Jairo ajiuzulu wadhifa wake

Status
Not open for further replies.
Kwa hii kitu sidhani kama hatapona ni ngumu mno kumeza , maana hata account namba aliyofanya mamboz inajulikana
kama wanataka kufanya cover up itakuwa mbaya zaidi

View attachment 34161



ngoja tumsubilie kikwete kama anaweza kufunika na ili
 
KWA UMBUMBUMBU HUU WA MAGAMBA, SIPATI PICHA 2015 KUTAKUWAJE, BILA SHAKA PATACHIMBIKA, Eee, Mola nijalie japo nione kitakachotokea 2015.
 
Pinda kakanusha anasema labda jairo kaipeleka hiyo barua kwenye vyombo vya habari lakini sio kwake hivo anamsubiria JK Atue bongo kutoka kwa madiba ndio ataamua ila yeye na ofisi yake hana taarifa yeyote TBC News imerushwa muda sio mrefu

Kwani Kikwete hajatua? Mbona nimesikia habari zake zinazohusi wawekezaji kwenye taarifa ya saa 7 mchana ikionyesha hiyo kauli kaitoa leo asubuhi akiwa nchini?
 
Inasemekana TZS 1bn/- zimekusanywa, tukichukua idadi ya wabunge 320 kila mmoja angelamba 3.125m/-, Loo! Aibu sana. Mapato haramu kabisa!

toa wa CHADEMA NA VYAMA VYA UPINZANIA bakiza cheyo tu
ndiye anayeza kuaminika, hisitoshe walengwa walikuwa ni ccm maana kama wao
wakisema ndio basi bajeti imepita wapindhani na mawaziri hawapo kwenye huo mgao
hivyo mgao ni mkubwa zaidi ya hiyo 3.125 milioni
 
tatizo serikali yenyewe ya ki..pu...zi haiwezi kuwa na maamuzi yenye akili
 
Naamini sikio la chief ni kubwa, hapa JF tuna machief wengi tena sana. Ombi langu ni kwa yeyote mwenye nakala ya barua aliyoandikia Mh Jairo kuzitaka taasisi na Idara zilizopo chini ya wizara ya nishati na madini kutumbukiza fedha kwenye account husika atuwekee hapa JF tupate kuisoma in detail.
Shukrani.
 
Amtume waziri wa mambo ya njee na akina boys 2 man atawatunza nani wakati yeye jk ni mshika dau wa good time...? membe yuko kwa ajili ya kujibu kashfa za njee na sio kuiwakilisha nchi...Pinda nae ni kibarakashia juu ya kapero...JK ni kila kitu balozi yeye, raisi yeye, waziri yeye, gavana yeye, hata kazi ya balozi wa nyumba kumi ingewezekana angewakilisha yeye...bahati yake agombei tena
Jamaa ameshindwa hata kukopi and paste from Mkapa. Wakati yeye Kikwete akiwa ni waziri wa mambo ya nje, safari nyingi za nje alikuwa anakwenda yeye, Mkapa alimwamini kama mwakilishi mzuri wa taifa (japo wakati mwingine inasemekana alikuwa anaacha mikutana na kwenda kujirusha na vimada). Lakini cha kushangaza yeye leo kamteua Membe kuwa waziri wa mambo ya nje, halafu mambo yote yanayohusiana na mambo ya nje anafanya yeye!! Membe ni kama sanamu tu. Kikwete ni kama hamuamini yeyote. Na hilo ndilo linalowapa wakati mgumu mawaziri wake katika suala zima la kufanya maamuzi na kufanya kazi kwa ubunifu. Kikwete ni zero kabisa.
 
Hakuna jipya kwa wadanganyika ndugu yangu ni sisi tunao tumia mitandao ndio tunajua mbivu na mbichi ila vijijini ndio wanatuua kwa kanga na kofia.
kwa umbumbumbu huu wa magamba, sipati picha 2015 kutakuwaje, bila shaka patachimbika, eee, mola nijalie japo nione kitakachotokea 2015.
 
Kwa hii kitu sidhani kama hatapona ni ngumu mno kumeza , maana hata account namba aliyofanya mamboz inajulikana
kama wanataka kufanya cover up itakuwa mbaya zaidi

View attachment 34161



ngoja tumsubilie kikwete kama anaweza kufunika na ili

Duh, sasa PCCB na Hosea sijui watasingizia nini. Kumbe mambo yote yalifanywa officially na ushahidi uko kwenye papers?? Kuna haja ya kuzichunguza wizara zote. Kuna haja ya waziri na naibu wake pia kujiudhuru, possibly hata wakurugenzi.
 
Sio lazima iainishwe kuwa ni rushwa, huo utaratibu sio rasmi that why Jairo anashutumiwa, Hata kama jambo hili linafanywa kitambo hiyo siyo tija, imejulikana rasmi kupitia Jairo na aliyekamatwa na nyama ndiyo mwizi wa kuku ila uwizi huu ni organized crime so tunahitaji adhabu kwa wote waliohusika kuorganize hii crime.
 
Kila jambo lina wakati wake mwana wa Mkulima hana chochote kwani naye ni Golipicha tu hana power kama alivokuwa mtanguliz wake alomrithi yeye alikuwa action ontime.Ngoja tusubiri bosi wake arudi labda atakuwa na say baada ya kuambiwa kaseme hivi
 
tumwacheni nae JAIRO astaafu kwa heshima kama tulivyozoea kwa viongozi wengine waliostaafu kwa heshima kwa makosa waliofanya.
kumshindikiza jairo aadhibiwe hatumtendei haki

kila la kheri...................
 
..I wish tungeelekeza nguvu zetu ktk ku-recover mapesa yaliyochangishwa na Jairo.

..pia ktk barua yake Jairo amebainisha kwamba huu ni utaratibu wa muda mrefu ambao umekuwa ukifanyika ktk kupitisha bajeti za wizara hiyo.

..kama wapo watu walikuwa wakicheza mchezo huu miaka ya nyuma ni vizuri na wao wakachukuliwa hatua.

NB:

..sijui kama mnakumbuka yale madai yaliyotolewa na Januari Makamba kuhusu wajumbe wa kamati ya Nishati na Madini kupewa mamilioni ya pesa kwa ajili ya lunch.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom