Wenyeji wa AFCON, Ivory Coast wamekubali kupigwa na wamepigika, wachapika 4-0

balibabambonahi

JF-Expert Member
Apr 5, 2015
14,458
12,584
Tuwaombeetu lakini mwenyeji sijui anapigaje

========

WENYEJI WA AFCON, IVORY COAST WAMEKUBALI KUPIGWA NA WAMEPIGIKA

Wenyeji wa Michuano ya Kombe la Mataifa ya Africa 2023 (AFCON), Timu ya #IvoryCoast imeishia Hatua ya Makundi baada ya kukubali kichapo cha magoli 4-0 kutoka kwa Equatorial Guinea ambayo imeingia Hatua ya 16 Bora toka Kundi A, leo Januari 22, 2024.

Timu nyingine iliyosonga mbele katika Kundi hilo ni Nigeria ambayo imeifunga Guinea-Bissau goli 1-0

Hivyo, Msimamo wa Kundi A ni Equatorial Guinea pointi 7, Nigeria (7), Ivory Coast (3) na Guinea-Bissau (0)
 
Mpfyuuuuuuuuuuuu Mpfyuuuuuuuuuuuu Mpfyuuuuuuuuuuuu Mpfyuuuuuuuuuuuu Mpfyuuuuuuuuuuuu Mpfyuuuuuuuuuuuu Mpfyuuuuuuuuuuuu
 
Nani alitarajia Equatorial Guinea kuipopoa Ivory Coast kikatili namna hii? Goli 4 kwa 0?

Jibu ni HAKUNA ila ukweli ni kwamba mpira ni mchezo wa plan, akili, nidhamu ya mchezo na juhudi za jasho na damu kitu ambacho wachezaji wa Equatorial Guinea wamekionesha uwanjani kwa vitendo 100% achana na wale wahuni wanaotamka uzalendo na kupigania nchi mdomoni ila uwanjani ni miso Misondo watupu
View attachment 2879901
 
Wenyeji Ivory Coast katika hali ya kushangaza wamefungwa goli 4-0 dhidi ya Equtorial Guinea.

Kwa matokeo hayo yanawafanya wenyeji kuwa katika hati hati ya kuondoshwa mashindanoni.

Ivory Coast wanashika nafasi ya 3 baada ya kushinda mechi moja na kufungwa mbili.
IMG_9546.jpeg


Katika mchezo mwingine wa kundi A, Nigeria imeibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Guinea Bissau.
 
Back
Top Bottom