😹😹😹 Atajiju!!
Hii tabia naipenda kweli.
Kuna likizo moja nilienda kumsalimia bibi, sasa si unajua ukifika binti wa mjini vijana wa mkoani shobo nyingi km wameona almasi.
Kuna jamaa akajitosa kuniwinda asijue km anawinda fisi. Basi nilimlia tuhela twake nikampanga njoo home ukifika rusha jiwe kwenye bati nitatoka twende ghetto. Lilivyo zuzu likaja kweli, akarusha kijiwe kidogo nikakausha…!!
Akaongeza lingine mlio ukazidi wa mwanzo, babu akauliza nini hiko? Eehh asichukue jiwe kubwa sijui tofali lile weeh tukasikia “Buu” juu ya bati. Akatoka babu na gobole alimkimbiza..!! 😹😹😹
Kesho yake nimepita kijiweni namuita mchumba mambo? Akaniambia “Achana na mimi nipotezee”