Is this the end of CHADEMA?

Is this the end of CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Wewe si umeshajitoa Ndugu toka CHADEMA? Waachie wenye chama chao waonyane,wanyooshane,wafukuzane na waelewane.Usiwaingilie

hii ya kusema waache wenye chama chao iko cku mtakuta chama kina mkt na mzee mtei tuu!!
 
watafukuza wote ila siku wakimfukuza ZZK ndio mwisho wa cdm kuwa chama kikuu cha upinzani! zitto ndio nguzo ya chadema iwe wanataka au hawataki yeye ndiye amebeba taswira ya chama
 
Mkuu Chilisosi kwa kuweka picha hii ulikuwa unakusudia kutuma ujumbe gani?

1.1276530557.wild-dogs-fighting.jpg


Hawa ni Mbweha, Mbwa mwitu, au hata Fisi hapo inavyoonyesha hawaaminiani tena
Maana hao wawili wa kulia wameamnza vita wao kwa wao
na wale wa kati nao vita vinanukia
kuna wengine wanapatana na wanakuja kuulizia chanzo ni nini? na hatimaye wataparurana na vita yake haitaweza kuzimika
Mimi naona Chilisosi kafikisha ujumbe kuwa naye alikuwepo katika hilo pori la wanyama mwitu akagundua mapema hakuna mwelekeo akajikata ndio maana hapo haonekani
 
Last edited by a moderator:
Hiki kipigo inaonekana kimeleta simanzi ccm kuliko chama chochote kile sijajua kwa nini???lakini hazina bado iko ya kutosha watu "wanatakiwa kuelewa demokrasia bila nidhamu ni fujo" waliogundua demokrasia wakaweka katiba,kanuni na taratibu ili kusimamia nidhamu,mwaka umeanza vizuri huu na hii ni salamu kwa wote ambao wanajiona kuwa wao ni maarufu kupita tasisi zinazowapa umaarufu,leo media zinakufuta kutokana na identity yako kuwa ni mwanachama mashuhuri wa ccm/cdm siku ukivuliwa uanachama ndio unaona kuwa you are notching outside the institution that made you to be there,uvccm chukueni hao vijana ambao mnawaita wapambanaji.
 
Unapolima shamba lazima uondoe magugu ili mazao yastawi vizuri,tunapojiandaa kunyakua dola lazima tuwaondoe wachumia tumbo wote nakubaki na watu makini kwa ukombozi wa nchi!viva cdm
 
Huu umbeya utawaponza, sasa CDM imehusikaje na kuchochea maandamano ya Mtwara? Kama Mbunge wa sisiemu kaunga mkono we unakuja kuropoka juu ya CDM, hivi mtaacha lini kuweweseka? unataja taja tu makabila, mara ngapi wasukuma wamafukiwa kwenye mashimo ya dhahabu? mara ngapi wakurya wamepigwa risasi na askari wa Barrick? Tumia akili kuliko......
 
uhafidhina unawatesa hawataki mabadiliko dk slaa anafanya juu chin et lazima awe mgombea hii timua timua ita ighalimu chadema kuja kufikia 2015 watakuwa vipande vipande.lazima wakubari mabadiliko mapema la sivyo tusubiri tu watch.
 
Mikimikiki ni jambo lakawaida katika vyama. Kwa nini unakimbilia kusema CDM imefikia mwisho. Yaani kuwafukuza wasaliti wa chama ndo kufikia mwisho. Mimi naona wewe gamba linakusumbua nenda kalivue kwamba ndo uje humu jf
Haya ona sasa,
Kila mtu akiwakosoa katumwa na Zito
Mie ni chilisosi na situmwi, I am my own boss
By the way mie natuma situmwi
 
Chadema ondoa takataka hilo ni pigo la CCM na si Chadema kana mnavyodhania
 
Mikimikiki ni jambo lakawaida katika vyama. Kwa nini unakimbilia kusema CDM imefikia mwisho. Yaani kuwafukuza wasaliti wa chama ndo kufikia mwisho. Mimi naona wewe gamba linakusumbua nenda kalivue kwamba ndo uje humu jf
Watu wanakuwa adabishwa na kupewa maonyo wasipojirekebisha ndio hufukuzwa ,
Kwa mtindo wenu nyie mtakuwa mnapiga risasi hadharani watu , kwa kifupi chama chenu na iddi amini hakuna tofauti
 
Kama ilivyo siasa za Tanzania hasa kwenye kambi ya upinzani,huibuka vyama venye nguvu na baada ya muda hupotea.
mimi nilijijengea imani kuwa CDM kuwa si chama cha mpito lakini sasa naona ni walewale tu.

Hii ni kutokana na siasa za undugu na ubaguzi zinazoibuka sasa,viongozi wa CDM wanatuhumiana pia wanapishana kauli,hapa sitapanzungumzia sana ila nieleze wasiwasi wangu mkubwa juu za tuhuma wanazopewa viongozi wa CDM.

1.Tuhuma zinazotolewa na wanachama wanaihama cdm na kueleza madudu yaliyo ndani ya cdm.unaweza kupuunza kwa kusema wanaponda kwasababu wametoka lakini hasha! mbona yanajirudia?.hapa tutafakari tuhuma ya Mke wa Dr Slaa kutuhumiwa kuhujumu chama lakini pia kutengeneza mtandao wa wabunge wa viti maalum anaowataka yeye uchaguzi ujao na kubagua wengine,lakini pia tuhuma za matumizi mabaya ya pesa ndani ya chama,mbaya zaidi mama huyu anatuhumiwa kuamrisha viongozi wa chama Taifa kuhidhinisha malipo kazi ambayo si yake ni ya katibu wa chama Dr Slaa anakwenda mbali zaidi pale anapokua mara kwa mara anadai pesa za mume wake wakati yeye hupo ata kama ni haki yake.HOJA ZOTE HIZI CHAMA HAKIJATOA MAJIBU,ni ishara tosha huu ni ukweli.

2.Tuhuma zinazotolewa na CCM kuwa CDM wanapanga mauwaji ya raia,mbona hawajibu viongozi wa CDM inamaana ni kweli kama ni kweli si kweli kama cdm wamepoteza dira na umaarufu wake sasa unashuka na hatimaye kufa kama ilvyokufa NCCR MAGEZI ya Mrema?.

3.CDM tunajua kilianza kama chama cha kufa na kuzikana cha wachaga,kwangu si shida kwani sasa kimesajiliwa kwa chama cha kisiasa lakini shida hapa ni tuhuma za kuendeleza dhana ya kufa na kuzikina na hapo ndipo utakuta viongozi wake ni wale wale akibadilika wanampa mkwe wao na mtu ambaye si mchaga kama kabwe akionesha niya tayari anaitwa CCM au Usalama, huu ni ushaidi wa tuhuma za kuendeleza dhana ya kufa na kuzikana. na hapa huwa ninamkumbuka sana marehemu CHACHA WANGWE ambaye amekufa kifo cha kutatanisha na cdm hata siku moja sijawai kusikia wakimkumbuka kwa lolote wakati kwangu mimi nilimwona kama mwanaharakati wa kweli.

najua mtatukana sana na kuniita CCM ila nitafurahi mkinita Mtanzania maana mi si mwamini wa vyama ila ni Mtanzania Ambaye si shabiki kama wengi walivyo na ushabiki ambao leo nawatabiria kutafuta chama kingine cha kushabikia maana CDM inakufa.

Ushauri wangu vijana wenye upeo na muona wa dhati wa kusaidia taifa fungueni macho muone kuwa nchi hii ina ombwe la chama cha kisiasa chenye sura halisi ya taifa la Tanzania wa sasa si watanzania wale wa ukoloni.tuungane tuanzishe chama chenye sura ya kitaifa na ambacho katiba yake itakuwa wazi kukemea uwepo wa mabepari ndani ya chama ambao mara zote ndiyo adui wa siasa za Tanzania, ebu chukua mfano cdm wakiamua leo kuwa wanamiliki mahotel wapandishiwe kodi Mbowe atakubali hoja hiyo wakati anajua zile protea,akina aishi hotel, amani beach na wakina Bill hali itakuwa mbaya.TUFUNGUKE WATANZANIA TUACHE USHABIKI.Tutaendelea kuhama vyama mpaka lini? ona sasa cdm hiyo inaporomoka kwa kasi kubwa kisa tu sheji ama ametumwa ama kwa akili zake anatuburuza! Mti wenye matunda ukipigwa mawe sana huku haupuputishi matunda mwisho hufa kwa majeraha ya mawe
 
Umaarufu + CHADEMA = Kuporomoka?

Mlinganyo huu umeniacha hoi.
 
Kimeporomoka wapi labda fafanua vizuri.

Mtasubiri sana hiki chama kuja chini na bado kinasonga mbele
 
Mkuu, kajipange upya.
Sijaona hoja yoyote yenye mantiki, sembuse mpangilio mzuri wa mada.
Mimi huwa ninaamini kuwa wanaoingi humu JF, ni watu waliosoma na kuelimika. Lakini kama kiashiria cha usomi wenyewe ndiyo hiki cha mtu kushindwa hata kupangilia anachokiandika ili kieleweke vizuri, basi haishangazi kwa nini JF inataka kuwa gulio.
 
duh..mods siku hizi wanakunywa sana viroba!!eti hii nayo ni thread!!!!!!!!!!!!!
 
Mtu kama wewe ni wa kutojibiwa hata hoja moja, amabayo kwa bahati mbaya huna.

Ila kukusaidia, nakkuliza wale masalia waliofukuzwa wangeondoka na kuandaa press conferncce ya kuisifu cdm na viongozi wake?
au kuzua uongo na kujiosha ili wahurumiwe na jamii. Unless wendio mmojawapo....pole!

Mabadiliko hayaji kwnye sahani, ila huo uwongo lazima uwepo ili watu waonyeshe walikuwa kazini. Kama c mvumilivu we jirushe baharini nyangumi wanakusubiri.


CDM iko strong ipo gear ya tatu, nne, tano inamaliza kazi ya kuwakomboa watz
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom