crabat
JF-Expert Member
- Dec 28, 2012
- 4,323
- 2,210
Kwanza nawapa pole wakenya kwa yaliyowakuta, Hatimae operesheni imemalizika na magaidi wote wameuawa, hivi ingekuwa ndio magaidi wameteka jengo Tanzania, vyombo vyetu vinauwezo kwa kukabiliana na tukio gumu la kigaidi? Wataalam tujuzeni.
Naliamini jeshi letu na vijana wa FFU nawaamini...na operation kama ile wala isingefika jumatatu , siku moja tu tungewamaliza.
usidharau kabisa JWTZ na FFU wa Tz ni wazoefu na wana mafunzo ya hali ya juu...na tukio kama lile wakenya ukweli usemwe wameshindwa na baada ya pole na huzuni kupita utaona wakenya watakavo kuja juu kuwataka wahusika wote wa jiuzulu....
operation gani mpama jeshi lote lishindwe kuwa smoke out watu watano tu kwa siku nne? kama walikua wamejificha ndani ya kajichumba na tabu kuwapata jee huo mlango au dirisha halivunjiki kwa RPG ? Mpaka uangushe Gorofa 3 ? kuna jambo lime fichwa hapa wakenya wame pigwa changa la macho....kuna uwezekano mkubwa kumefanyika jinai nyengine ndani ya ku ransack mali za watu na baadae kuangusha jengo ili kuficha uhalifu huo...
hivo jeshi letu lipo juu ndugu....wala mtu asilinganishe kwa dharau ati mbona wamwaga acid mbona hawapatikani hayo yana fanyika mafichoni ...
poleni kenya lakini vijana wenu wa usalama wana hitaji kuchunguzwa