Inakuaje radio frequency zitofautiane?

Inakuaje radio frequency zitofautiane?

Wanawasikia kupitia azam dish
Kwahiyo kumbe hii Wasafi FM ni kachannel kadogo tu!.
PS: Kuna siku nilikuwa nacheki channel startimes nikakutana na Vatican channel siku nzima imekaa kama wameiconnect na CCTV za St. Peters' Basilica. Nikajiuliza wanafaidikaje pale wakati hakuna kipindi chochote!.
 
Yeye anamaanisha kuwa wasafi wanasikika nchi nzima kupitia frequency ya 88.9
Hiyo wasafi 88.9 ni kama e fm 97.3.

Sawa na ea radio 88.1

Vile vile clouds 88.5!

Hayo ni masaya ya dar, ila mikoani kuna code zao tofauti na hizo hapo juu.

Kwani wewe unataka kujua nini hasa?
 
Yah choice fm mkuu wanatumia frequency moja dom na dar sielewagi
Kama ndio hivyo, bado nitauliza inakuaje Radio Station isinunue frequency moja kwenye kila mkoa ili iweze kutengeneza a strong brand base!. Au ukubwa wa mawimbi unatofautiana kila mkoa?.
 
Kama ndio hivyo, bado nitauliza inakuaje Radio Station isinunue frequency moja kwenye kila mkoa ili iweze kutengeneza a strong base!. Au ukubwa wa mawimbi unatofautiana kila mkoa?.
Ndo hapo watu wajibu kitaalamu wengi hawajui kitu wanajibu pumba tu
 
Una maswali mazuri Ila naona baadhi hawajakuelewa itakuwa..

Siku zote nilikuwa nawaza kwanini hao tcra wasiwape hizo radio frequency moja nchi nzima kwa kila radio badala ya kuwa tofauti kila mahali
 
Kwa uelewa wangu wa darasa la saba iko hivi.

Unapoenda TCRA kuomba masafa wanakupa masafa ambayo hayaingiliani na chombo chochote kile katika eneo hilo. Hivyo ukienda mikoani pia watakupa masafa yako mwenyewe katika eneo hilo pia. Hii hufanyika ili kuepusha mwingiliano wa sauti au mawasiliano kwani masafa hayo hayo hutumika hata kwenye mambo ya kiusalama nchini.

Wakati mmoja nilikuwa nafanya kazi kwenye chombo kimoja cha habari, siku moja masafa yetu ya kutangazia yakayumba mfano ilikuwa ni 94.3 yakaenda 94.5. Redio ilikuwa haina usikivu mzuri na tuliingilia matangazo ya wenzetu na meneja ilibidi ashauri redio itolewe hewani ili kurekebisha tatizo kwani ni kosa kubwa kutoka nje ya mipaka yako ya matangazo.

Nimejaribu kuelezea kutumia elimu ya darasa la saba. Wenye Gidiriii 4 mnaruhusiwa kukosoa.
 
Una maswali mazuri Ila naona baadhi hawajakuelewa itakuwa..

Siku zote nilikuwa nawaza kwanini hao tcra wasiwape hizo radio frequency moja nchi nzima kwa kila radio badala ya kuwa tofauti kila mahali
Exactly!!.. au kama vipi mfano hizi Radio kubwa kwanini wasinunue frequency moja kwenye kila eneo (hata kama anaimiliki mwingine bei si maelewano) ili sisi wateja badala ya kufika mkoani naanza hangaika itafuta frequency ya pale.
Basi najua kabisa nikiwa mkoa wowote TZ nikiweka hiyo frequency nimeipata radio niitakayo!.
 
Kwa uelewa wangu wa darasa la saba iko hivi.

Unapoenda TCRA kuomba masafa wanakupa masafa ambayo hayaingiliani na chombo chochote kile katika eneo hilo. Hivyo ukienda mikoani pia watakupa masafa yako mwenyewe katika eneo hilo pia. Hii hufanyika ili kuepusha mwingiliano wa sauti au mawasiliano kwani masafa hayo hayo hutumika hata kwenye mambo ya kiusalama nchini.

Wakati mmoja nilikuwa nafanya kazi kwenye chombo kimoja cha habari, siku moja masafa yetu ya kutangazia yakayumba mfano ilikuwa ni 94.3 yakaenda 94.5. Redio ilikuwa haina usikivu mzuri na tuliingilia matangazo ya wenzetu na meneja ilibidi ashauri redio itolewe hewani ili kurekebisha tatizo kwani ni kosa kubwa kutoka nje ya mipaka yako ya matangazo.

Nimejaribu kuelezea kutumia elimu ya darasa la saba. Wenye Gidiriii 4 mnaruhusiwa kukosoa.
Darasa la 7 mwenzangu, kwani frequency ni gharama kuinunua mara ya kwanza au ni sababu ipi inayofanya kampuni isiamue kufanya "frequency takeover" mikoa yote!?.
 
Exactly!!.. au kama vipi mfano hizi Radio kubwa kwanini wasinunue frequency moja kwenye kila eneo (hata kama anaimiliki mwingine bei si maelewano) ili sisi wateja badala ya kufika mkoani naanza hangaika itafuta frequency ya pale.
Basi najua kabisa nikiwa mkoa wowote TZ nikiweka hiyo frequency nimeipata radio niitakayo!.
Na hichi ndicho hasa nachomaanisha...inazingua kila mkoa ukienda inabidi uanze fuatilia frequency ya radio yako upya kulingana na eneo. Hiyoharmonization ingeweka situation poa sana yani..

Sidhani kama Kuna redio zingeshindwa nunua yawezekana tcra ndo wanaweka usiku
 
je;
1. frequency ni gharama kuinunua first time?.
2. frequency ni gharama kulingana na wimbi husika?
3. gharama kuinunua toka kwa mtu?.
4. Kipi kinafanya kampuni moja isiwe na frequency moja kwa kila mkoa?.
5. Au frequency mfano 88.9 ikiwa Dsm ina nguvu kuliko hii hii 88.9 ikiwa Lindi?.
 
Darasa la 7 mwenzangu, kwani frequency ni gharama kuinunua mara ya kwanza au ni sababu ipi inayofanya kampuni isiamue kufanya "frequency takeover" mikoa yote!?.
Frequency hulipiwa na huwezi kulipia masafa hayo hayo kwa mikoa yote nchini kwani huko mikoani huwenda hayo masaa yanatumika kwa shughuli nyingine. Rejea andiko langu nimesema muda mwingine yanaweza kutumika hata kwa mambo ya usalama.
 
Kiongozi upo mkoa gani, ili wanaojibu waweze kukujibu ipasavyo?

Wajuvi wa mawimbi ya sauti ningependa kupewa somo kuhusu masuala ya mawimbi ya sauti.

Swali langu ni kuwa inakuaje Wasafi FM wanatumia 88.9 pekee kujitangaza wakati radio nyingine hawajitangazi kwa frequency moja.

Mfano ukiwa Dar es salaamClouds FM utawasikia kwa 88.5 ukiwa Dodoma utawasikia kwa 104.5.

Je ni suala la ukubwa wa mitambo, bei au ni kipi hasa kinafanya mmoja atumie frequency moja kujitangaza Tanzania nzima mwingine atumie frequency tofauti kujitangaza.

Ni taasisi binafsi, serikali au nani anayepanga na kumiliki hizi frequency?
 
Frequency hulipiwa na huwezi kulipia masafa hayo hayo kwa mikoa yote nchini kwani huko mikoani huwenda hayo masaa yanatumika kwa shughuli nyingine. Rejea andiko langu nimesema muda mwingine yanaweza kutumika hata kwa mambo ya usalama.
ooh kwa nilivyoelewa basi mfano 93.5 ikiwa ni radio dsm unaweza kuta ni wimbi la TISS morogoro so itabidi wenye radio wapewe wimbi jingine morogoro!.
Sasa kama ni hivi kwanini usiwepo utaratibu mawimbi fulani yawe ya usalama then kuanzia wimbi fulani yawe ya radio.
Yani mawimbi yapangwe kwa vigezo au wimbi la 98.6 dsm likienda Mtwara litakuwa na nguvu ndogo thats why itabidi wapewe wa karibu hilo wimbi!.
 
Back
Top Bottom