Isingekuwa Kujitoa CHADEMA na Kujiunga CCM...

KalamuTena

JF-Expert Member
Jul 7, 2018
13,189
17,157
CHADEMA ingekuwa katika hali mbaya sana, kama wote waliojitoa ndani ya chama hicho, huku wakielekeza tuhuma zao kwa viongozi wa chama, wangekomaa tu, angalau kwa muda bila kujiunga CCM, watu wengi wangeelewa kwamba ndani ya CHADEMA pana matatizo makubwa.

Lakini hizi juhudi za kukidhoofisha CHADEMA kwa njia hii inayotumika sasa hivi, badala yake inaweza ikawa inawaongezea CHADEMA nguvu.

Kwa hali hiyo basi, juhudi za CCM kukidhoofisha CHADEMA zinafifishwa (diluted) kwa kutokuwa na kutoelewa mbinu sahihi kwa upande wa CCM.

Hao wanaolipwa na CCM humu mtandaoni kuwalaumu Mbowe, 'specifically', nao wanakosa weledi wa kujua kwamba historia ya mabandiko yao humu JF siku zote yanaelekezwa kwenye kumkatisha tamaa Mbowe ili CHADEMA isambaratike.
Sasa hii "Misimamo Rasmi" ndiyo itakayowaaminisha wasiokubali hadaa hizo?

Watu wenye kufikiri watajiuliza, leo itakuwaje huyo anayeiua CHADEMA ashutumiwe kwa vile anatimiza lengo lao?

N.B. Sina 'interest' yoyote na CHADEMA au Mbowe, mbali ya kutetea haki ndani ya nchi yetu Tanzania, na kutamani uwepo wa mabadiliko. CCM sasa basi, inatosha.
 
Huyu mzee ukiacha kkubari kupokea hongo ya ubalozi Ana hoja Nzito khs Chadema...
tapatalk_jpeg_1581335643965.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kalamu1.

Ni kweli ulichosema, nimeona andiko kwenye comment fulani ya M.M. nikagundua kweli huyo Mzee Mwanakijiji amechoka akili, anapiga kelele tu; anadai CDM ilikosea kuwafukuza Kitila na wenzake, kwamba hao jamaa walikuwa ndio "think tank" ndani ya CDM, sasa kama walikuwa think tank kwanini huyo mmoja akarudi CCM kule kule alipoaminisha umma miaka yote akiwa CDM kuwa CCM imechoka inahitaji mbadala, then yeye pamoja na uwezo wake wa kufikiria akaamua kurudi kujiunga na wale wachovu!.

Huu mchezo CCM wanaucheza kishamba sana, watake wasitake lazima wahakikishe huko mbele wanazuia malalamiko ya wanachama wao wakati wa kuteua wagombea utakapofika, ni either wampitishe alietoka upinzani wanaeamini anakubalika kwa wapiga kura wake, at the same time wawatose wote waliobaki ndani ya chama chao kwa miaka yote wakikipigania au wawatose hao wageni siku ya kuteua wagombea itapofika. Hapa lazima watalipizana visasi tu.

Huyo mwenyekiti wao japo amebariki huu mchezo wa kununua wapinzani uendelee, but ajiandae kuwa mpatanishi siku sio nyingi zijazo, na kwa tabia yake ya ubabe, sidhani kama ataweza, wajiandae kwa mpasuko.


Sent using Jamii Forums mobile app[/USER]
 
Hakuna mpambano wa vyama kwa sababu vyama havina tena itikadi zinazoeleweka. CCM haijulikani inasimamia na kuongozwa na itikadi gani kama ilivyo kwa baadhi ya vyama vya upinzani

CCM inachotaka inachukua! Inachukua iwe ni "wanachama" iwe ni ushindi nk, inachukua kwa sababu CCM sio kwamba ni Chama Dola bali CCM ndio DOLA yenyewe(tafakari hata usajili wake). Hao kina Balozi Dr Slaa, Dr Mashinji, Mwanakijiji na weengi wengine ambao bado wapo vyama vya upinzani ni watumishi wa DOLA wakitumikia mfumo kwa kadri wanavyoelekezwa

Ajabu ni kwamba weledi ni kama unapungua/ umepungua katika kuyaendesha mambo haya kiasi cha watu wa kawaida kugundua na kuhisi uwepo wa nguvu hii ambayo kikawaida inatakiwa ijifiche sana. Tangia enzi za awamu ya kwanza kwa mfano kulikua na Majaji ambao ni wa kwenye "mfumo" lakini kulikua na weledi wa hali ya juu kutokuwa expose tofauti ilivyo sasa ambapo you can easily spot them

Mwalimu Nyerere alipotoa hoja na shinikizo kwa CCM(dola) kukubali mfumo wa vyama vingi alisema ni muhimu CCM(DOLA) isimamie kuanzishwa kwa siasa hizo ili "iuratibu" mfumo huo yenyewe kabda watu hawajaudai. Mwalimu alikua ni bingwa wa siasa na ndie aliyeusuka 'mfumo" na wengi hawakumuelewa alikua na maana gani aliposema CCM (dola) "iratibu" ujio na uwepo wa vyama vingi

Ushauri wa Mwalimu ulifuatwa ila kwa sasa kinachokosekana ni weledi. Angekuwepo nadhani CCM(dola) ingeshameguka kama "alivyotamani" na kungekua na vyama viwili vikubwa vyenye nguvu sawa vikiachiana madaraka kwa maelekezo kutoka "mahala" na huku kukiwa na stability ya kisiasa na kiusalama nchini. Ni wachache walimuelewa. Mwenyewe aliwahi kusema kua Marekani kuna chama kimoja tu hayo mengine mbwembwe tu

Alimaanisha uwepo wa Republican na Democrat ni uratibu wa Dola na hivyo vyama ndio Dola la Marekani. Ndio maana misingi ya kitaifa ya nchi ile ikiwa ni pamoja na ubabe na ubeberu kwa mataifa mengine uko palepale miaka yote, watawale Democrats au Republicans. Natamani watu waelewe
 
Ukweli uko hivi, ccm tayari ni chama ambacho wananchi wameishakichoka, hata ifanye nini sio rahisi tena watu kukikubali. Ndio maana unaona ccm inajisifu kufanya makubwa, na kuwanunua viongozi wa upinzani ili kipate mvuto, lakini hakipati huo mvuto.

Ushahidi kuwa ccm imechokwa, pita kwenye vituo vya kujiandikisha wapiga kura, kwanza wako wachache mno, na wanaojitokeza hawana hamasa yoyote. Iwapo CCM itaendelea kubaka box la kura ili iendelee kukaa madarakani, naiona kabisa ikitolewa madarakani kwa machafuko.
 
Hayo ni mawazo ya Nyerere,lakini mwenyewe anakiri kwenye kitabu chake kwamba katika uongozi wake kuna makosa alifanya.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Aliyafanya sababu hakutaka kushaurika ugonjwa wa watawala wa kiafrica kuamini wanaakili wanajua kuliko wote wanaishia kuungua na jua.Ujuaji wake akauwa uchumi
 
Chadema kwa sasa kiko juu sana CCM inahaha sana kujaribu kuimaliza lakini ukweli ni kwamba CCM hawajui kusoma alama za nyakati na ndio anguko lao
Mkuu labda hujaijua organisation ya CCM. Hata kama unatamani lakini kuitoa CCM madarakani futa kabisa akilini mwako
 
Mkuu labda hujaijua organisation ya CCM. Hata kama unatamani lakini kuitoa CCM madarakani futa kabisa akilini mwako
Labda kama hujui historia ila CCM kiko katika hali mbaya sana tokea kiundwe kwa sasa ni ubabe tu wa vyombo vya dola ndio unakilea.mbeleko ya Majeshi ya ulinzi huwa haidumu sana kumbuka Romania ambako ndiko wamesomea wana CCM wengi leo iko wapi.
 
Km kweli unaitakia mema Chadema yko naushauri tafuta hicho kitabu ukisome Kuna ya kujifunza pia ukiacha Kampeni aliyomfanyia Mh Magufuli Dr Slaa Ana hoja nzuri na nzito khs Chadema pia...
Chadema ni baba lao mpaka imetungiwa vitabu, chama hakijawahi shika dola lakini kinasakamwa kila kona mpaka kutungiwa vitabu
tapatalk_jpeg_1581335643965.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom