Hakuna mpambano wa vyama kwa sababu vyama havina tena itikadi zinazoeleweka. CCM haijulikani inasimamia na kuongozwa na itikadi gani kama ilivyo kwa baadhi ya vyama vya upinzani
CCM inachotaka inachukua! Inachukua iwe ni "wanachama" iwe ni ushindi nk, inachukua kwa sababu CCM sio kwamba ni Chama Dola bali CCM ndio DOLA yenyewe(tafakari hata usajili wake). Hao kina Balozi Dr Slaa, Dr Mashinji, Mwanakijiji na weengi wengine ambao bado wapo vyama vya upinzani ni watumishi wa DOLA wakitumikia mfumo kwa kadri wanavyoelekezwa
Ajabu ni kwamba weledi ni kama unapungua/ umepungua katika kuyaendesha mambo haya kiasi cha watu wa kawaida kugundua na kuhisi uwepo wa nguvu hii ambayo kikawaida inatakiwa ijifiche sana. Tangia enzi za awamu ya kwanza kwa mfano kulikua na Majaji ambao ni wa kwenye "mfumo" lakini kulikua na weledi wa hali ya juu kutokuwa expose tofauti ilivyo sasa ambapo you can easily spot them
Mwalimu Nyerere alipotoa hoja na shinikizo kwa CCM(dola) kukubali mfumo wa vyama vingi alisema ni muhimu CCM(DOLA) isimamie kuanzishwa kwa siasa hizo ili "iuratibu" mfumo huo yenyewe kabda watu hawajaudai. Mwalimu alikua ni bingwa wa siasa na ndie aliyeusuka 'mfumo" na wengi hawakumuelewa alikua na maana gani aliposema CCM (dola) "iratibu" ujio na uwepo wa vyama vingi
Ushauri wa Mwalimu ulifuatwa ila kwa sasa kinachokosekana ni weledi. Angekuwepo nadhani CCM(dola) ingeshameguka kama "alivyotamani" na kungekua na vyama viwili vikubwa vyenye nguvu sawa vikiachiana madaraka kwa maelekezo kutoka "mahala" na huku kukiwa na stability ya kisiasa na kiusalama nchini. Ni wachache walimuelewa. Mwenyewe aliwahi kusema kua Marekani kuna chama kimoja tu hayo mengine mbwembwe tu
Alimaanisha uwepo wa Republican na Democrat ni uratibu wa Dola na hivyo vyama ndio Dola la Marekani. Ndio maana misingi ya kitaifa ya nchi ile ikiwa ni pamoja na ubabe na ubeberu kwa mataifa mengine uko palepale miaka yote, watawale Democrats au Republicans. Natamani watu waelewe