Nauliza tu kwa nia njema kwa sababu malezi yana maana pana.
Mara ya mwisho nilimuona msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Mutungi kwenye mkutano mkuu wa CCM.
Baada ya hapo amekuwa akiwakilishwa na msaidizi wake mh Nyahoza katika Mikutano yote ya Vyama vya Upinzani iliyofuatia huku akitoa udhuru kuwa msajili ana majukumu " muhimu"
Hali hii sikuwahi kuiona kwa msajili mstaafu Jaji Tendwa ndio maana nauliza labda kanuni na taratibu zimebadilika.
Kuna uzito wa pekee pale msajili " mwenyewe' anapohudhuria mikutano hii na kutoa nasaha kama mzazi badala ya kumtuma baba mdogo.
Jambo moja nina hakika nalo ni kuwa Mutungi hajawahi kufanya kazi kiuweledi wala busara. Uzoefu wangu wa kuwa naye karibu Dodoma miaka hiyoo,unaonyesha hana uwezo wa chochote kinachohitaji werevu, weledi, akili na busara.