Kamanda wa Kamandi Kuu ya Khatam al-Anbiya ya Jeshi la Iran amesema makamanda wa Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani katika eneo la Asia Magharibi (CENTCOM), na vile vile makamanda wa Kikosi cha Majini cha nchi hiyo wapo Tel Aviv kuwasaidia maafisa wa utawala haramu wa Israel kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
Meja Jenerali Gholam Ali Rashid, Kamanda wa Kamandi Kuu ya Khatam al-Anbiya alisema hayo jana Jumanne hapa Tehran na kuongeza kuwa: Majeshi ya Iran yana taarifa kwamba makamanda wa CENTCOM na vile vile jeshi la Marekani na jeshi lake la baharini wanashirikiana na makamanda wa Israel katika kambi ya kijeshi iliyoko Tel Aviv kusimamia na kuongoza mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni dhidi ya taifa la Palestina.
Kamanda huyo amesema kushindwa Wazayuni katika Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa ni moja ya vipigo vikubwa vya aina yake ambavyo havijawahi kushuhudiwa.
Meja Jenerali Gholam Ali Rashid ameongeza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel, si tu kwamba umepata pigo kubwa bali pia umeshindwa kwa fedheha na wanamuqawama wa Palestina.
Meja Jenerali Gholam Ali Rashid, Kamanda wa Kamandi Kuu ya Khatam al-Anbiya alisema hayo jana Jumanne hapa Tehran na kuongeza kuwa: Majeshi ya Iran yana taarifa kwamba makamanda wa CENTCOM na vile vile jeshi la Marekani na jeshi lake la baharini wanashirikiana na makamanda wa Israel katika kambi ya kijeshi iliyoko Tel Aviv kusimamia na kuongoza mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni dhidi ya taifa la Palestina.
Kamanda huyo amesema kushindwa Wazayuni katika Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa ni moja ya vipigo vikubwa vya aina yake ambavyo havijawahi kushuhudiwa.
Meja Jenerali Gholam Ali Rashid ameongeza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel, si tu kwamba umepata pigo kubwa bali pia umeshindwa kwa fedheha na wanamuqawama wa Palestina.