Ni dhahiri shayiri kuwa uchaguzi huu umekuwa mgumu sana kwa CCM kuliko miaka yote. Mwaka 95 ulikuwa mgumu ila hayati Mwl. Nyerere alikuwepo kuokoa jahazi, na mwaka 2015 ulikuwa mgumu ila Mkapa alikuwepo kuokoa jahazi.
Mwaka huu sijaona wa kuokoa jahazi, hata hao wastaafu waliingizwa kwenye kampeni wamekosa mvuto tofauti na ilivyotarajiwa.
Swali langu ni kuwa: Itakuwaje kama Lissu akashinda kisha akakosa kupata wabunge wa kutosha? Si CCM wataamua kumkwamisha?