Ishu ya Wilaya mpya ya Kisesa imeingia wapi

Ishu ya Wilaya mpya ya Kisesa imeingia wapi

Halafu unagawa je wilaya ya Magu yenye nwgative growth of population wakati kuna wilaya kibao mikoani zenye wakazi zaidi ya laki 9 na positive growth of population?

No. Kama ni population kwa kisesa hawajakosea, lakini pia hata magu walishashindwa kuilea kisesa, kwani mpaka mda huu kisesa inategemea huduma muhim zte mwanza mjini
etc, umeme, maji, afya, nakila kitu, mpaka police operations.
 
Haya mambo ya kugawa mikoa,wilaya,kuongeza majimbo,huwa yanafanyika hata ulaya/usa au ndio mbinu za ulaji za wanasiasa wa Afrika?sijawahi sikia State ya washington imegawanywa,mfano kulikuwa kuna ulazima gani wa kugawa mkoa wa Arusha kutengeneza Manyara?kwani bila kuweka tawala za kisiasa,vituo vya polisi,afya,shule haziwezi kujengwa mpaka uweke mkuu wa mkoa?


Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
 
1.kata ya sangabuye
2.kata ya usagara
3.kata ya fela
4.kataya kisesa
5.kata ya bujashi
6.kata ya bukandwe

Jina ..... wilaya ya sanjo
Jimbo la ... usagara

Au nasema uongo ndg zangu.
That name Bujashi killed my day 😅😅😅
Kata ya Bhusangambiri mbona hujaitaja?
 
Ipo mbioni na Makonda anamalizia malizia mipango kuwa DC hapo
Yaani awe demoted kutoka kuwa RC awe DC?
By the way inatengenezwa kwanza wilaya mpya ya Busanda kule Geita, nyie wa Mwanza msubiri kidogo. Details za hii wilaya zipo kwenye hotuba ya mzee wakati anazindua shamba la miti la Chato
 
Ondoeni shaka.kwa Sasa hakuna Kijiji,au kata,au wilaya,au mkoa,utakao ongezeka tena.kama haya yaliibuliwa,Basi ilikuwa kimakosa.kwa Sasa hakuna kitakachoongezeka.
 
Haya mambo ya kugawa mikoa,wilaya,kuongeza majimbo,huwa yanafanyika hata ulaya/usa au ndio mbinu za ulaji za wanasiasa wa Afrika?sijawahi sikia State ya washington imegawanywa,mfano kulikuwa kuna ulazima gani wa kugawa mkoa wa Arusha kutengeneza Manyara?kwani bila kuweka tawala za kisiasa,vituo vya polisi,afya,shule haziwezi kujengwa mpaka uweke mkuu wa mkoa?


Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
Hii ni ilani ya chama katika kuongeza namba za ajira kwenye makaratasi na kwa wenye navyo.
Ukisikia mkoa mpya umeanzishwa jua kuna ajira mpya zisizopungua 200 mfano: RC, DCs, RPC, OCDs, RTO, Wakurugenzi wa wilaya na mkoa juu, madreva wa hao niliowataja, wafagiaji, walinzi, n.k
 
kisesa inafaa kua jijini kabisa kwa hio ni jambo jema tu,ila kubaki magu inakua haikai sawa na magu yote kama halmshaur bado kuna vijiji vingi sana so yote haiwez kupelekwa jijini
Mimi nadhani tuko pamoja ile kisesa ilibidi baadhi ya sehemu ziwe kwenye Jiji, maeneo mengine yabaki huko huko kwenye Wilaya ya Magu. Maana haileti maana MTU atoke Kisesa afate huduma za Serikali Magu hali ya kuwa kutoka pale na Mwanza Mjini ni jirani sana. Hili watu wenye mamlaka wangelitazama zaidi.
 
Wanakata misungwi kidogo, magu kidogo na ilemela kidogo
Wilaya ya Magu walishaipunguza sana tokea sidhani kama wataendelea kuipunguza, maana kabla ya hapo kuanzia Lamadi unakuja mpaka Nyashimo Busega yote ilikuwa Magu hapo zamani kabla ya Simiyu sasa wakiendelea kukata ina maana watabaki na Tarafa moja au Mbili ni kitu ambacho hakiwezekani.
 
Wilaya ya Magu walishaipunguza sana tokea sidhani kama wataendelea kuipunguza, maana kabla ya hapo kuanzia Lamadi unakuja mpaka Nyashimo Busega yote ilikuwa Magu hapo zamani kabla ya Simiyu sasa wakiendelea kukata ina maana watabaki na Tarafa moja au Mbili ni kitu ambacho hakiwezekani.
wanazipunguza ili kupatikana kwa uraisi huduma za kijamii kwa wananchii na hii ni kwa sababu kila kukicha watu wanaongezeka chukua mfano temeke ilivyokua mwanzoni ilikua inahudumia hadi kigamboni amapo ilikua ni usumbufu sana kwa wananchi wa kigamboni kufuata huduma za kiutawala temeke halikadharika ilivyokua kinondoni
 
No. Kama ni population kwa kisesa hawajakosea, lakini pia hata magu walishashindwa kuilea kisesa, kwani mpaka mda huu kisesa inategemea huduma muhim zte mwanza mjini
etc, umeme, maji, afya, nakila kitu, mpaka police operations.
Wilaya zingine pia kama Misungwi na Kwimba zina maeneo yaliyo karibu na jiji. Sio Magu tu. Namaanisha hii ni sababu isiyokuwa na nguvu.
 
Kwa nini kisiwezekane ?
Wilaya ya Magu walishaipunguza sana tokea sidhani kama wataendelea kuipunguza, maana kabla ya hapo kuanzia Lamadi unakuja mpaka Nyashimo Busega yote ilikuwa Magu hapo zamani kabla ya Simiyu sasa wakiendelea kukata ina maana watabaki na Tarafa moja au Mbili ni kitu ambacho hakiwezekani.
 
Kutoka rohoni mwangu iSerikali iachane na kuanzisha Wilaya ya Kisesa na Katoro. Nikianza na Kisesa, Wilaya inayotarajiwa kuanzishwa halina eneo Kabisa. Tayari Wilaya ya Magu ilikwisha megwa sehemu kubwa kupelekwa Busega. Senta ya Nyanguge na Kisesa ndiyo tegemeo la Magu. Vilevile Misungwi bado ni Wilaya ndogo sana katika Wilaya zilizopo Mkoa wa Mwanza. Ukimega Usagara, Kigongo Ferry Misungwi itabaki na nini?. Ukichukua pia Wilaya ya Katoro pia halina eneo. Umbali wa Katoro na Geita mjini ni kilomita 20 na katoro iko Geita Vijijini. Tayari Geita ilikwisha megwa na na kuanzisha Halmashauri ya Mji wa Geita. Binafsi sioni sababu ya kuanzisha Wilaya hizi ni ufujaji wa fedha za Serikali. Tufanye kazi kwa takwimu siyo mihemuko za kisiasa.
 
Hivi mkuu wa wilaya kama hiyo itakayoanzishwa ya Kisesa akikaa jirani na mkuu wa wilaya kama Ilala au Kinondoni si atajisikia mnyonge sana. Ni kama mwanafunzi wa shule ya kata kutoka kijijini huko akutane na mwanafunzi mwenzie kutoka shule kama Feza n.k.
 
Mhhh hapana. Kumbuka Jimbo la Busanda lina Tarafa mbili Busanda na Butundwe na Kata 22 ! Wakati wilaya ya Mbogwe ina kata 17 tu na Bukombe ina kata 18 tu. Hivyo Busanda imechelewa sana kupewa Wilaya. Wewe akili yako yote unadhani jimbo la Busanda ni Katoro tu umekosea sana. Wilaya hiyo tarajiwa inaanzia huko Butundwe ziwani hadi Bukoli mpakani na Kahama na ikiwa na idadi kubwa ya watu kuliko jimbo lolote la uchaguzi mkoani Geita. Kumbuka sasa hivi wananchi wanasafiri umbali wa karibu km 100 kutoka Ntono hadi Nzera kufuata huduma za Halamashauri ya Geita vijijini. Ndhani hujui chochote kuhusu maeneo haya. Kwa kuanzishwa kwa Wilaya ya Busanda ni hoja ambayo inapaswa kuungwa mkono na kila mwananchi.
Kutoka rohoni mwangu iSerikali iachane na kuanzisha Wilaya ya Kisesa na Katoro. Nikianza na Kisesa, Wilaya inayotarajiwa kuanzishwa halina eneo Kabisa. Tayari Wilaya ya Magu ilikwisha megwa sehemu kubwa kupelekwa Busega. Senta ya Nyanguge na Kisesa ndiyo tegemeo la Magu. Vilevile Misungwi bado ni Wilaya ndogo sana katika Wilaya zilizopo Mkoa wa Mwanza. Ukimega Usagara, Kigongo Ferry Misungwi itabaki na nini?. Ukichukua pia Wilaya ya Katoro pia halina eneo. Umbali wa Katoro na Geita mjini ni kilomita 20 na katoro iko Geita Vijijini. Tayari Geita ilikwisha megwa na na kuanzisha Halmashauri ya Mji wa Geita. Binafsi sioni sababu ya kuanzisha Wilaya hizi ni ufujaji wa fedha za Serikali. Tufanye kazi kwa takwimu siyo mihemuko za kisiasa.
 
Akiruhusu tu kugawanywa na baadhi ya wilaya hasa za kanda ya ziwa, basi itakuwa chaos. Kuna watu wanataka mikoa yao igawanywe. Morogoro kusini wanataka mkoa wa Kilombero, Ruvuma kaskazini mashariki wanataka mkoa wa Tunduru, Tabora kaskazini wanataka mkoa wa Nzega. Kuna miji midogo inataka kupandishwa hadhi kuwa mamlaka ya mji yenye kuunda halmashauri. Mfano ni Tukuyu mkoani Mbeya, Ngaramtoni mkoani Arusha, Karatu Mkoani Arusha, Mbalizi mkoani Mbeya etc. Kama hatuko tayari kugharamia maeneo mapya ya kiutawala basi tuwe uniform. Sio tunakataza Kaskazini na Nyanda za Juu Kusini lakini tunaruhusu Kanda ya Ziwa. Mimi sioni kama tuko tayari kugharamia maeneo mapya ya utawala. Tuache tuone serikali ya awamu ya 6 itakuwaje.
Lakini pia serikali inatakiwa kufuata ushauri wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Wizara ya fedha, Mamlaka ya mapato na Ofisi ya Taifa ya Takwimu. Sio tunaanzisha tu wilaya au mkoa just kwa maombi ya mabaraza ya madiwani au migogoro. Serikali ifuate ushauri wa kitaalam wa Taasisi zake.
Acha uchochezi Mkuu...unauthibitisho upi kwamba taratibu hazifuatwi!?
 
Back
Top Bottom