Israel inaomba silaha!!

ni makosa kuilinganisha marekani na israeli, mmarekani ni wa kumlinganisha na mchina na mrusi labda na nato
 
nchi ambazo kamwe marekani haitazisahau katika medani ya vita ni: cuba na bay of pigs; vietnam na saigon , japan na kamikaze pearl harbor, urusi na missile crisis enzi za sputnik, somalia na black hawk down, afghanistan na kandahar
 
Nikubaliane na mwenzetu aliyetofautisha kati ya nguvu za kijeshi (military power) na ushawishi (influency).
Waisrael wapo wachache sana katika taifa kama la Marekani na hawawezi kuathiri mwenendo wa uchaguzi kwa kura.
Kinachotisha wanasiasa ni ushawishi wao (influency) unaotokana na matajiri ambao kwa mkakati kabisa wamemiliki vyombo vya uchumi na habari. Kwahiyo ushawishi wao ni mkubwa sana kutokana na nguvu hizo mbili.

Marekani inawahitaji sana Waisrael si kwasababu ya nguvu za kijeshi bali mshiriki muhimu sana(ally) katika eneo la mashariki ya kati. Israel inazijua vizuri nchi za mashariki ya kati kwa kupitia MOSAD ambayo ni sehemu muhimu sana ya kazi za CIA.

Mwaka jana Marekani iliipatia Israel msaada wa kijeshi wa Dollar bilioni 10 ikiwa ni pamoja na kuwapa Technology ya kuzuia makombora ya Wapalestina (Katush) yaliyoonekana kutoweza kukabiliwa na technology ya anti-missile. Katushi ni kitu tofauti na missles kwani yametengenezwa uani na hayana uelekeo, ingawa madhara yake ni 100% yakitua mahali.

Vita ya mwaka 1967 na zingine, Israel haikufanikiwa bila msaada wa Marekani. Kwahiyo si sahihi kudhani walifanya mambo bila baraka za White house.

Israel ni tegemezi sana kwa nchi za Magharibi hasa katika maazimio ya UN. Katika siku za karibuni nchi za EU zimeanza kuitenga Israel na mshirika wake mkubwa amebaki kuwa US.

Funzo la vita vya Hisbollah linaitia kiwewe Israel kwasababu pamoja na uthabiti wa teknolojia bado vita ile Israel ilionekana kushindwa kabisa na hata wenyewe wamekiri hivyo kwa kupitia tume waliyounda. Hisbollah ni mshiriki mzuri sana wa Iran na hiyo inaonyesha nguvu aliyo nayo Iran.

Watu wasisahau kuwa kama kuna nchi Israel inaiogopa ni Syria. Hakika mgogoro unaoendelea ni faraja kubwa kwa Israel.
Syria sio wazuri wa teknoloji ila ni 'warriors' wanajua mbinu za vita. Ndiyo maana Israel kamwe haitaachia Milima ya Golan ili kumdhibiti Syria.

Ni makosa kupima nguvu za Israel kwa kuwaangalia Wapalestina. Wapalestina hawana chochote zaidi ya mawe na madongo. Kama kuna kitu Waisrael wasichokitaka ni kuona Mpalestina anapata silaha maana wanajua kazi itakuwa ngumu sana.

Ni ukweli kuwa teknolojia yao ya kijeshi ni kubwa sana kwasababu ya usalama wao, lakini hiyo haitokei bila msaada mkubwa sana kutoka Marekani, na Israel haiwezi kusimama bila msaada wa Marekani. Na wala haiwezi kusimama kama nchi yenye nguvu za kijeshi kuliko mataifa kama China na Urusi.
 
Imeandikwa kuwa, kila atakayeilaani Israel atalaaniwa, na kila atakayeibariki atabarikiwa. Endeleeni kupata laana na warabu wenu. Poleni sana.

Taifa la israel linalozungumziwa kwenye biblia ni wale wacha mungu wote pasipokujali huyu ni muha, msukuma au muyahudi. Tatizo mtu akisoma biblia anachukulia jinsi ilivyo bila kutafakari. Sasa kama ni Taifa teule basi wale waha wakigoma ni Taifa laaniwa na hamna hata haja ya kusali kwa sabab wote wataenda moton kasoro waisrael ambao wataenda mbigun hata kama walikuwa mashoga
 
Msimamo wangu wa kuchangia thread hii ni "Naunga Mkono hoja ya Nyani Ngabu. Huwezi kuwa huru iwapo wewe ni ombaomba.

... huyo Albeto eistein a; myahudi hivyo marekani inalipa fadhila mpaka kufa!
Imeandikwa wapi hiyo? Marekani ilipe fadhila kwa kichw kimoja cha kisayansi kwa miaka yote? Do your homework brother

...utake ustake uchumi wa marekani wameshika wao! wanatoa mfuko wa kulia wanaweka kushoto!
Mleta mada kasema mumpe ushahidi wa hizi nadharia, kwa sababu kuongea tu bila ushahidi haileti maana


.... Kwa Asilimia kubwa ISRAEL ana Marefa wengi sanaaaaaa
..Na hao marefa ndiyo wanaoifanya inaonekana ina ubavu wa kushindana katika vita, ilhali hali si kama hiyo. Kwa hoja hiyo, unakubali kwamba Israel bila 'kuomba omba' kwa marefa (Marekani na baadhi ya nchi za Ulaya) si lolote wala chochote. Iwapo Israel wameshindwa kutokomeza kikundi kidogo kisicho na serikali cha Hizbollah, kikiongozwa na Hassan Nasrallah, wataweza kweli kupigana na 'nchi' yenye uwezo wa kuleweka kivita?

....On the other side, Iran si wa kupuuzwa hata kidogo, na kuna karespect flani hivi wanapewa na haya mataifa, kwanza wanajuwa uwezo wao kupitia Hizbolah pamoja na Syria, Bashar amepewa msaada wa unmaned drones from Iran.Israel peke yake vs Iran itabidi wawe makini sana.
I second the idea.

Hakunaga MBABE kama Israel.
Pole sana. CNN na BBC inaonesha zimekuharibu sana.

Narudia, iwapo Israel wameshindwa kutokomeza kikundi kidogo kisicho na serikali cha Hizbollah, kikiongozwa na Hassan Nasrallah, wataweza kweli kupigana na 'nchi' yenye uwezo wa kuleweka kivita bila msaada wa nchi yoyote? Huwezi kuwa mbabe kama wewe ni ombaomba wa silaha toka kwa jirani. Nukta.

 
Hakuna kosa. Ila kuna watu humu bila hata soni eti wanasemaga Israel ni zaidi ya Marekani katika kila kitu ikiwamo uchumi, nguvu za kijeshi, influence, na kadhalika, kitu ambacho si cha kweli hata kidogo.

I agree with u 100%, i have been in & out of US mara
nyingi, did my Piloting there, na nimetembea nchi mbali mbali Israel unayosemea hadi Tel Aviv, Yerusalem, HUWEZI KAMWE MILELE YOTE KULINGANISHA MAREKANI NA NCHI YEYOTE ILE DUNIANI, hasa KIUCHUMI, TEKNOLOGY, KIJESHI, INA LAND KUBWA,
na hata KIDEMOKRASIA, na vitu nilivyo vitaja hapa VIPO OPEN, AMERICAN POWER CAN BE SEEN KWA MACHO,
wapo mbali, they are really powerful..... ukiangalia Airports, Railway, Roads, American Navy, American Air Force, Viwanda, Makaazi ya watu, Kilimo, Matibabu, Vyuo vikuu,
wapo mbali mno na kisayansi zaidi, security wise usiongee.....na ikumbukwe THERE ARE MANY ISRAELIS ambao ni wamarekani & have a powerful union AIPAC, ndio maana Israel wanasapptiwa na US bcoz of this guys, na ni matajiri haswa...... hiyo ndio US, inabidi uone, utembee ndio ujue US vizuri, HATA Mwingireza akienda US anajisifia katoka STATES bana.....
 
Kwa mtu asiyejua siasa za mashariki ya kati anaweza kushawishiwa na ulichoandika. Kumbe ni UTUMBO tu. Nani asiyejua kuwa Jeshi la Israel (IDF) ndiyo jeshi makini zaidi na committed kuliko jeshi la taifa lolote duniani including Marekani! Ukisoma historia ya IDF na mambo waliyofanya maeneo mbalimbali duniani utabaki kinywa wazi na kama una akili nzuri utajiuliza kama matendo hayo yalikuwa yanafanywa na binadamu au la. Ipo mifano mingi sana mojawapo ikiwa ni 90 minutes to Entebbe na kulipuliwa kwa ndege za kirusi zikiwa Egypt zikijiandaa kushambulia Israel. Endeleeni kujipa moyo kwamba Israel hakina kitu wakati mataifa yote ya kiarabu pamoja na hasira zao za kujitoa muhanga, wameshonwa mdomo na hawakohoi hata sekunde mbele ya wayahudi.

Bila msaada wa Ulaya na Marekani Israel itakuwa na wakati mgumu sana. Ukumbuke kuwa Ni Marekani na Russia waliowanusuru kutokana na chinja chinja ya Hitler.

IDF ni jeshi disciplined lakini si kweli kuwa IDF ni jeshi makini zaidi duniani, unless hujui majeshi ya dunia hii na kazi yalizofanya. Huwezi kuamini kuwa kikundi kinachoitwa Hamas (si jeshi) kinaweza kufanya operesheni ndani ya ardhi ya Israel na kuwaua askari wa IDF na hata kuwateka nyara, kuna kundi la Hizbolah linaweza kufanya same, kwa hiyo kusema ni jeshi makini zaidi unajidanganya au hujui unachosema, au hujui majeshi makini ni yapi, au utakuwa unaongea kama mlokole ambaye hajui anaongea nini zaidi ya Christian fundamentalism, ambaye hata ahjui kuwa Israel si nchi ya wakristo.

Unatakiwa kujua internal politics za Israel, na unatakiwa ujue how good is Israel for American strategic interests in the middle east. Bila msaada wa Marekani na Ulaya survival ya Israel ni ndogo sana. Survival of Israel ni muhimu sana kwa Europeans kwa kuwa they do not need more jews going to Europe, walijitahidi kuwaondoa na kuwatafutia nchi, they can not afford to have them back.

Nchi za kiarabu kama zikipenda, zinaweza kuwa mwiba mchungu kwa Israel, Israel si tatizo kwao na wao si tatizo kwa Israel. Kama Israel ingekuwa na uwezo wa kudeal na Iran isingeomba msaada kwa Marekani, kelele zote za sasa zinaonesha kuwa inahitaji msaada. Na ni vizuri ikisiaidiwa ili isijeangamia
 
Taifa la israel linalozungumziwa kwenye biblia ni wale wacha mungu wote pasipokujali huyu ni muha, msukuma au muyahudi. Tatizo mtu akisoma biblia anachukulia jinsi ilivyo bila kutafakari. Sasa kama ni Taifa teule basi wale waha wakigoma ni Taifa laaniwa na hamna hata haja ya kusali kwa sabab wote wataenda moton kasoro waisrael ambao wataenda mbigun hata kama walikuwa mashoga

Mkuu jaribu kutafuta mlokole yoyote kaa naye muulize maswali kuhusu Israel halafu umsikie, unaweza kuona hata huruma. Mpaka leo kuna watu wamejipa majina ya kiyahudi halafu wanajiita wakristo, kuna wengine wanasema Israel ni taifa teule na wanaona hata mataifa yao yamelaaniwa. Kibaya zaidi angalia hawa watu wanaoisifu Israel wanavyofanywa wakienda huko Israel kwenyewe, wengine wanatukanwa hadi utacheka. Unajua hili ndio tatizo la umaskini, Bible inapitkana bure kwa hiyo ndio source of education kwa walokole, bila kujali ni education ya mwaka gani. Wengine wanadhani hata waziri Mkuu wa Israel ni Musa, na waziri wa Fedha ni Yuda eskarioti.
 
Does this say anythings in relation to America and Israel ? Out of over Eigh hundred Nobel Prizes awarded to date 20% of the Nobel laureate are JEWS, although JEWS population comprise of only 0.2% of the world's population. kama Noble prize kwenye nyanja zote muhimu hawa jamaa wanazo wao,haina maelezo nyuma ya pazia kuonyesha kuwa wao ndiyo vinara wa technologia ya marekani ikiwa ni pamoja na uchumi wao ? wanaweza wakawa dhaifa kitechnologia ndani ya Israel lakini wana access na technolojia yao iliyoko Amerika...
 
Does this say anythings in relation to America and Israel ? Out of over Eigh hundred Nobel Prizes awarded to date 20% of the Nobel laureate are JEWS, although JEWS population comprise of only 0.2% of the world's population. kama Noble prize kwenye nyanja zote muhimu hawa jamaa wanazo wao,haina maelezo nyuma ya pazia kuonyesha kuwa wao ndiyo vinara wa technologia ya marekani ikiwa ni pamoja na uchumi wao ? wanaweza wakawa dhaifa kitechnologia ndani ya Israel lakini wana access na technolojia yao iliyoko Amerika...

Source(s) please....
 
Mkuu jaribu kutafuta mlokole yoyote kaa naye muulize maswali kuhusu Israel halafu umsikie, unaweza kuona hata huruma. Mpaka leo kuna watu wamejipa majina ya kiyahudi halafu wanajiita wakristo, kuna wengine wanasema Israel ni taifa teule na wanaona hata mataifa yao yamelaaniwa. Kibaya zaidi angalia hawa watu wanaoisifu Israel wanavyofanywa wakienda huko Israel kwenyewe, wengine wanatukanwa hadi utacheka. Unajua hili ndio tatizo la umaskini, Bible inapitkana bure kwa hiyo ndio source of education kwa walokole, bila kujali ni education ya mwaka gani. Wengine wanadhani hata waziri Mkuu wa Israel ni Musa, na waziri wa Fedha ni Yuda eskarioti.

Una hasira na walokole hadi basi,kuna wakati Musa amewahi kuwa waziri mkuu wa Israel au Yuda Eskariot kuwa waziri wa Fedha ? ungesema wanadhani bado mfalme Daudi/Suleiman au pontio pirato bado wanatawala ukgemaanisha kweli,njee ya hapo nawe kama unachemsha vile. Ukiwalaumu unawaonea bure,mambo ya imani at times watu wanakuwa kama mazombies mbele ya watu waaminio tofauti na wao.
 
Una hasira na walokole hadi basi,kuna wakati Musa amewahi kuwa waziri mkuu wa Israel au Yuda Eskariot kuwa waziri wa Fedha ? ungesema wanadhani bado mfalme Daudi/Suleiman au pontio pirato bado wanatawala ukgemaanisha kweli,njee ya hapo nawe kama unachemsha vile. Ukiwalaumu unawaonea bure,mambo ya imani at times watu wanakuwa kama mazombies mbele ya watu waaminio tofauti na wao.

Mkuu i may agree with you that my choice of words are not good, nadhani wewe umeweka vizuri zaidi. I have nothing against imani yao, tatizo ni akili yao mgando, wanadhani dunia bado iko mwaka 10AD na sio 21st century, kama kuna mtu dunia hii haamini kuwa so far US ndio super power basi atakuwa anaishi katika dunia ya kina Musa na Pharao. Kuna mjumbe mmoja amesema vizuri sana u super power wa Marekani uko wapi, na kwanini wengine si super power.
 
Back
Top Bottom