Mkuu Kalamu1, how I wish ingekua ni just a myth. But this is real. The fact that this subject is so confusing ndio mafanikio ya mpango mzima.
Stability tunayoiona nchini(namaanisha tranquility) haipo by chance, imefanyiwa kazi. Vinginevyo mambo "yangeshaharibika" siku nyiingi sana.
Tufungue macho yetu. Tuangaze huku na huku, karibu yetu na hata mbali ya hapo. Kuanzia mtaani kwetu kwenye serikali za mtaa, angazia kwenye taasisi za umma, serikali kuu, halmashauri za miji na majiji, vyombo vya sheria, jumuiya na vyama vya kijamii zikiwemo hata NGOs, vyama vyote vya wafanyakazi, jumuiya za wanafunzi, taasisi za dini, vyama vya michezo na hata vilabu vikubwa vya michezo kama Simba na Yanga.
Kote huko kumejaa watu wanaohakikisha "mfumo' unafanya kazi na kila kitu kina ratibiwa. Chukulia mfano Taasisi moja kubwa ya miongoni mwa dini kubwa hapa nchini uendeshwaji wake unaonekana waziwazi kua unaratibiwa kutokea mahali fulani. Na hata waumini wa dini hiyo wanajua. Pamoja na kutoikubali wanajikuta hawana budi bali kufuata tu. Kwenye vyombo vyote vya habari vikiwemo vya binafsi hasa vikubwa ndio kabisaaa wamejaa
Wanasiasa tunaoona wanaamrisha na kuviendesha hivi vyombo ni kwa mambo yanayokubalika tu na "mfumo", na wakivuka mstari huvutwa mkono. Kwa mfano leo hii kwenye uchaguzi mkuu atokee Rais wa Tanzania kutoka CCM atake kufanya uadilifu, kwenye uchaguzi wa Zanzibar awe kama anawapa Serikali chama kingine kikichoshinda tofauti na CCM(dola) ndio utajua kama kweli Rais anamamlaka ya kila kitu au la! Nguvu inayoongoza mambo kwenye nchi (dola) haitamkubalia, itamdhibiti mchana kweupee
Kwa Marekani ni hivyohivyo pia. Sio kama vyama vyao vinaitegemea Dola bali vyama hivyo ni zao la makusudi (sio bahati mbaya) la Dola ya Marekani. Ila wenzetu wametuzidi weledi kiasi kwamba inaonekana wananchi ndio wanaziweka Serikali madarakani! Kwamba kwa zaidi ya miaka 150/200 ya uhai wa Taifa hilo lenye kusifika kwa "demokrasia" duniani eti imeshindikana kuibuka chama kingine kiundwe na watu wenye ushawishi wa hadhi na pesa(na wapo wengi tu huko)ili na chenyewe kichukue Serikali ni jambo lsiloingia akilini kabisaa
Haingii madarakani Rais Marekani kisha akajiamulia tu kwa kusema "Mimi leo sitaki vita, nataka amani duniani, kwa hivyo majeshi yetu yaliyopo nje ya Marekani yarudi nyumbani". Nakuhakikishia huyo Rais asipoondolewa kwa taratibu za kisheria hata kwa kosa lisilokuwepo basi ataondolewa kwa "njia mbadala" ambazo wenye kuendesha nchi wanazijua the next day!
Hiyo nguvu imekuwepo Marekani miaka yote kama ambavyo ipo Tanzania kwa kipindi kirefu sana ila kwetu tumekosa weledi kiasi cha kujulikana kwa kila kinachoendelea kama hizi cross overs za wanasiasa ambazo naona ni mbinu za ki amateur amateur sanaaa
Sesten Zakazaka,
Ngoja nikujibu kwa kifupi tu.
Lakini naomba usinielewe kwa ubaya kwa haya maneno nitakayotumia hapa, kwa sababu naona wewe ni mtu mwenye busara hasa na mwenye akili inayo'charge' kwelikweli kuliko wengi wetu tuliomo humu jukwaani.
Haya yote uliyoandika hapa ni 'dhana' tu; wengine wanaweza kutumia maneno makali kama "figment of imagination" ikiambatana na "conspiracy theory" kem kem.
Naweza hata nikathubutu kwa kusema kwamba upo vizuri sana kwenye eneo hili, kama mwenye kuwa na kipaji juu yake.
Sasa ngoja kidogo niivute akili hii inayo'charge' hasa, kuunganisha "mfumo" (DOLA) ya kimarekani inavyo'control' wapiga kura wa nchi hiyo.
Chaguzi nyingi katika nchi hiyo, pamoja na hizi nyingi zilizoendelea, kama Japan, Ujerumani, Uingereza na kwingineko na sasa hata kwenye nchi zinazoendelea zinaangukia huko..., chaguzi zao kuu utakuta hata nusu ya wananchi wanaoshiriki haifiki katika kuwachagua viongozi wao haifiki!
Najua hapa ndipo 'conspiracy theory' yako inaposhamiri kabisa.
Uamini wangu ni huu kwa Tanzania yetu hii.
Vyama vyetu vya upinzani bado havijajua mbinu za kuwa'engage' wananchi na kupata baraka yao kuwaondoa CCM.
Kilichopo sasa ni kwamba CCM pamoja na uozo mwingi ilionao kwa miaka hii ya karibuni, lakini muundo wake ulioimarishwa sana tokea zamani, huko vijijini, hicho ndicho kinachowabeba hadi sasa.
Muundo wao ni imara sana tokea mashinani na kupanda juu.
Itakapotokea pawepo na chama kitakachoweza kuuvuruga mpangilio huo, na wao wakajiimarisha tokea huko chini, CCM itaanguka vibaya sana bila ya kujali hiyo "mifumo' unayoiongelea wewe.
Dawa pekee ya vyama vya siasa ni kuuvuruga mpangilio wa CCM tokea chini.
Kwa sasa hivi wanategemea tu kuvuruga huko juu, ambako haiwezekani, kwa sababu hao walioko huko juu wameshikilia silaha zote, mabunduki yote na majela yote ya kuwaumiza wanaotafuta kuwaondoa madarakani.
Niliandika hapo juu nitaandika kwa kifupi...najikuta nikiendelea kutiririka tu bila kujifahamu!