Hamas inasema kuwa makundi ya Wapalestina yamepinga matarajio ya kuachiliwa zaidi kwa mateka hadi Israel ikubali kumaliza vita Gaza.
Katika taarifa ya Kiarabu iliyosambazwa kwenye Telegram, Hamas ilisema: "Kuna uamuzi wa kitaifa wa Palestina kwamba kusiwe na mazungumzo kuhusu wafungwa au makubaliano ya kubadilishana mateka isipokuwa baada ya kusitishwa kikamilifu kwa uchokozi."wa Israel.
Haijulikani ni mirengo gani mingine ya Palestina inayohusishwa na kauli hiyo. Islamic Jihad, kikundi kidogo katika Ukanda wa Gaza, pia kinawashikilia mateka wa Israeli.
Mazungumzo ya kufikiwa kwa makubaliano mapya kuhusu vita hivi sasa yanafanyika mjini Cairo, Misri, ingawa mazungumzo ya awali siku ya Jumatano hayakuzaa matunda, huku Hamas wakiripotiwa kusema kuwa hawatakubali kusitishwa tena kwa muda kwa mapigano.
Wakati wa usitishaji mapigano wa siku sita mwishoni mwa Novemba, mateka 105 wa Israel waliachiliwa kwa kubadilishana na Wapalestina waliokuwa katika magereza ya Israel. Takriban mateka 120 wa Israel wanaaminika kuwa bado wako wanashikiliwa Gaza.
Israel imekataa mara kwa mara usitishaji vita wa kudumu na Hamas, huku waziri wa usalama wa taifa Itamar Ben Gvir akisema kwenye mtandao wa X kwamba kusitisha vita kwa majeshi ya Israel kabla ya Hamas kushindwa na mateka wote kurejeshwa kungekuwa ni "kushindwa".
Katika taarifa ya Kiarabu iliyosambazwa kwenye Telegram, Hamas ilisema: "Kuna uamuzi wa kitaifa wa Palestina kwamba kusiwe na mazungumzo kuhusu wafungwa au makubaliano ya kubadilishana mateka isipokuwa baada ya kusitishwa kikamilifu kwa uchokozi."wa Israel.
Haijulikani ni mirengo gani mingine ya Palestina inayohusishwa na kauli hiyo. Islamic Jihad, kikundi kidogo katika Ukanda wa Gaza, pia kinawashikilia mateka wa Israeli.
Mazungumzo ya kufikiwa kwa makubaliano mapya kuhusu vita hivi sasa yanafanyika mjini Cairo, Misri, ingawa mazungumzo ya awali siku ya Jumatano hayakuzaa matunda, huku Hamas wakiripotiwa kusema kuwa hawatakubali kusitishwa tena kwa muda kwa mapigano.
Wakati wa usitishaji mapigano wa siku sita mwishoni mwa Novemba, mateka 105 wa Israel waliachiliwa kwa kubadilishana na Wapalestina waliokuwa katika magereza ya Israel. Takriban mateka 120 wa Israel wanaaminika kuwa bado wako wanashikiliwa Gaza.
Israel imekataa mara kwa mara usitishaji vita wa kudumu na Hamas, huku waziri wa usalama wa taifa Itamar Ben Gvir akisema kwenye mtandao wa X kwamba kusitisha vita kwa majeshi ya Israel kabla ya Hamas kushindwa na mateka wote kurejeshwa kungekuwa ni "kushindwa".