Habari za saa hizi wanajamvi,
Nina rafiki yangu moja mzuri alinena na kuniambia "
mapenzi ni mazoea". Maneno hayo machache nimegundua yamebeba uzito mwingi na yana maana kubwa na pana.
Katika mapenzi yoyote mwanzoni yananoga na yanakuwa na shamrashamra nyingi, kwasababu kipya kinyemi, hamuishi kumisiana, kila mtu hamu haimuishi ya mwenzie alimradi kila kitu kinaenda kama maji mtoni.
Mnaweza hata mjiulize kwanini hatukuonana mapema. Hii ni
phase ya mwanzo ya mapenzi ambayo inaitwa
falling in love. Baada ya muda kama miaka kadhaa hayo mapenzi yote yanaweza yachuje mtu akikugusa unaona kero, akikupigia simu anakubughudhi na kukufatilia,yaani mnakuwa mmechokana.
Hii inakuwa
phase inayofuatia ya mapenzi ambayo zile chachu zote za mapenzi zinashikiliwa na chuki na ubinafsi fulani na katika wakati huu unaweza ujiulize pia je nipo na mtu sahihi?
Yaani yale yaloyojiri mwanzo yote yanakuwa kinyume chake, kama ni ndoa unaanza kuiona chungu. Unaweza hata ufikirie pengine nikipata mwengine mambo yatakuwa kama awali ufurahie mapenzi.
Lakini nikudissappoint jibu ni
hapana kwasababu hata ukipata mwengine baada ya muda fulani mapenzi yatachuja. Kwahio suluhisho ni nini? ukitaka mafanikio kwenye mahusiano yako mpende mtu ulompata/ulo kuwa nae kama ni mtu sahihi au lah kuna sababu zilizokufanya umchague yeye.
Jenga mazoea ya kumpenda yeye kama yeye, mapenzi yanahitaji wito, kujitolea, nguvu, wakati, muda na kikubwa zaidi busara. Unatakiwa kujua nini chakufanya na kwa wakati gani ili unawirishe mapenzi yako.
Usikosee katika hilo. Mapenzi ni zaidi ya hisia ni maamuzi na ni mazoea.
Au mnasemaje wenzangu?
View attachment 161621
View attachment 161622
Cc
utafiti