SEPTEMBER 2015,
Nyota wa filamu nchini, Jacqueline Walper Massawe ‘Wolper’ amemchana staa mwenzake, Chuchu Hans kufuatia kutofautiana kiitikadi kisiasa kati ya chama tawala (CCM) na Ukawa.
Awali, Chuchu Hans na wasanii wenzie walitangaza kuhamia Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi) na kushiriki kikamilifu kwenye uzinduzi wa kampeni uliofanyika katika Viwanja vya Jangwani, Dar wiki iliyopita. Lakini ghafla, Chuchu alionekana akiwa amevaa sare za Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kutangaza kwamba ameamua kurudi nyumbani, kitendo kilichoonekana kumkera mno Wolper.
Wolper akizungumza na mwandishi wa habari hizi alisema “Sijui huu uzalendo wa Tanzania utakuja lini, yaani huyu Chuchu juzi tuwe wote na sare amevaa, leo umetusaliti kisa vijisenti. Sasa aliyemwambia kwamba UKAWA tunapewa hela ukaja na mbwembwe zote nani? UKAWA hatupewi hela, huku ni uzalendo tu. Wenye tamaa ya pesa ndio wanarudi CCM"
JULY 2016
Msanii wa Bongo Movie, Jacqueline Walper usiku wa leo ameamua kurejea Chama cha Mapinduzi na kumkimbia aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa.
Walper ambaye alizunguka mikoani kumnadi Lowassa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 amewaomba radhi wafuasi wa CCM akidai aliteleza tu pale alipoamua kukipigia debe Chadema kipicha hicho cha uchaguzi.