Inside Considence: Utata juu ya kifo cha muigizaji Bruce Lee..

Inside Considence: Utata juu ya kifo cha muigizaji Bruce Lee..

Da'Vinci

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2016
Posts
36,442
Reaction score
110,068
Salute Comrades:

Wakuu leo naomba tujadidili juu ya kifo cha muigizaji BRUCE LEE.
Hivi ni kweli alikufa kifo cha kawaida..?
Alikufaje? Sababu ya kufariki ni nini..?

Kwa story nazo zifahamu juu ya kifo chake (Sijui kama ni sahihi) eti chanzo cha kifo walikua CIA kwa kumtumia Mkewe!
Je hii hoja ni kweli? Alikua na masrahi yapi kwa CIA..?

Lakini pia Mwanae Brandon Lee inasemekana Kua Alienda Hongkong kupeleleza kifo cha baba ake akarudi NA ushahidi akasubiri acheze picha iliyokua imeandaliwa, Lakini hata hivo picha hakuimaliza alikufa akiigiza hiyo picha kwa risasi akafa na siri za kifo cha baba yake.

Ikumbukwe.
-Bruce lee ni mtu pekee aliyekua anaweze kupiga kalatasi inayoninginia ngumi ikatoboka [Sio kuchanika ]

-Alikua na uwezo wa kupiga pushap 100 kwa kutumia kidole kimoja cha shahada.

-Alikua na uwezo wa kurusha punje ya mchele angani akaidaka kwa kijiti.

-Alikua yupo faster sana hadi kwenye kuigiza wakawa wanamuweka in Slow motion ili mapigo yaonekane vizuri. Etc

Tiririkeni wakuu..
Cc.
Malcom Lumumba mngony The bold MSEZA MKULU izzo Slowly mshana jr zitto junior Infantry Soldier @Consigilere GuDume elmagnifico

Aksanteni.

-Da'Vinci Learning
 
Pia alikuwa ni Mwanafalsafa mzuri sana, nakumbuka nukuu zake alisema

"Usiombe kuwa na maisha rahisi , bali omba nguvu za kukabili maisha magumu"

"Mtu mwenye busara anaweza kujifunza mengi kutokana na swali LA kipumbavu kuliko mpumbavu anavyoweza kujifunza kutokana na jibu LA busara"
 
Bruce Lee alikufa kifo cha kawaida hakuna utata wowote ule (Utata unatengenezwa na watu)
1.Miezi ya mwisho mwisho kabla ya kufariki, afya ya Bruce Lee haikuwa nzuri. Alikuwa akisumbuliwa na maumivu makali ya kichwa na mgongo. Kumbuka miezi miwili kabla ya kifo chake alipoteza fahamu akiwa mazoezini, alipata matibabu na kupata nafuu.
2.Bruce alijikuta akitumia madawa makali ya kutuliza maumivu kwa mda mrefu (bila kufata taratibu za kitabibu). Hii ni kutokana na Kusumbuliwa na maumivu mazito ya mwili hasa kichwa na mgongo.
3Kuna wakati ilibidi atumie mitishamba kutuliza maumivu.
4.Siku ya kifo chake akiwa nyumbani kwa mcheza sinema wa kike aitwaye Betty Ting Pei, wakijadili script ya filamu ya Game of death ,alipatwa na maumivu makali ya kichwa.
Mwanadada Betty Ting Pei ilibidi ampatie dawa ya maumivu jamii ya aspirin, na Bruce lee akaomba apumzike kwenye kitanda apoapo nyumban kwa bety. Alivyoenda kuamshwa kwa ajili ya chakula Bruce Lee hakuamka tena adi Leo hii.
5. Postmortem ilifanyika na kuonyesha ubongo ulikuwa umevimba sana, wakihusisha allergic reaction iliyosababishwa na dawa aliyomeza.
6. Mwana dada Betty ambaye kipindi hicho alikuwa na Miaka 25,hamekuwa hakikana siku zote kuhusika na kifo change Bruce Lee.Ile dawa aliyompa Bruce Lee ata yeye alikuwa akiitumia.
Mengineyo kuhusu Bruce Lee.
1.Alifia Hongkong akiwa na umri wa miaka 32, ila alizikwa Marekani
2. Alikuwa mwana philosophy mzuri,kumbuka msemo wake maarufu "my friend be like water, water can flow, water can crash".
3.Bruce Lee alitokea familia ya kitajiri uko Hong Kong.
4.Wacheza sinema waliokuwa karibu naye miaka hiyo(Bolo yeung, Chuck Norris, marehemu Jim Kelly) wanathibitisha speed ya Bruce Lee ilikuwa kama ya mnyama duma.
5. Kwenye mazoezi/maandalizi ya inter the dragon (kama sijakosea) Jack chain akiwa underground aliumizwa kwa bahati mbaya na Bruce Lee, wakati wa kutoka mazoezi Bruce Lee alimwona Jack chain akienda nyumbani kwa miguu alimwita akampatia fedha ya tax. Hili tukio Jack chain analisimulia adi leo hii.
 
Upuuzi mwingine.sisi tuna mambo yetu ya ndani ya nchi ya kuleta maendeleo wewe unatuletea mambo ya marehemu.
 
mkuu ukiona watu wanachangia thread zaidi ya 10 kisha wewe ndio ukawa unaharibu thread basi jua kati ya hao 10 wewe nini mwendawazimu

Dada yangu wee,mwendawazimu ni yule anayeanzisha thread ambazo hazimsaidii mtanzania kwa lolote.Kuna maswala mengi katika nchi kwa sasa siyo ujinga kama huu.
 
Back
Top Bottom