JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Licha ya Timu ya Taifa ya Ivory Coast kucheza pungufu kuanzia kipindi cha kwanza dhidi ya Mali katika Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, bado hiyo haikuwa kikwazo cha kuingia Nusu Fainali kwa kushinda magoli 2-1, Februari 3, 2024.
Ivory Coast ilimpoteza Odilon Kossounou aliyepata kadi nyekundu dakika ya 43, kisha Nene Dorgeles akaipatia Mali goli dakika ya 71, wenyeji wakasawazisha dakika ya 90 kupitia kwa Simon Adingta, baada ya hapo Oumar Diakite akafunga la pili katika dakika za 30 nyongeza (120).
Hivyo, Ivory Coast itacheza dhidi ya DR Congo katika Nusu Fainali, Februari 7, 2024.
Ivory Coast ilimpoteza Odilon Kossounou aliyepata kadi nyekundu dakika ya 43, kisha Nene Dorgeles akaipatia Mali goli dakika ya 71, wenyeji wakasawazisha dakika ya 90 kupitia kwa Simon Adingta, baada ya hapo Oumar Diakite akafunga la pili katika dakika za 30 nyongeza (120).
Hivyo, Ivory Coast itacheza dhidi ya DR Congo katika Nusu Fainali, Februari 7, 2024.