Is Jamii Forums the best Discussion forum in Africa?

Is Jamii Forums the best Discussion forum in Africa?

Mkuu hapo umegusa pazuri sana. Kuna watu wana interest tofauti ilihali hawana majukwaa yao. Kuna wadau nawaona mara kwa mara wanaomba majukwaa na moderators wanakaa kimya kuliko kutoa feedback. Hadi sasa nimeona kuna gape kubwa kwenye;
1. Jukwaa la magari
2. Jukwaa la fasheni za nguo.
3. Jukwaa la malezi ya watoto

2 and 3 asee!
 
Huo muonekano mpya umetulia, Ni wapi tuliambiwa tutembelee huo muonekano mpya!? kwa maana niliona ile siku moja halafu mkaiondoa... lakini kitu kimetulia...

Mkuu wa chuo siwezi kukupinga mtazamo wako, lakini ukweli utaendelea kubaki pale pale kwamba huo muonekano mpya haufai.

sisi wadau tunachohitaji zaidi ni mgawanyo mzuri wa majukwaa kuna mambo muhimu katika jamii lakini hayana majukwaa jf.
 
Last edited by a moderator:
In Kenya there are Mashada and Kenyan List, Ugandan Red pepper, South African The South SA, and Nigerian NaijaLand while in Tanzania we have our dear JF...so which is the best Discussion forum in Africa?

i think you are wrong... unaangalia forums zilizokaa ki-nchi zaidi
 
Yuko wrong kivipi wakati kauliza swali nakuweka references?

Acha kukurupuka ili uonekane umechangia.
sasa yupi kakurupuka hapa dogo

huwezi kucompare apples with oranges

Tanzania ni tanzania, uganda ni uganda etc.

If you want to compare kwa idadi ya subscribers, then nchi zenye population kubwa definitely zitakua na more subscribers; if you want to check kwa namna ya ratings, we dont have standards za ratings, if you want to compare foreigners wangapi wanatumia forum, pia hatuna, its an online community

Even if tungesema Geographical coverage, bado tungehitaji proper measures, sio mtu anayeweza list two or three forums basi tunacrown superiority...

Tanzania hata online subscribers to ni wachache kuliko many African countries.
 
Janjaweed


Unazidi kuonyesha ujinga wako wapi mleta mada ame conclude kiasi cha wewe kumpinga?

Unafikiri kwa kutumia nini? Hapo ulitakiwa kuja na majibu kwa mujibu Wa facts zako kwamba unafikiri IPI ni the best kuljko kukurupuka Kama umeshikwa wizi....

Tuliza mshono huo jibu kwa busara...
 
Last edited by a moderator:
lusungo

That sums up your ignorance and stupidity... any smart person would never dare ask such a stupid question

Its bu!!sh!t all along

Now save your little hole... jibu basi swali la mleta mada

Maana hadi sasa huna ulichojibu umerukia tu kutaka ligi na wanaume

JIBU SWALI then we can take it from there
 
Last edited by a moderator:
That sums up your ignorance and stupidity... any smart person would never dare ask such a stupid question

Its bu!!sh!t all along

Now save your little hole... jibu basi swali la mleta mada

Maana hadi sasa huna ulichojibu umerukia tu kutaka ligi na wanaume

JIBU SWALI then we can take it from there


Kwa uelewa wako unafikiri smart person anauliza maswali gani?

Kuna swali lisilo na majibu?

Dhima ya kuuliza maswali ni nini? Kipi bora Kati ya kutoa jibu la swali au kutoa kejeli kwa swali?

Hivi unaelewa hata nini malengo ya kuuliza maswali? Au unafikiri kila MTU anajua yote kwenye ulimwengu huu?

Mwerevu hujibu alichoulizwa bali mpumbavu na punguani hutoa kejeli kwa alichoulizwa....

Wewe ni debe tupu tu kima wewe huna lolote ujualo bora ukae kimya kuficha utupu Wa kichwa chako.
 
Kwa uelewa wako unafikiri smart person anauliza maswali gani?

Kuna swali lisilo na majibu?

Dhima ya kuuliza maswali ni nini? Kipi bora Kati ya kutoa jibu la swali au kutoa kejeli kwa swali?

Hivi unaelewa hata nini malengo ya kuuliza maswali? Au unafikiri kila MTU anajua yote kwenye ulimwengu huu?

Mwerevu hujibu alichoulizwa bali mpumbavu na punguani hutoa kejeli kwa alichoulizwa....

Wewe ni debe tupu tu kima wewe huna lolote ujualo bora ukae kimya kuficha utupu Wa kichwa chako.
Unachemka fululu fululu
 
Tuwe wakweli. Wananchi wengi wa Nigeria wameelimika kuliko sisi na wana uzoefu mwingi wa kufanya kazi nje. Huu uzoefu na elimu unauona katika maoni yao. Sisi mara nyingi mijadala yetu ina hisia kuliko ushahidi. Na tuna tabia ya kutojiamini. Na akija Mtanzania na elimu ya juu kidogo hasa kama anaishi nje basi inakuwa shidaaaaaaa!
 
tutoe ombi kwa
Invisible na viongozi waige mazuri ya hiyo forum na walete hapa jf na sisi tufaidi
maana kuna mdau alishasema weee liletwe jukwaa la usalama barabarani lakini kwa kweli haikupewa kipaumbele japo ilikuwa ni swala zuri sana!

Siyo waige Bali waboreshe iwe zaidi ya hiyo forum kwa nafasi yao na wachangiaji wa mada na waleta mada tubadilike tuchangie na tulete mada za maana.
 
Last edited by a moderator:
Ufahamu wanajf uko katika
maswala ya kimungu, mapenzi, na miujinza, na kujadili viongozi wa taifa.

ni wachache sana wenye uelewa kuhusu maswala ya uchumi, tekinolojia na viwanda.

Hiki ndicho kilichoiua JF ya Late 1990's, sasa hivi imejaa watu wasioweza kujenga hoja zaidi ya Mapenzi, Dini na Miujiza. Lakini hii inaonyesha ni wananchi wa aina gani taifa ili walivyo,

kama tunawakilisha jamii yetu na sisi ndio GT halafu tunakata issues kwa level hii, basi mjue kuwa tuna safari ndefu sana. Ndio maana GT waliokuwepo zamani hasa walimu wa vyuo vikuu na viongozi wa serikali na vyama vya siasa wameacha kuingia hapa kwa kuwa watu wanathamini matusi, udini na unazi kwenye siasa badala ya kujadili kwa hoja

Natamani sana JF ya wakati ule ambayo nilikuwa nikilog in nakutana na wow factor, hivi sana ukilog in unajua kabisa utakutana na mabishano ya kidini yamejaa watu ambao hawawezi hata kujenga hoja kutetea anachokiamini zaidi ya kuishia kutukana matusi, tatizo liko wapi?

mfumo wetu wa elimu umeshindwa kuzalisha watu wenye kujenga hoja za msingi na kuzalisha watu wanaothamini matusi? tumekosea wapi?
 
kati ya tatizo kubwa ambalo Watanzania wengi wanalo ni kushindwa kutengeneza question tags.
 
Mkuu wa chuo siwezi kukupinga mtazamo wako, lakini ukweli utaendelea kubaki pale pale kwamba huo muonekano mpya haufai.

sisi wadau tunachohitaji zaidi ni mgawanyo mzuri wa majukwaa kuna mambo muhimu katika jamii lakini hayana majukwaa jf.

Ukweli kwa mujibu wa nani ya kwamba haufai!? Na huo muonekano mpya haufai kivipi!?
 
Acheni pumba. Nendeni huko kwa Wanaigeria mkachangie hzo mada sasa. Aliyeanzisha JF anatakiwa kupewa credit pia.

Haitoshi kusema kuwa JF sio nzuri kama forum fulani. Njoo na idea fulani zitakazo iwezesha JF kuwa juu zaidi.

Otherwise wanaoiponda JF na 24 hrs wanashinda hapa nawaona wanafiki tu. period!!!

Hiyo Nairaland nadhani IPO kukidhi mahitaji ya Wanaijeria. Swali la kujiuliza "je, jamiiforums inakidhi mahitaji ya sisi tunaoitumia?" Kwa kiwango kikubwa inakidhi mahitaji yetu na ndiyo maana kila siku tunakutana hapa.

Kama ni mapungufu basi ni madogo sana na hayatupi uhalali wa kutopongeza juhudi za uongozi mzima wa JF.

NAKUUNGA MKONO MKUU.
 
Is Jamii Forums the best discussion forum in Africa?!
 
Watanzania wengiwanajua maneno ya Kiingereza ila hawajui kanuni za lugha ya Kiingereza.......

kati ya tatizo kubwa ambalo Watanzania wengi wanalo ni kushindwa kutengeneza question tags.
 
Hapana! best disscussion forum in Africa inaweza kuwa Nairand ya wanaigeria! Lakini nina hakika Jamiiforums inaweza kuwa ya pili baaada ya Nairanda...! Uzuri Mimi hizi mbili nazijua vizuri!

Ukiangalia kwenye umakini wa wanachama Nairand wana wanachama wengi makini ukilinganisha na Jf maana ni mara chache ukakuta matusi na utani ambapo hapa husiki!

Muonekano/mpangilio/ wa majukwaa! Katika hili Jamiiforums is the best ukilinganisha na Nairand..
Nairand hawana mpangilio mzuri kabisa wa forums kiasi kwamba unaweza kuchukua muda mrefu kutafuta jukwaa unalo liihitaji kifupi majukwaa yao wame yarundika kama nyanya hivyo mtu mgeni anaweza kupata shida pakuanzia . katika hili nitawawekea picha!

Uzuri wa application kati ya Nairandforum na Jamii forums...na hapa bado Jf inaongoza kwa kuwa application nzuri na yenye mvuto ambayo utafurahia na majukwaa yote lakini katika hili Nairandforum pamoja na kuwa na wametupita kwenye technology still wameshindwa kuipatia Nairandforum application nzuri...application walionayo haina tofauti na mtu kutumia browser kwa hiyo katika kipengele hiki tumewapiga bao!

Upole/Ukali wa moderators! Hakika moderators wa kule ni wakali ukifanya kosa ukapigwa ban hairuhusiwi kufungua id nyingine labda wasikubaini ..lakini hapa Jf tuna moderators wapole na wanao vumilia sana..kule ukifungua thread utakutana na sheria mwanzoni wana sahihisha hadi lugha..kuandika kitoto ni kosa ..ku chit-chat kwenye thread ni kosa ..nafikiri ukali wao ndio unafanya Nairand kuwa the best ukilinganisha na Jf!

Uzalendo kwa nchi yao! Duu hawa wenzetu ni wazalendo sana kwa nchi yao ukilinganisha nasisi hata ukipitia disscussion zao zote wao ni Nigeria kwanza!

Siasa za majitaka kwenye forum! Hawa jamaa pamoja na kuwa na mikwaruzano kati ya wana siasa na wana siasa lakini siasa zao hazijafikia za kwetu kabisa ...sisi huwa tuna dhalilishana sana.ukipitia jukwaa lao la siasa unakutana na mada za siasa za msingi na zenye tija tuu ..pengine ni sababu ya sheria zao kali kwenye forum.

Wanachama wanavyo changamkia thread! Nairand pamoja na kuwa na member wengi sana lakini uchangamkiaji wa thread si mkubwa sana ukilinganisha na Jf ..Jf watu wanajua kushambulia sana thread..na comment zinapanda kwa kasi ukilinganisha na Nairand forums ambapo inategemea ni jukwaa gani labda sports au political..

Fikra za wanachama..kuhusu siasa! Hata kule Nairand kama ilivyo Jf kuna watu wana amini kabisa kuwa kuna watu ni vibaraka wa watu na wanalipwa kuwasifu au kuwatetea watu fulani..

Ubinafsi na utaifa! Kule Nairand wakijua wewe si Mnigeria wanachama wanachukia unapo comment kwenye mambo yanayo ihusu Nigeria....

Urahisi wa kuwasiliana na moderators ! Kule Nairand ni rahisi sana kuwasiliana na moderators maana kila jukwaa kuna sehemu juu ya kuwasiliana na moderator wa jukwaa husika kama una maoni au ushauri..kuna sehemu pa kumuandikia Email kirahisi kabisa..ni tofauti na kitufe cha report abuse..hiki kipo separate..katika hili wametushinda bila shaka Invisible na timu yake wanaweza lifanyia kazi!

Idadi ya wanachama wanao kuwa hewani or on line...katika hili pamoja na Nairand kuwa na wanachama wengi sana lakini ni wanachama wachache wanaweza kuwa on line kwa wakati mmoja..hata kama kuna issue nyeti wanachama huwa hawazidi 2000 tofauti na Jf japo siku hizi hawaonekani!

Kuhusu Matangazo..hakika kama ni hela mmiliki wa Nairand anapata hela nyingi kupitia matangazo maana wana matangazo mengi hadi.... nafikiri hili linachangiwa na kujitangaza na pia wanaigeria wengi wana uelewa mkubwa wa matumizi ya internet na umuhimu wake hivyo ni rahisi watu kupekeka matangazo wakijua yata wafikia watu wengi...

Mada kuandikwa kwa umakini! Kule wanachama wengi wanajua kuandika mada zao vizuri hawakuachi mwanachama unajiuliza! Wanaandika kwa undani kabisa sio vipisi..ukienda kwenye habari za uchunguzi ndio utapenda kabisa!

Ni kweli tuna Mengi ya kujifunza kutoka Nairand na wao wana ya kujifunza kutoka kwetu hasa mpangilio wa thread na muonekano wa jukwaa sisi tuko bora!

Nairand forums is the best though
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom