Uchaguzi 2020 Itakuwaje kama Lissu akashinda Urais bila kupata Wabunge wa kutosha?

Subiri tumnyooshe naona nawewe hupendi yanafanywa nahuyu jamaa ilatatizo haupo huru
Mimi napenda sana ambayo yananihusu mengi kayafanya. Nina watoto wangu wawili nilikuwa nawasomesha shule ya kulipia milioni 2 kila mwaka. Lakini Sasa nimewahamishia shule ya serikali natumia laki3 tu kwa kuwagaramia uniform na matumizi binafsi wanapokuwa shule.
 
Sehemu zote walizopita mafisiem bila kupingwa lazima uchaguzi urudiwe hatuwezi kukubali kuongozwa na watu ambao hawakuchaguliwa.

Nb:Uwezekano wa kuitoa CCM kwa sanduku la kura hata kama tumepata kura zote haupo lazima Wananchi tuingilie kati.
 
Ataunda baraza lake la mawazili, CCM itabid wakubali tuu kwa sababu kama watamgomea waziri mkuu mteule Mara 3 bunge litavunjwa, likivunjwa CCM itapoteza hata hao wabunge watakaokuwa wamewapata wakati chadema wakinufaika kwa sababu system ya nchi itakuwa upande wao
Bunge likivunjika, raisi nae anapaswa kuachia ngazi.
Hapo uchaguzi unakuwepo kuanzia raisi Hadi wabunge..
 
Je hakuna uwezekano wa kuingia madarakani na kulivunja bunge kabla hajateua waziri mkuu na uchaguzi ukaitishwa upya ili apate wabunge wanaoweza kuunda serikali?
Akivunja bunge, yampasa kuachia madaraka , achaguliwe upya.. Ina maana uchaguzi wa raisi na wabunge utaitishwa upya..
 
Mna maana gani? Kama siyo NEC na upenfeleo wa wazi cvm ingekuwa wapi!
Mtanzania anayechagua ccm ambayo imetumia fedha za nchi kihovyo kama walivyofanya hii miaka mitano hawastahili kuitwa watanzania!
Mkuu amesema, kama chama kinakosa angalau asilimia sabini ya wabunge , raisi anakuwaje ameshinda katika mazingira ya Tanzania..
 
Tanzania ni nchi ya Mfumo wa vyama vingi hata yule mama anayegombea Uraisi akishinda bila mbunge mmoja bado atachagua mawaziri na waziri mkuu kutoka kwenye vyama vyenye wabunge na watamsapoti kinafiki au kiupendo ni kulingana tu na uwezo wa mtu wa kuongoza kwa umoja na upendo na huwa havijifichi kama unafiki usivyojificha.
CCM Lisu anao marafiki wengi mno lakini hujificha kwa hofu ya kaburu Mkoloni mweusi kuwafanyizia
 
Propaganda za kujifariji. Mwenyemacho ambiwi tazama na mwenyemasikio asikie. Ngome za CDM zote zimebomoka.
CCM bila uchakachuaji bila wizi wa kura bila Polisiccm bila Tumeccm bila mahakamaccm bila wakurugenziccm bila Msajiliccm ni weupe sana
 
Kama unaamini Wabunge was CDM hawatashinda, kwa angalau 70% huo ni ushahidi kuwa Lissu naye atashindwa.
Watanzania wenye uwezo was Kumchagua Mbunge was CCM na Wakamchagua Lissu ni wachache japo 2015 Mimi nilifanya hivo. Nilimchagua Mama Anna Mgwilla na Halima Mdee. Lakini ninachojua asilimia 99% ya Watanzania wanapenda kupiga hatrick.
Kuna ujinga ulifanywa na NECCCM Tumeccm kuwakata wagombea wa chadema kwa kisingizio cha CCM kupita bila kupingwa kwa njia haramu za kishetani, wananchi wamekosa fursa ya kuchagua wamechaguliwa watu kwa nguvu na NECCCM Tumeccm kwa njia haramu za kishetani
 
Sehemu zote walizopita mafisiem bila kupingwa lazima uchaguzi urudiwe hatuwezi kukubali kuongozwa na watu ambao hawakuchaguliwa.

Nb:Uwezekano wa kuitoa CCM kwa sanduku la kura hata kama tumepata kura zote haupo lazima Wananchi tuingilie kati.
Ni Hatari kuwa mbunge ambaye siyo chaguo la wapi kura
 
1)Tunafungua kesi mahakani nchi nzima
.kuwaondoa wabunge wa ccm waliopitishwa kwa rushwa kwenye kura za maoni, uchaguzi utarudiwa

2.) Tutarudia uchaguzi majimbo ambayo waliopitishwa bila kupingwa

3). Tutawafuta wabunge wote ambao ushindi wao umepatikana kwa figisu ikiwa Ni pamoja na kukiukwa kwa sheria na kanuni za uchaguzi

No1-4 tuta fanikiwa kurudisha majimbo kama100 kabla ya december 2020

4 tutaunda serikali ya mseto na ACT wazalendo
Dah Ndio mnataka nchi nyinyi yaani hamshindi hata kwa Ndoto ni Maruku kuota Lissu kashinda
 
Mimi napenda sana ambayo yananihusu mengi kayafanya. Nina watoto wangu wawili nilikuwa nawasomesha shule ya kulipia milioni 2 kila mwaka. Lakini Sasa nimewahamishia shule ya serikali natumia laki3 tu kwa kuwagaramia uniform na matumizi binafsi wanapokuwa shule.
Sasa mimi nimemchukia kwasababu amechoma nyavu zangu 2 na ameteka engeine zangu mbili za boat anasema nikazininue kwake wakati nyavu zangu nihalali zilikuwa nazilipia leseni nawachomaji walisema zipo sawa lakini wao wametumwa pesa kama sina wanazichoma yote haya yamemuumiza hata lisu kasema anatulipa
Nasomesha watoto 4 wawili wapo chuokikuu 1college afya 1form 5 napata taabu kwajili yammtu kujidaia madaraka alikuwa amefanya makubwa lakini yameharibiwa na kiburi kujidai madaraka yanampa uwezo wakujiona yeye ndio mungu achagui lolote anakuchapa nalo
 
Watanzania Leo Kuna jamaa yangu kaniambia yupo kwenye usimamizi wa uchaguzi

Sasa semina Yao ya siku mbili iliyoanza leo wamepewa 80000/=

Chakushanga maneno waliyoambiwa kwamba presha huku nje ipo kubwa sana kwaiyo ikiwezekana kuua wakala waue tu ili mradi Maghufuri ashinde.

Kwanza walitolewa wote ambao walifatiliwa habari zai zikaonekana zinavinasaba vya upinzani.

Jaman tuweni makini uchaguzi huu ni hatari sana Kuna watu wapo tayari kuwa ili Meko ashinde usimwamini mtu.

Haki huinua TAIFA

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Ni dhahiri shayiri kuwa uchaguzi huu umekuwa mgumu sana kwa CCM kuliko miaka yote. Mwaka 95 ulikuwa mgumu ila hayati Mwl. Nyerere alikuwepo kuokoa jahazi, na mwaka 2015 ulikuwa mgumu ila Mkapa alikuwepo kuokoa jahazi.

Mwaka huu sijaona wa kuokoa jahazi, hata hao wastaafu waliingizwa kwenye kampeni wamekosa mvuto tofauti na ilivyotarajiwa.

Swali langu ni kuwa: Itakuwaje kama Lissu akashinda kisha akakosa kupata wabunge wa kutosha? Si CCM wataamua kumkwamisha?
Jamaa hebu acha bange basi. Urais wa wapi?

Muulize tu hata urais wa TLS alifanya nini cha maana.

Sembuse urais, hapati hata wabunge 10 wa majimbo.
 
Atakuwa na option mbili
1.kufanya maridhiano na chama tawala ili aunde serikali kwa serikali ya mseto
2. Kutumia mahakama kutengua wabunge wote waliopita bila kupingwa ili kukiongezea wabunge chama chake kisha kuendelea na kazi ya kujenga nji
Kama ni stori za gahawa kusubiria 28 Oktoba sawa.

Ila huyo simuwazii hata kama angeenda jimboni au kata kugombea ubunge au udiwani bado alikuwa anapigwa mchana kweupe.


Ndio kajiandaa kabisa na tiketi ya kurudi kwa mabwana zake
 
Kama ni stori za gahawa kusubiria 28 Oktoba sawa.

Ila huyo simuwazii hata kama angeenda jimboni au kata kugombea ubunge au udiwani bado alikuwa anapigwa mchana kweupe.


Ndio kajiandaa kabisa na tiketi ya kurudi kwa mabwana zake
Wewe ndiyo upo kwa bwawa yako cyprian Musiba anakudanganya hivyo?
 
Jamaa hebu acha bange basi. Urais wa wapi?

Muulize tu hata urais wa TLS alifanya nini cha maana.

Sembuse urais, hapati hata wabunge 10 wa majimbo.
Kama magufuli mtesi muonevu aliyeuza nyumba za Serikali akagawa nyumba kwa hawala yake akanunua kivuko kibovu cha Dsm Bagamoyo na kupiga bilion 252 wizara ya ujenzi kwa kuwalipa makandarasi hewa kawa Rais sembuse mtu mpenda haki kama Tundu lisu?
 
Dah Ndio mnataka nchi nyinyi yaani hamshindi hata kwa Ndoto ni Maruku kuota Lissu kashinda
Wewe hurejei ikulu hata kwa ndoto na wewe ni marufuku hata kuwazia Urais subiria uhuru tarehe 28 CCM bye bye Mkoloni kaburu mweusi mtesi muonevu anarejea kijijini chato
 
Mimi napenda sana ambayo yananihusu mengi kayafanya. Nina watoto wangu wawili nilikuwa nawasomesha shule ya kulipia milioni 2 kila mwaka. Lakini Sasa nimewahamishia shule ya serikali natumia laki3 tu kwa kuwagaramia uniform na matumizi binafsi wanapokuwa shule.
Je wanasoma na kupata maarifa huko shuleni au wanaambulia masimango na vipigo toka kwa waalimu?
 
Back
Top Bottom