Ipi ni dawa ya wivu?

Ipi ni dawa ya wivu?

Dawna ni hii Kama ana kutuhumu unatembe na Salma wakati siyo kweli basi mtafute Salma kiukweli alafu umuonyeshee live. Wivu utaisikia kwa jirani
 
Mgombeze tu hahahaha me mwanaume akiniletea habari za wivu namkatia maneno harudii tena.......nipo nae MTU kama huyo nlikua sipumui yaan simu akipiga ipokelewe ndani ya sec hiyhiyo ukichelewa bifu nkaona anataka kuleta upuuzi nlimzingua akaacha
 
Habari za mida hii wakuu
Naombeni mnisaidie njia za kumfanya huyu mtu aachane na hii tabia...nimechoka asee
BADILI WIVU KWA HISIA CHANYA
Jifunze kutafsiri matendo yake kwa upendo. Vuta picha na ujipe hamasa chanya badala ya kuumia kwa kila atendalo. Katika hili, ni vizuri ukaongozwa na subira, kwani asili ya watu wenye wivu wa kupindukia, hukimbilia kupandwa na jazba badala ya kuuliza kwa utaratibu na kupokea jibu linalojitosheleza.
Hata siku moja usije ukadanganywa kwamba ukiwa mkali ndiyo utamfanya mpenzi wako asikusaliti. La hasha! Wekeza upendo kisha muishi kwa maelewano, hapo utaweza kumpa sababu ya kuishi kwa uaminifu. Utafiti unaonesha kuwa kundi la wasaliti wa uhusiano wao, huundwa na idadi kubwa ya watu waliochoshwa na migogoro ya kimapenzi.
Mantiki hapa ni kuwa mtu yupo kwenye uhusiano wake lakini anaamua kutoka nje baada ya kuona hana maelewano na mwenzi wake. Hivyo basi, ni vizuri ukawa unafuata hatua zinazofaa katika kupata ufumbuzi wa kila jambo unaloona halipo sawa kwa mwenzi wako, badala ya kugombezana. Itakugharimu.
Kama wivu wako unakufanya ujione wewe ni dhaifu, huna jambo la kufanya zaidi ya kuhakikisha unaishinda hali hiyo. Ukiwa na tabia ya kujiamini, itakusaidia kuufunika wivu, japo bado utaendelea kuwepo ndani yako lakini jinsi utakavyokuwa unashughulikia mambo yako na mwenzi wako, itakupa heshima zaidi.
Wivu ukizidi ni hatari kwa sababu unaweza kukuweka roho juu muda wote, ukaonekana mapepe na jamii ikakucheka kutokana na jinsi kichwa chako kilivyo rahisi kushika moto. Hii ina maana kuwa kudhibiti wivu ni kujiongezea heshima. Tafakari mwenyewe, unataka uheshimiwe au udharauliwe?
 
Habari za mida hii wakuu
Naombeni mnisaidie njia za kumfanya huyu mtu aachane na hii tabia...nimechoka asee
Dawa yake jitahidi kupunguza ujana delete baadhi ya mambo ambayo yanamfanya aone kama utamegwa
 
We sio muaminifu ama hujapenda kwa dhati ndio maana unaona kero. Kwa mtu ajuaye thamani ya mapenzi lazma atakuwa na wivu tu mind that,its auto!

Ila kwa wasiojua thamani ya neno nakupenda wataona sawa tu kwa lolote ufanyalo maana haumii kwa ajili yako. Huwez kuwa na mtu unampenda kwa dhati halafu uone anawasiliana kimapenz na mtu mwengine af usijiskie vibaya hata kama ni utani. Never!!! We hujapenda
 
na mm nna wivu sana kwa mpenzi wangu nisiwe muongo....ngoja nione hiyo dawa yetu.
khaaaa,,,!!!,, hapo tu nyie wanaume,,, wivuu umepilitiza ,,, aaaa!!!! hadi bafuni unanilinda,, sokoni hamna kwenda ,, cmu yng unayo muda wote,,, lkn ujiamini bado,, mmmmmhhh,,


hapo tu nakonda bila kunyanyaswa
 
khaaaa,,,!!!,, hapo tu nyie wanaume,,, wivuu umepilitiza ,,, aaaa!!!! hadi bafuni unanilinda,, sokoni hamna kwenda ,, cmu yng unayo muda wote,,, lkn ujiamini bado,, mmmmmhhh,,


hapo tu nakonda bila kunyanyaswa
huo ss sio wivu ni ujingaa
 
Back
Top Bottom