Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
💭 Hivi utajisikiaje pale ambapo mpaka ukawa na Neno la Siri ndo utaweza kufungua post za watu kwenye mtandao wa Instagram??
🥂 Instagram Iko kwenye majaribio ya kuweza kuachia mfumo mpya wa watu kuweza kuficha post zao kwa kutumia Neno la Siri.
💭 Mtumiaji atapaswa kufungua post za watu kama vile video au picha kwa kutumia Neno la Siri, itakupa uwezo wa kuweka neno la Siri ambapo mtu ili aweze kufungua post yako video / picha inabidi aweke neno la Siri (password) ambalo umeweka kwenye post yako.
🌍 Sababu kubwa Instagram kuweka mfumo huu ili kufanya followers wako (wafuasi) kuweza kuwa karibu na watengeneza maudhui (creators) ili kujua neno la Siri au kuweka ushindani kwa followers wako kutafuta password.
Mabadiliko haya Bado hajatangazwa Rasmi lini itaachiwa kwa watu wote lakini baadhi ya watu wameshaanza kutumia Tembelea page ya Design utaweza kuona mfano wake.
Password yake ni "Threats" .