inakuwaje mnakuwa wapenzi

CharmingLady

JF-Expert Member
Apr 16, 2012
18,250
12,868
mamboz wana jf, polen kwa kuimiss jf. Hivi ni kwanini watu wanaweza kumudu kuwa wapenzi "boyfriend na girlfriend" kwa muda wa mwaka au zaidi ya mwaka then wakifunga ndoa hawamalizi hata mwaka wanatalikiana?? hii inatokana na nini?
 
mamboz wana jf, polen kwa kuimiss jf. Hivi ni kwanini watu wanaweza kumudu kuwa wapenzi "boyfriend na girlfriend" kwa muda wa mwaka au zaidi ya mwaka then wakifunga ndoa hawamalizi hata mwaka wanatalikiana?? hii inatokana na nini?

'Mapenzi ya mbali' (marafiki bf + gf) matamu kwa wasio wanandoa lakini mapenzi ya ndani ya ndoa ni matamu zaidi kwa wanandoa wanaopendana kikweliii
 
'Mapenzi ya mbali' (marafiki bf + gf) matamu kwa wasio wanandoa lakini mapenzi ya ndani ya ndoa ni matamu zaidi kwa wanandoa wanaopendana kikweliii

Aisee Listener Asante kutujuza hili, kumbe maisha ya ndoa ni matamu ehhh! Wale mnaonitishia mkome, Yule bf sasa ruksa kuwa mume
 
'Mapenzi ya mbali' (marafiki bf + gf) matamu kwa wasio wanandoa lakini mapenzi ya ndani ya ndoa ni matamu zaidi kwa wanandoa wanaopendana kikweliii

tatizo ama swali langu, kwanini wakioana hawadumu? while ktk urafk wa gf na bf walidumu let say mwaka au zaidi ya mwaka?
 
ndoa ni zaidi ya BF & GF, mkiwa BF & GF mnakuwa mnafichana mambo mengi sana na mara nyingi mnakuwa mnapena vile vitamu tu lakini vichungu hutokea mnapokuwa mmeoana na ndio hapo ngumi za macho hutokea
 
eish!ndoa ndoano bf na gf si ni mchezo wa ki nyumba nyumba kabla ya nyumba ambayo haitaki tena maigizo.
 
mamboz wana jf, polen kwa kuimiss jf. Hivi ni kwanini watu wanaweza kumudu kuwa wapenzi "boyfriend na girlfriend" kwa muda wa mwaka au zaidi ya mwaka then wakifunga ndoa hawamalizi hata mwaka wanatalikiana?? hii inatokana na nini?

Ukweli ni kwamba wakati wa "boyfriend na girlfriend" watu huishi maisha ambayo siyo real, I mean huwa wana-simulate maisha ya ndoa. Na ktk kipindi hicho chote kila mtu hujitahidi kuficha makucha yake na kumpendezesha mwenzake ili wafike salama katika ndoa. Baada ya hapo kila mtu humtambua mwenzie jinsi alivyo, na kugundua udhaifu mkubwa ambao husababisha washindwe kuvumiliana na kujikuta wakipeana talaka.

Na pia ahadi nyingi ambazo hupeana kabla ya ndoa, huwa si za kweli. Ni hii hukatisha tamaa na kupunguza makali ya mapenzi baina ya wanandoa hao baada ya kufunga ndoa ....

Zaidi ya hapo, kuna suala la kujisahau. Wengi wakishaingia kwenye ndoa hudhani wamefika na kusahau yale mambo mazuri waliyokuwa wakifanyiana na kupeana kabla ya ndoa. Hii husababisha ndoa kupoza na kukosa msisimko na hivyo kuanza kuboa ...

Sabau zipo nyingi ila kwa sasa hizo zinatosha ...

HP
 
Mkiwa wana-ndoa mnachukuliana for granted, baadhi ya mambo yanakuwa ni wajibu wa kufanya na ukifanyiwa unaona ni haki yako (no appreciation)

Wengine wakishapata they don't try anymore yaani wameshapata, kwahio wanaacha kuendelea kupalilia mahusiano.

Kuishi na mtu ni kazi.., bila uvumilivu hamuwezi mkakaa utofauti lazima utapelekea kutokuelewana sasa kama nyote mkiwa ni mafahari its no wonder hamuwezi kukaa zizi moja..., tofauti na mwanzo mlivyokuwa ma-zizi tofauti
 
ndoa ni zaidi ya BF & GF, mkiwa BF & GF mnakuwa mnafichana mambo mengi sana na mara nyingi mnakuwa mnapena vile vitamu tu lakini vichungu hutokea mnapokuwa mmeoana na ndio hapo ngumi za macho hutokea

ni kweli lakn once mnapotaka kuoana mnakuwa mmefanya maamuzi magumu.pia mmekubaliana kuchukuliana madhaifu yenu kwanin msivumiliane? make hakuna mtu mkamilifu!
 
unategemea nini kama muwa umeisha utamu! halafu wengi waliozoea kufanya usanii wa ki-BF na GF ni vigumu sana ku-face real challenges in real life na hasa wanapokuja kutambua kwamba si kila king'aacho ni dhahabu...
 
tatizo ama swali langu, kwanini wakioana hawadumu? while ktk urafk wa gf na bf walidumu let say mwaka au zaidi ya mwaka?
Charminggirl, huu uzi ni mzuri. Ingawa sijashuhudia ndoa za muda mfupi ila naweza sema kitu hapa.

Mapenzi ya bf+gf ( urafiki wa kimapenzi/ngono) mara nyingi haujumuishi watu kuishi pamoja, na kutokana na hilo madhaifu mengi huwa yamejifisha, as mnakutana kwa muda mfupi tuu, then kila mtu anaishia kivyake. Hivyo ule muda mfupi wawili hao hujitahidi uwe ni wa furaha na kufarijiana, na ndio maana wote huenjoy.

Sasa tuje kwa wenyendoa, ambao kwa namna moja hulazimika kuishi "under the same roof, same room, same bed" lol. Hapo ndo kivumbi huanza. Kama ni uchafu utaanza kuonekana hapo, kama ni ulevi ndo utauconsider kwa uzito wake, kama ni ulafi nao utauona kwa mapana yake, nao ubahili utaujua. Hatimaye unagundua Aaaah! kumbe huyu mwenzangu yuko hivi? Sasa maisha ya ndoa na kuishi umoja katika wawili, yahitaji uvumilivu na kujitolea, wawili hao wanaposhindwa sasa kuyaishi mapungufu ya "one another" ndo hapo utasikia ooh! mwanamke mwenyewe hata sikumpenda, au mwanaume mwenyewe mlevi?

Hivyo mapenzi ya gf+bf, kwa mtazamo wangu hutawaliwa zaid na LUST na starehe zingine, ndo maana yananoga. Ukiingia kwenye majukumu ya kutoa hela ya mboga daily au kufua nguo za hubby na kumpikia, ndo hapoo sasa!
 
Last edited by a moderator:
unategemea nini kama muwa umeisha utamu! halafu wengi waliozoea kufanya usanii wa ki-BF na GF ni vigumu sana ku-face real challenges in real life na hasa wanapokuja kutambua kwamba si kila king'aacho ni dhahabu...

sasa kuna maana gani kuwa wapenz kabla ya ndoa. me nafikiri ndoa yahitaji uvumilivu wa hali ya juu make kila m1 anakuwa amekulia ktk mazingira tofauti tofauti!
 
asante sana bombu bombu jf ni kisima kisichoishiwa maji. ucpokunywa,utayaoga,ucpooga utanawa. so hata kama ushauri unaotolewa unakuwa hauna faida kwa wakat huo, lakn ipo cku utajikuta tu unaufanyia kazi. ubarikiwe!
 
Last edited by a moderator:
asante sana bombu bombu jf ni kisima kisichoishiwa maji. ucpokunywa,utayaoga,ucpooga utanawa. so hata kama ushauri unaotolewa unakuwa hauna faida kwa wakat huo, lakn ipo cku utajikuta tu unaufanyia kazi. ubarikiwe!

Karibu mwaya Charminggirl, maisha haya we acha tuu. Sometimes ujue tunashindwa na hisia za miili. Sual la ndoa lahitaji sana hekima na kuushirikisha ubongo pia. Hatatakiwi kutawaliwa na hisia zaidi. Eti utasikia mtu anamwambia mumewe "siku hizi hunipendi, mbona zile baby baby siku hizi hazipo?", ilhali wana watoto tayari. haya ndo mambo yanayoaleta mitafaruku kwa ndo za siku hizi.

Ndoa ni taasisi, bwana, haitofatuiani na Serikali, lol. Akili kichwani ndo itawale matendo yoote ya ndoani.
 
Last edited by a moderator:
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom