siwezi kuwa na hofu ya kitu kisivhokuwepo
Denial...the most primitive defense mechanism
siwezi kuwa na hofu ya kitu kisivhokuwepo
Kiranga Mungu ni UPENDO, unatakiwa ujue complexity ya upendo ktk mantiki ya kuwa huwezi kutofautisha kati ya Mungu na UPENDO.
hivyo basi kwa nini Mungu anahuzunika? ni kwa sababu alimuumba mwanadamu na free will (kumbuka nilishakubana kuhusu free will ukakimbia)... mwanadamu ana uhuru wa kuamua kufanya jambo lolote jema au baya...ndivyo Mungu alivyotaka iwe. sasa anahuzunika pale mtu anapoamua kufuata njia potofu as a result of him being free to choose btn right and wrong.
God cannot contradict himself, atakuacha ufanye yako na ataumia coz he loves u unconditionally, but cant go against his own nature
nakuja kukujibu
Kwa tafsiri yako hiyo basi leo hii wasingeendelea kuwepo binadamu.
Hahah mkuu Kiranga umewashika pabaya hapo hawatoki!,hili swali niliwahi kuwauliza siku za nyuma katika uzi flani wakasepa.Inashangaza sana kuambiwa maneno kama,
Mungu akaona huzuni
Mungu akaghadhabika
Hasira ya mungu ikashuka juu yao
Mungu akawalaani
Mungu akapendezwa nao
Hapa inathibitisha kwamba mungu ni man made kama vitu ama idea nyingine nyingi tu.Mungu mwenye uwezo wote hawezi kuona huzuni wala hasira labda kama mi sielewi nini kinaleta hasira na huzuni.Hapa hawachomoki ndugu!
We unadandia mambo tu..hadi sasa mmeshindwa kuthibitisha dai lenu la kupinga uwepo wa Mungu.
Hujajibu swali.
Mungu anayejua yote (pamoja na hilo la kwamba mwanadamu atafanya mabaya kabla hajafanya hivyo) atahuzunikaje?
Kuhuzunika kunakuja baada ya kujua kitu ambacho hukukijua.
Huyu mungu kajua yote, hakuna kipya atakachokijua.
Anahuzunukaje?
Halafu, mungu anayejua nitafanya mabaya kabla sijazaliwa, na akijua hivyo aiwezi kubadili, utasemaje kanipa freewill?
Free will itatoka wapi ikiwa siwezi kubadili alichoona nitafanya kabla sijakifanya?
vitu vile vile ndugu.Hivi unajua maana ya Uhuru?,ni aina ganibya uhuru wenye adhabu baadae?.Labda kama sielewi maana halisi ya Freedom.Yaan ametupa uhuru wa kumjua ama kuacha kumjua lakini kuna adhabu ya moto na mateso baadae?.Sasa kama ametupa uhuru kwa nn kuna adhabu kwa waendao kinyume?.Think Big bro
The deity called "God" does not exist.There is no point on discussing his/her/its egalitarian tendacies.
Any efforts are futile
Mungu anakupenda ndo maana anahuzunika. unajua kupenda wewe? mwanao akiumia si unahuzunika? Mungu ni zaidi ya mara elfu
alafu kusema eti kitu ukikijua kabla usihuzinike umeitoa wapi hiyo?
huwezi kubadili asili. you can exercise your free will to the extent that you will not contradict nature.
Nitathibitishaje kwamba kisichopo hakipo?
Unaweza kuthibitisha chumbani kwako hakuna kibatari cha dhahabu kisichoonekana kinaelea katikati?
Kinachothibitishwa ni kilichopo, si kisichopo.
Sasa wewe inayeaema mungu yupo inaweza kuthibitisha kwamba yupo?
...na kwa akili yako usichokiona wewe HAKIPO.vipo unavyoviona wewe tu.
kiwango chako cha upumbavu kiko juu mnoo...
yaani unakutana na mtu then unamwambia kwamba chumbani kwake kuna kibatari cha dhahabu kisichoonekana kinaelea katikati...
kwamba ni illusionist ni kukupa ujiko usio stahili.labda ni mwezi mchanga...
mifano yako imejaa majinga majinga na wala huoni soni.
unategemea ignore list imekupa kiburi cha kuandika majinga majinga...
Majinga majinga yenyewe ni :
kama unafahamu kutokuwepo kwa kibatari cha dhahabu kwa nini uulize au wewe ni chizi ?
wewe umesa chumbani kwangu "HAKUNA " then wataka uthibitishiwe hakuna yako. bogus
umeambiwa Mungu ndiye Muumbaji angalau kina pa kuanzia.
wewe unasema huyo ninayesema ni Muumbaji hayupo ! nakuuliza umejuwake hayupo ? Wakati mimi nafahamu yupo na amewahi kuja duniani akakanyaga ardhi akiitwa Yesu.
badala ya kuniambia namna ulivyomtafuta ukamkosa na ukahitimisha hayupo unabuni mfano uliojaa majinga majinga.
wewe jamaa mzigo kweli kweli...
cc Ishmael
Kuhuzunika kunatokana na kujua kitu kipya.
Sakika moja unajua mwanao mzima, inayofuata unajua anaumwa, unahuzunika.
Huyu mungu ambaye hakuna kipya kwake, maana kajua yote kabla hayajatokea, anatokaje kwenye furaha na kuanza kuhuzunika?
Ina maana hakujua kitakachokuja au vipi?
Anayejua yote anaanzia wapi kuhuzunika?
Kama huwezi kubadili asili, free will itatoka wapi? Free will ni uwezo wa kibadili. Wewe unasema mungu kaumba asili ambayo haiwezi kubadilishwa, sasa hapo free will ipo wapi?
what's wrong with u kiranga???? hivi unataka kuniambia kuwa kwa kuwa Mungu anajua kitakachotokea mbeleni afurahie tu? hapo upendo wake utakuwa wapi? Mungu wa kufurahia viumbe wake wapatapo tabu atakuwa Mungu kweli?
aliyekwambia kuhuzunika kunatokana na kujua kitu kipya ni nani? umeitoa wapi hii dhana?
rejea nilichokiandika...sijasema Mungu ameumba asili, nimesema Mungu ni asili na huwezi kwenda kinyume na asili in the name of exercising your free will.
naona narudia kitu kilekile now and then, you choose not to comprehend.you guys keep on asking the same questions mkijibiwa mnakimbia na kurudi tena with a twist of words.
you are all simply scared and the thought of God really scares you.
First thing first, wapi nimesema nisichokiona hakipo?
...hakuna kibatari.cha shahabu kisichoonekana...
Hujaonyesha bado ni vipi nimesema nisichokiona hakipo.
...KISICHOONEKANA...sio lazima unachosema hakionekani iwe kweli hakionekani kwa kila mtu.na wakati wote na maxingira yote.
...kisichoonekana...kwako
Umahiri wa busara za mtu huonekana pale anapojadili na watu ktk mada tofauti.
Nadhani wewe hauko hapa Kuelewa bali ni kuleta ubishi usiokuwa na Tija na kupoteza muda wako na wangu.
Unarudia maneno km matangazo ya vifo. Hali ukitambua kuwa km ungeamua Kufikiri kidogo usingefanya hivyo. Na mada hii isingekuwa na mlolongo mrefu namna hii bila sababu za msingi.
Nadhani kwa mtu mwenye busara itakuwa si jambo la busara kuendelea Kujadili na wewe manake Umeziba njia zote za Uelewi.
Nakusikitia sana kiranga Kwa kumkana MUNGU aliyekupa nafasi ya kuuona Utukufu wake uliokuzunguka.
Ni masikitiko kuona kwamba Mpaka leo hii 2015 kuna baadhi ya binaadamu wanakubali kabisa kuwa wao wako hapa duniani na kila kitu kinachowazunguka vyote vimekuwepo hapa kwa BAHATI NASIBU (Chance).
Nakutakia mjadala mwema.