FT: Nigeria 1-2 Ivory Coast | 2024 AFCON Final | Stade Alassane Outtara | 11.02.2024. Ivory Coast abeba ubingwa

Teko Modise

JF-Expert Member
May 20, 2017
1,914
6,029
Majira ya Saa 5:00 Usiku kutapigwa mchezo wa Fainali ya AFCON 2024 ambapo Nigeria atawavaa wenyeji Ivory Coast.

Ni mchezo unaovuta hisia za wengi hasa kutokana na viwango vya timu zote mbili. Nigeria ikionekana ni timu iliyokamilika huku Ivory Coast unyumbani ukiwasaidia.

Kura yako unampa nani kuibuka na ubingwa?

Tukutane hapa kuanzia saa 5 usiku, huku mechi ikiwa mubashara Azam Tv, Star Times, DStv.

=========

Timu ya Taifa ya Ivory Coast imefanikiwa kubeba ubingwa wa Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) kwa kuifunga Nigeria magoli 2-1 katika Fainali, ikiwa ni ubingwa wao wa tatu kutwaa baada ya kufanya hivyo Mwaka 1992, 2015 na sasa 2024.

Licha ya Nigeria mbayo imetwaa kombe hilo mara 3 kutangulia kufunga kupitia kwa William Troost-Ekong dakika ya 38, wenyeji wa michuano hiyo walipambana na kusawazisha kupitia kwa Franck Kessié dakika ya 62 kisha kuongeza la pili dakika ya 81 mfungaji akiwa ni Sébastien Haller.

Ivory Coast ilianza michuano hiyo kwa kusuasua, ikipita katika Kundi A kuendelea na Hatua ya Mtoano licha ya kushika nafasi ya Tatu.
GGFm3rPW4AAhIby.jpg

GGFnAsOXQAAFVHt.jpg
 
Nikiongelea ubora na uwezo wa team ni nigeria,, wanaweza kuwa quality kwenye sehemu zote ila kwenye mchezo huwa kuna kitu bahati so nikiongelea bahati ivory coast ana bahati na tofauti yake kuna team inaweza kushinda kwa uwezo na kuna team inaweza kushinda kwa bahati mi nampa mwenye bahati ivory coast.
 
🇳🇬🇳🇬🇳🇬🇳🇬🇳🇬🇳🇬🇳🇬🇳🇬
 
Niko na Didie hapa anasema madogo hadi walipiga nao mazoezi kuwahamasisha kujitahid ila nikama wamezingua ngoja tuone watafanyaje
 
Majira ya Saa 5:00 Usiku kutapigwa mchezo wa Fainali ya AFCON 2024 ambapo Nigeria atawavaa wenyeji Ivory Coast.

Ni mchezo unaovuta hisia za wengi hasa kutokana na viwango vya timu zote mbili. Nigeria ikionekana ni timu iliyokamilika huku Ivory Coast unyumbani ukiwasaidia.

Kura yako unampa nani kuibuka na ubingwa?

Tukutane hapa kuanzia saa 5 usiku, huku mechi ikiwa mubashara Azam Tv, Star Times, DStv.
Mbona we umetuacha
 
Back
Top Bottom