Zee la madawa
JF-Expert Member
- Nov 28, 2022
- 1,878
- 4,427
Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel imetangaza kuandaa tamasha kubwa la jamii ya LGBTQ+ (mapenzi ya jinsia moja) linalofahamika kama "Pride Land," ambalo linatarajiwa kufanyika katika fukwe za Bahari ya Chumvi mwezi Juni.
Tukio hilo limetajwa kuwa tamasha kubwa zaidi la aina yake kuwahi kufanyika katika kanda ya Mashariki ya Kati, likiwaleta pamoja maelfu ya watu kwa ajili ya ushirikiano na sherehe.
Tamasha hilo litadumu kwa muda wa siku nne mfululizo katika eneo la Bahari ya Chumvi, litaanzia tarehe Moja mwezi wa sita mpaka tarehe 4, Picha za tangazo hilo zinaonyesha umati wa watu wakiwa wamebeba bendera za taifa la Israel sambamba na bendera za rangi ya upinde wa mvua, huku kukiwa na jukwaa kubwa la muziki lililopambwa kwa rangi za kisherehe ufukweni.
Hii Ina leta tafsiri Gani?
#fblifestyle
Tukio hilo limetajwa kuwa tamasha kubwa zaidi la aina yake kuwahi kufanyika katika kanda ya Mashariki ya Kati, likiwaleta pamoja maelfu ya watu kwa ajili ya ushirikiano na sherehe.
Tamasha hilo litadumu kwa muda wa siku nne mfululizo katika eneo la Bahari ya Chumvi, litaanzia tarehe Moja mwezi wa sita mpaka tarehe 4, Picha za tangazo hilo zinaonyesha umati wa watu wakiwa wamebeba bendera za taifa la Israel sambamba na bendera za rangi ya upinde wa mvua, huku kukiwa na jukwaa kubwa la muziki lililopambwa kwa rangi za kisherehe ufukweni.
Hii Ina leta tafsiri Gani?
#fblifestyle