Israel yarudisha majeshi nyuma kutoka Rafah na katikati ya Gaza. Hii ina maana gani

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,208
10,965
Ikiwa ni miezi sita kamili tangu vita vianze baina ya Hamas na Israel,na baada ya vifo vingi vya raia na askari wa Israel,na baada ya Israel kuwaudhi washirika wake, hatimae leo jeshi hilo limeamua kurudisha nyuma vikosi vyake kutoka kusini ya Gaza na Rafah.

Baadhi ya taarifa zinaeleza kuwa maelfu ya askari wanaorudi nyuma ni wale ambao wameamua kukimbia vita kurudi nyumbani.

Katika maelezo yake Israel kupitia redio ya channel 2 , imesema inarudisha nyuma jeshi kutokana na kukamilisha majukumu yao na kwamba Gaza nzima imeachwa na brigedi moja tu ambayo kazi yake kubwa itakuwa ni kuangalia uzio ambao umewekwa ili kuzuia wapalestina waliokimbilia kusini wasirudi tena kaskazini ya Gaza.

Itakumbukwa kuwa waziri mkuu wa Israel.Benjamin Netanyahu mwanzoni alisema lazima mateka wapatikane kabla ya Ramadhani ama sivyo hakuna kingemzuia kuingia Rafah.Hata hivyo mwezi umeisha na Hamas hakurudisha hata mateka mmoja.

Na vile vile wakati mwezi wa Ramadhani ukikaribia kuisha idadi ya vifo vya askari wa IDF kwenye maeneo yale yale Israel iliyojitangazia ushindi vimekuwa vikiongezeka sana kutokana na kuongezeka kwa mapigano.

Kurudishwa kwa vikosi hivyo kumeleta sherehe kwa wapalestina na pia kuleta kuchanganyikiwa kwa baadhi ya wafuatiliaji wa vita hivyo.

Chanzo: Aljazeera.
 
images (1) (1) (1).jpeg
 
anaenda kujiandaa na vita dhidi ya Iran! middle east patachafuka this time.
 
Muislam hapotezi kitu. Akikua au akiuliwa kwake ni faraja akiwa anatetea mali yake au ardhi yake.
 
Benyamin Netanyahu ngoma imekua ngumu kwake kuanzia ndani ya nchi mpaka nje ya nchi...ikimbukwe Israel ni nchi ambayo inapewa silaha na kununua silaha nyingi toka mataifa ya nje kuliko wengi wetu tunavohisi... Vifo vinazidi kuongezeka toka kwa Hamas na Islamic jihad bado Hezbollah ambae ana makombola mengi kuliko ata baadhi ya nchi ya ulaya kila siku wanashambuliana na kupelekea maelfu ya wayahudi wanaishi jilan na Lebanon kuhamishwa.

Bado Wa Houth wanaendelea na kuzuia meli zinazoelekea Israel hivo kupelekea uchumi wa Israel kuyumba sana... Bado kuna vikundi vya Irak vinavyosapotiwa na Iran vikiendelea kurusha Drone mpaka bandar ya Eliat uko Israel...Kosa kubwa alilolifanya Israel ni kushambulia Jengo la makaz ya ubaloz (consulate) la Iran na Iran kuapa kulipiza kisasi hii imepelekea presha kua kubwa kwa Israel kua muda wowote tutashambuliwa na Iran.

Sasa hajui lengo lake lilikua ni HAMAS apa kapoteza direction wayahud wameanza kupelekwa kwenye mahandaki ikitokea Iran watashambulia, Wayahud wanaandamana wakitaka Netanyahu atoke madarakan na Uchaguz ufanyike.

Jana Biden kaongea na Netanyahu wadadis wanahis Biden kamwambia umekosea sana kushambulia consulate ya Iran maana US yuko Syria sio kwakingine ni kuilinda Israel maana Iran alishaunda Land corridor from Iran to Syria to Lebanon na Israel ilishaapa haitakubali Iran iunde kundi lingine uko Syria ambalo litaizunguka Israel... Angalia Yemen kuna Houth angalia Lebanon kuna Hezbollah angalia Irak kuna PMU na angalia jinsi makundi ya Irak yanavyoisumbua US forces.
 
Trap hiyo kama al shifa.. Hasam lazima waingizwe king tena... IDF wamekaa tu ila kikosi kimoja kimeachwa like chambo.

News kutoka kwa IDF preparation now ya Rafah inaanza Hamas kaeni mkao wa kwenda choo
 
Back
Top Bottom