Ishu ya Wilaya mpya ya Kisesa imeingia wapi

Ishu ya Wilaya mpya ya Kisesa imeingia wapi

Awamu ya tano ulikuta taratibu zote za kuanzisha mkoa wa Songwe zimekamilika. Walichofanya ilikuwa ni kuitangaza kwenye gazeti la serikali kama hatua ya mwisho ya kuanza kwa operation na establishment of public offices.
Tuthibitishie basi hilo la kutofuatwa taratibu kwa Maeneo mengine
 
Halafu unagawa je wilaya ya Magu yenye nwgative growth of population wakati kuna wilaya kibao mikoani zenye wakazi zaidi ya laki 9 na positive growth of population?
Why negative growth Mkuu hapo Magu?
 
Haya mambo ya kugawa mikoa,wilaya,kuongeza majimbo,huwa yanafanyika hata ulaya/usa au ndio mbinu za ulaji za wanasiasa wa Afrika?sijawahi sikia State ya washington imegawanywa,mfano kulikuwa kuna ulazima gani wa kugawa mkoa wa Arusha kutengeneza Manyara?kwani bila kuweka tawala za kisiasa,vituo vya polisi,afya,shule haziwezi kujengwa mpaka uweke mkuu wa mkoa?


Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
Mtu makini Aje hapa aisee
 
nakubaliana na Mdimay. hakuna haja ya kuanzisha wilaya, Mikoa nk. kwa sasa. Mfano Kisesa na Katoro for what reason?.
 
Hi
Kutoka rohoni mwangu iSerikali iachane na kuanzisha Wilaya ya Kisesa na Katoro. Nikianza na Kisesa, Wilaya inayotarajiwa kuanzishwa halina eneo Kabisa. Tayari Wilaya ya Magu ilikwisha megwa sehemu kubwa kupelekwa Busega. Senta ya Nyanguge na Kisesa ndiyo tegemeo la Magu. Vilevile Misungwi bado ni Wilaya ndogo sana katika Wilaya zilizopo Mkoa wa Mwanza. Ukimega Usagara, Kigongo Ferry Misungwi itabaki na nini?. Ukichukua pia Wilaya ya Katoro pia halina eneo. Umbali wa Katoro na Geita mjini ni kilomita 20 na katoro iko Geita Vijijini. Tayari Geita ilikwisha megwa na na kuanzisha Halmashauri ya Mji wa Geita. Binafsi sioni sababu ya kuanzisha Wilaya hizi ni ufujaji wa fedha za Serikali. Tufanye kazi kwa takwimu siyo mihemuko za kisiasa.
Hizo km za Geita to katoro umezipata wapi kagoogle upya
 
Kutoka rohoni mwangu iSerikali iachane na kuanzisha Wilaya ya Kisesa na Katoro. Nikianza na Kisesa, Wilaya inayotarajiwa kuanzishwa halina eneo Kabisa. Tayari Wilaya ya Magu ilikwisha megwa sehemu kubwa kupelekwa Busega. Senta ya Nyanguge na Kisesa ndiyo tegemeo la Magu. Vilevile Misungwi bado ni Wilaya ndogo sana katika Wilaya zilizopo Mkoa wa Mwanza. Ukimega Usagara, Kigongo Ferry Misungwi itabaki na nini?. Ukichukua pia Wilaya ya Katoro pia halina eneo. Umbali wa Katoro na Geita mjini ni kilomita 20 na katoro iko Geita Vijijini. Tayari Geita ilikwisha megwa na na kuanzisha Halmashauri ya Mji wa Geita. Binafsi sioni sababu ya kuanzisha Wilaya hizi ni ufujaji wa fedha za Serikali. Tufanye kazi kwa takwimu siyo mihemuko za kisiasa.
Jiji la Mwanza linakuwa sana. Ni muhimu ipatikane Wilaya mpya ya tatu, halafu iunganishwe ndani ya Jiji.

Sasa hivi, Jiji limepanuka mpaka Usagara ( Misungwi ) na Kisesa ( Magu ).

Huduma nyingi wakaazi wa Usagara, Fela na Kisesa wanapata Jijini ambako Ni karibu zaidi.

Hata kama hakutakuwa na Wilaya mpya, afadhali Fella na Usagara ziungwr Nyamagana na Kisesa iungwe Ilemela kuupa mji nafasi ya kupumua.
 
Back
Top Bottom