Kama ilivyokuwa kwa NCCR mageuzi baada ya uchaguzi wa 1995 chama kinachojiita cha demokrasia chadema kimekumbwa na migogoro isiyokwisha
Kila kukicha hapa utasikia ngumi zimezuka kona fulani
Mara ooh Saa nane kamuanika Zito
Mara ooh Zito msaliti
Mara ooh Sshibuda anadhamini wasaliti
Mara ooih CCM wanaingiza mapandikizi,
Mara ooh juliana kafanya vilee
Mara ooh sijui nani kafanya vile, yaani imekuwa kero sasa kwani kila siku sasa ukiingia jamii forums au kusoma magazeti hukosi vichwa vya habari vya chadema wakinyoosheana vidole na kutimuana kama kuku bila kufuata katiba wanayodai kuwa ndiyo ya kidemokrasia.
Hiki chama mie nimeanza kukitilia mashaka kuwa kinaweza kuja kuleta maafa kwa nchi yetu kwani wao hawahubiri amani bali wanaeneza machafuko kama vile uamsho tu hakuna tofauti yoyote.
Hebu fikiria suala la gesi watu na akili zao wanashinikiza maandamano gesi ibakli mtwara. haya yangesemwa huko zenji ingekuwa balaa hapa. huu si uchonganishi huu, unaposhinikiza hayo maandamano hujui sie wahehe, wanyakyusa, wakurya, waha, wafipa, wahaya, wachaga nk pia tunahitaji kuona faida ya hiyo gesi.
Uliwahisikia wasukuma wakiandamana kudai mapato ya dhahabu na almasi au minofu yawe kwa ajili ya mwanza tu?
Au uliwahi sikia umeme unaotengenezwa mtera wahehe na wagogo wakasema ubaki iringa na dodoma tu taifa libaki kiza?
What about gesi itakayopatikana lake rukwa? lake tanganyika? selous?
Chadema mie kwa sasa nawafananisha na Kundi la mbwa mwitu waliokosa mawindo kwani wana hasira kali na matokeo yake wamepoteza muelekeo wanaanza kuumana wenyewe kwa wenyewe
![]()
Sijui kama wewe mtoa mada unajua kinachodaiwa na wana Mtwara, wanachodai ni kujengwa kwa kiwanda cha kuchakachua gesi (yaani malighafi ya gesi) Mtwara na si Kinyerezi maana huko ndiko malighafi hiyo inakopatikana kama ilivyo kwa viwanda vya MINOFU YA SAMAKI kama ulivyotaja vipo Mwanza, Mara na Kagera na si Dar. Na faida inayopatikana kutokana na minofu hiyo hunufaisha Taifa kwa ujumla. Ndivyo wanamtwara wanavyodai Kiwanda cha GESI KIJENGWE KUSINI na si Dar-es-Salaam (Kinyerezi) na BIDHAA ZA GESI hiyo kuenezwa nchi nzima wala si Dar peke yake na ikiwezekana hata nje ya nchi kwa MANUFAA YA TAIFA na wewe ukiwemo utafaidi kwa namna moja ama nyingine. Sasa hilo ni kosa? Nakushauri ni vyema ukafanya uchunguzi kwa kina kisha toa hoja zenye maana na si lugha za maudhi kama unavyotaka kupotosha umma wa Tanzania.