Iselamagazi
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,922
- 6,009
Hi! wana JF!
Hivi kuna uwezekano wa mwanaume na mwanamke kuwa ktk uhusiano wa kawaida kabisa kama marafiki tu bila kuwa wapenzi?
Kuna mkasa mmoja ambao naufahamu wa mwanaume na mwanamke ambao waliishi ktk ndoa kama mume na mke kwa takribani miaka 12 na baadae kulitokea kutoelewana kwa wana ndoa hawa na kupelekea kutalikiana kwa miaka mitano (5) sasa!
Wawili hawa nafanya nao kazi ktk ofisi mmoja. Kitu cha ajabu ni kuwa wana ushirikiano mzuri sana ktk masuala ya kazi na huwezi kujua kama kuna tofauti za kuachana kama tulivyo zoea ktk jamii zetu kuwa bibi na bwana wakishatengana ni nadra sana kukuta jambo kama hili. Si ofisini tu, ushikiano wao upo hata katika masuala ya kijamii mathalani, utawakuta wakiwa pamoja ktk misiba, harusi n.k.
Kurizuka rumours pale kibaruani kwetu kuwa hawa wawili wana kula mshedede kwa siri sana! Jamaa mmoja pale kibaruani alishawahi kumtania yule bwana mtalaka kuwa bado wanaendeleza kale kamchezo; yule bwana mtalaka alikataa kata kata kwamba yeye na mtalaka wake wamebaki kuwa marafiki tu wa kawaida na kwenye masuala ya kale kamchezo kila mtu kivyake na kwamba kama ana wasiwasi afanye uchunguzi anaojua yeye. Ilikuja thibitika baadaye kuwa ni kweli wawili hawa wamebaki kuwa marafiki tu.
Is it entirely possible for a man and woman to be friends and not be romantically interested for some reason?
Hivi kuna uwezekano wa mwanaume na mwanamke kuwa ktk uhusiano wa kawaida kabisa kama marafiki tu bila kuwa wapenzi?
Kuna mkasa mmoja ambao naufahamu wa mwanaume na mwanamke ambao waliishi ktk ndoa kama mume na mke kwa takribani miaka 12 na baadae kulitokea kutoelewana kwa wana ndoa hawa na kupelekea kutalikiana kwa miaka mitano (5) sasa!
Wawili hawa nafanya nao kazi ktk ofisi mmoja. Kitu cha ajabu ni kuwa wana ushirikiano mzuri sana ktk masuala ya kazi na huwezi kujua kama kuna tofauti za kuachana kama tulivyo zoea ktk jamii zetu kuwa bibi na bwana wakishatengana ni nadra sana kukuta jambo kama hili. Si ofisini tu, ushikiano wao upo hata katika masuala ya kijamii mathalani, utawakuta wakiwa pamoja ktk misiba, harusi n.k.
Kurizuka rumours pale kibaruani kwetu kuwa hawa wawili wana kula mshedede kwa siri sana! Jamaa mmoja pale kibaruani alishawahi kumtania yule bwana mtalaka kuwa bado wanaendeleza kale kamchezo; yule bwana mtalaka alikataa kata kata kwamba yeye na mtalaka wake wamebaki kuwa marafiki tu wa kawaida na kwenye masuala ya kale kamchezo kila mtu kivyake na kwamba kama ana wasiwasi afanye uchunguzi anaojua yeye. Ilikuja thibitika baadaye kuwa ni kweli wawili hawa wamebaki kuwa marafiki tu.
Is it entirely possible for a man and woman to be friends and not be romantically interested for some reason?