizungumza na Raia Tanzania ofisini kwake jijini Dar es salaam, Jaji Warioba alisema ripoti ya PAC imeacha maswali kadhaa bila majibu.
"Wameacha maswali hayana majibu, la kwanza, taarifa ya kamati ya Hesabu za serikali (PAC), imeonyesha udhaifu katika maeneo mengi. Moja ni katika eneo linalohusu Wizara ya Nishati na Madini, pili ni yale yanayohusu Wizara ya fedha na tatu ni yale yanayohusu Wizara ya Viwanda na Biashara.

Alisema katika mjadala wa sakata la Escrow Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara hazikuguswa licha ya kwamba ndio wahusika wakuu wa hasara inayojulikana.

" Katika mawasiliano yote (kuhusu utoaji fedha Escrow) Waziri mkuu walimuingiza kwa kusema alikuwa akipata nakala za barua lakini wizara ya Fedha ilihusika katika mawasiliano na wameachwa" alisema Warioba.

Yafuatayo ni maelezo ya kina ya Jaji Warioba:

IPTL NI MZIGO

"Nataka nizungumzie mchakato wa Escrow, kwanza, IPTL imekuwa mzigo kwa nchi kwa muda mrefu tangu kampuni hiyo ilipoundwa, imekuwa na matatizo mengi. Katika kipindi hicho nchi imepoteza fedha nyingi kupitia kesi zilizotokana na IPTL ".

Nimesikia kwenye bunge kampuni moja ya wanasheria imelipwa sh.bilioni 62 lakini haikuwa peke yake, katika kesi hizo kulikuwa na gharama za TANESCO kwa kuwa walikuwa wakipeleka watu na kulikuwa na gharama za serikali, kwa hiyo fedha zilizotumika kwa migogoro hii ni nyingi.

"Katika utendaji wenyewe kulikuwa na matatizo, kwa hiyo nadhani ni jambo jema kwa sababu ya tatizo lililotokea lizungumzwe kwa undani ili kumaliza matatizo ya IPTL, tusiendelee nayo na gharama zake kwa nchi..
Kwa hiyo kulipeleka bungeni ilikuwa ni jambo zuri na limezungumzwa na ninaamini baada ya mchakato huu tutafika mahali tumalize matatizo ya IPTL na kuendelea na shughuli zingine za uchumi" alisema Warioba.

MAMBO MATATU MUHIMU

Warioba alisema hadi suala la IPTL linafikishwa bungeni na kisha kupatikana kwa maazimio ya Bunge kuna mambo matatu yameongoza mjadala:

La kwanza, ni wananchi, wananchi walikuwa na hamu ya kusikiliza mjadala Hui na kuona matokeo yake ni nini. Yalipokuwa yakitokea matatizo kama vile ya umeme, walikuwa wakilalamika kwa kuwa walitaka wafuatilie kwa ukaribu sana.

Hili kwa kiwango kikubwa naweza kusema ni kama vile imani ya wananchi kwa uongozi, hivyo kwa kila jambo linalotokea likiwahusu viongozi, wananchi wanakuwa makini kuona ni nini kitatokea. Hivyo bunge lilipokuwa likizungumza walijua kwamba wananchi wanatarajia kutatokea uamuzi mzito na si mazungumzo tu.

La pili, ni kwamba tunazungumza wakati huu ni kama wahisani wamesimamisha misaada kwa serikali na hata katika mjadala wengine walitaja hilo, kwamba limetuletea matatizo nchi sasa haipati misaada, kwa hiyo walipozungumza walijua kuwa wahisani walitaka waone matokeo ya hilo.

La tatu, nadhani ni siasa kwa kiwango kikubwa. Tunaingia katika kipindi cha uchaguzi, kwa hiyo vyama vinatafuta mambo ya kampeni kwa pande zote mbili, chama tawala na vyama vya upinzani. Nina hakika hili litaendelea kuwa jambo litakalozungumzwa wakati wa kampeni, kwa hiyo mazungumzo yote, huo ndo ulikuwa msingi wake.

FEDHA ZA ESCROW NI ZA NANI?

Mazungumzo yalivyokwenda utaona kubwa ambalo ndilo msingi wa uamuzi uliofanywa na bunge ni kuwa fedha za Escrow zilikuwa mali ya umma na ndivyo wananchi wamefanywa waamini hilo lakini hakuna palipothibitishwa kuwa ni za umma. Msingi wa Escrow ni kwamba pande hizi mbili hazikuwa zikikubaliana kuhusu capacity charge, hivyo kwa kuwa hawakuwa wakikubaliana waliona wawe na utaratibu, kwanza waendelee kushauriana wao wenyewe au kwenye mahakama ya nje; lakini kwa kipindi hicho kwa kuwa hawakuwa wakikubaliana, iliafikiwa kuwe na mpango wa kuweka fedha mpaka watakapofikia makubaliano. Katika kipindi chote hicho IPTL ilikuwa ikitoa huduma, kwa hiyo kwa vyovyote vile ilikuwa na haki ya kulipwa capacity charge watakapokubaliana.

Hivyo kilicho cha uhakika katika fedha zile ni kwamba, zipo za capacity charge, hawakufika mahali waseme ni kiasi gani, lakini kwa kuwa sasa wanakwenda kuchunguza nina hakika mwisho itaonekana sehemu kubwa ya fedha hizo zilikuwa ni za capacity charge", alisema warioba.

Hata hivyo, wananchi wamefanywa waamini kwamba fedha zote zilikuwa ni za umma, hilo ni mwelekeo wa kisiasa. Ni sawa wamefikia hapo, kama wameamua kwa msingi huo, wanasema kuna watu ni lazima wawajibike kwa hasara ambayo nchi imepata.

VIPORO VYA MASWALI

Jaji Warioba alisema mchakato huu wa IPTL na akaunti ya Escrow umeacha maswali kadhaa.:

" Wameacha maswali hayana majibu, la kwanza , taarifa ya kamati ya Hesabu za serikali (PAC), imeonyesha udhaifu katika maeneo mengi. Moja ni katika eneo linalohusu Wizara ya Nishati na Madini, pili ni yale yanayohusu Wizara ya ya Fedha na tatu ni yale yanahusu Wizara ya viwanda na biashara.

" Hasara inayotajwa kwa uhakika ilikuwa inahusu kodi inayotokana na mauzo ya hisa na hiyo si strictly ya Escrow ni kodi ya mauzo ya hisa , kwa namna ya capital gains tax na stamp duty. Wanaohusika hasa ni Wizara ya Fedha na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na pia wizara ya viwanda kwa maana ya Brela.

"Katika mjadala huu inaonekana kama wizara ya fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara hazikuguswa na huko ndiko yametokea matatizo ya hasara inayojulikana. Nimesoma taarifa ya PAC, wakifika kwenye wizara ya fedha, wanasema PAP kwa kushirikiana na maofisa wadogo wa TRA walofanya dhambi hii, sasa ni kama wanataka kuilinda Wizara ya Fedha. Katika mawasiliano yote Waziri Mkuu walimuingiza kwa kusema alikuwa akipata nakala za barua kakini Wizara ya Fedha ilihusika kabisa katika mawasiliano na wameachwa.

Brela wamefanya uzembe kwamba, unaweza kuandikisha kampuni na watu wakatia saini na majina hayapo, unaona kulikuwa na kasoro lakini haikuguswa. Kwa hiyo licha ya kuwa wameamua kuchagua watu waliohusika, inaonekana walikwenda mahali pamoja na huku kwingine wamewalinda.

Wamewalinda viongozi wa wizara ya fedha na Wizara ya Viwanda, wakati vitendo vilivyosababisha hasara ya kodi kupatikana vimetendwa katika wizara hizi. Nijachouliza hapa ni kwa nini hawakutajwa, kuna element ya kulindana.

La pili linaloonekana kwamba kuna kulindana ni kwamba, waliopokea fedha kutoka kwa Rugemalira (James) wote wametajwa. Akaunti ya Rugemalira imetajwa katika benki ya mkombozi na hao wametuhumiwa lakini wanaohusika na fedha zilizotolewa stanbic bank , ambazo kamati inasema zilichukuliwa kwenye mifuko ya rambo, lumbesa na kwenye magunia, hawakutaja ni nani alichukua.

"Kwa sababu kama wanajua zilichukuliwa kwa njia hiyo, lazima watakuwa wanajua ni nani alichukua. Hivyo ni kwa nini hao waliochukua upande huu hawakutajwa? Unaaanza kuwa na maswali kuwa hapa kuna dalili za kulindana na wameendelea hivyo na kutoa uamuzi.

"Umuzi ule ni kama wa mahakama, bunge limekaa na kuamua kwamba fedha hizi na hasa alizolipa Rugemalira zilikuwa chafu na wote waliopokea fedha hizo walizipokea zikiwa chafu, hivyo na wao waadhibiwe. Wana ushahidi gani? Hawakuwasikiliza wale watu. Unasema kuna askofu amepewa fedha umuhukumu kwamba alijua kuwa ni fedha chafu, kuna jaji hapa alipata fedha unasema alijua ni fedha chafu, kuna Waziri alichukua fedha unasema alijua kuwa ni chafu, lakini hawakuwasikiliza.

" Kwa hiyo, wamehukumu bila kuwasikiliza na wamependekeza hatua za kuchukua. Baadhi yao wamesema wachukuliwe hatua za kinidhamu na wengine walipe kodi. Najiuliza kama askofu amepewa fedha, unasimama kwenye bunge unasema ajiandae kulipa kodi, najiuliza hivi ni mara ya kwanza kwa wao na watu wengine kupata fedha za aina hii? Mbona viongozi hao hao wanatoa misaada tena mikubwa na mahali pengi, mamilioni hatujasikia wakisema waliopewa walipe kodi.

" Hivi tuna uhakika gani kwamba hizi site zinazochangwa ni halali? Kwanini hawa ndio walipe kodi lakini zinazotolewa na wanasiasa husemi zilipiwe kodi.
Nadhani bunge halikutumia madaraka yake sawasawa. Unamwambia rais aunde tume ya kuwachunguza majaji walipata fedha, anaunda tume kwa msingi gani?

"Kwa sababu sheria inasema yakiwapo malalamiko kuhusu jaji, rais ataunda tume. Sasa hapa bunge linampelekea malalamiko gani yatakayomfamya aunde tume. Bunge lina ushahidi gani kwa sababu halikuwasikiliza ili kusema kuna malalamiko? Hilo nadhani bunge limeingilia mambo yasiyolihusu, ingekuwa haki kwamba hujatamka hatua gani zichukuliwe wangepata maelezo kutoka kwa wote wanaohusika ndipo ubaini kama kuna shaka ndipo uchukue hatua.....

Na Ester Mvungi, Dar es salaam
 
Back
Top Bottom