IMF wathibitisha, Serikali imeishiwa!

IMF wathibitisha, Serikali imeishiwa!

ukiwauliza wanakwambia uchumu unakuwa kwa 7% .........nimeshasema mwakani mwezi wa pili tutakuwa hatuna pesa....
 
ni kweli hapa, kuwa na sera nzuri za uchumi ni kitu kimoja lakini utekelezaji wake ni kitu kingine ambavyo inabidi viende hand in hand. Kuna gap kubwa kati ya wataalamu (watengeneza sera/wachumi) na wanasiasa (watekelezaji) hapa TZ ambao ndio wanasimamia hizo pande mbili na ndio maana resources zote zikiwa supported na amani iliyopo havionyeshi mafanikio yoyote ya maana.
Lakini kitu kikubwa kabisa kilichosahaulika ni kuwa uchumi wa kweli unajengwa na mtu mmoja mmoja ambapo linakuja suala la mass education (universal education) ili kumwezesha mtu binafsi atakapokuwa kuwajibika strategically kuleta mabadiliko. Sasa hapa serikali inawa mislead wananchi wake kwa kuwaambia kuwa itawafanyia kila kitu na kutowaeleza ukweli wa mambo pale mambo yanapohalibika. Kwa sasa hivi hakuna kabisa uwajibikaji wa binafsi hapa Tanzania na hasa kwenye taasisi za umma ambazo ndizo zinasimamia uchumi kwa vile hiyo spirit imeanzia uongozi wa juu. Tatizo kuu likiwa lilelile kuwa kwa kutowas sensitize kama individuals!
Hizi 'variables' (wataalamu+wanasiasa+wananchi=maendeleo) endapo zitakuwa katika mpango huo zinaleta maendeleo lakini ukizieuza "kichwa chini miguu juu" inakuwa equivalent na UMASIKINI kama tulivyo sasa!
Pamoja na ushabiki, kuna tatizo lingine la msingi......humu ndani, wengi wetu sio critical and analytical thinker bali ni political thinkers!!! Economic data zinahitaji critical and reasonable thinking na ndio maana unakuta mkuu EMT anabisha kwamba makusanyo hayaongezeki huku data alizo-quote zinaonesha kuna ongezeko!!!!! Tuliosoma A-Level mwishoni mwa miaka ya 1990 na early 2000's, watakumbuka kwamba ilikuwa ni NADRA sana, tena sana mtu kukuta amepata A or B ya Economics A-Level. Ilikuwa hata ukipata C, basi fahamu utakuwa upo kwenye 10 best students TZ !!!!! The reason behind, kulikuwa na paper 2 wakati ule(am not sure abt cku hizi). Paper I ni paper ambayo ilihitaji tu kusoma madaftari na kukariri na Paper II ilikuwa ni paper iliyohitaji zaidi critical and reasonable thinking kuliko kusoma madaftari. Kwa critical and reasonable thinker, angeweza kufanya na kufaulu Paper II hata bila ya kusoma lakini paper I ilikuwa ni lazima usome!!! More often than not, watu walikuwa wanababua sana (na kupata hata A) kwenye Paper I; lakini ilipokuja Paper II, A zote zingeweza kuwa dropped to C, or even D!!!! Economics, is all about critical and reasonable thinking, otherwise tutaishia ku-define economy in political persepectives ambazo most likely zinakuwa biased!! Lipumba, ni among the Greatest Economist in the country, lakini unatakiwa kuangalia jukwaa analotumia pale anapozungumzia masuala ya uchumi! Is it political or academic/proffesional platform!!! Atakapokuwa kwenye political platform lazima atakuwa bias as compared to professional platform.
wasomi wa tanzania-wachumi hawana nafasi, maamuzi yote ni ya kisiasa tu bila kupata ushauri wa kuaalamu
 
Merekani wanakopa itakuwa Tanzania? mnanchekesha!
Declaration of bankruptcy is always a shame especially at the amidst of ample resources!! and rampant corruption like TZ led by Msanii.
 
Wachumi wetu mko wapi?mbona mambo yanazidi kuwa magumu kwa walalahoi.Haya ndiyo maisha bora kwa kila mtanzania ?

Mkuu, kama Serikali ingelianzisha kitu kinachoitwa "Dawati la JF" kwa maana ya kutumia michango mbalimbali inayotolewa na wanaJF na kuifuatilia na hatimaye kuitekeleza, nadhani swali hili usingeliuliza. Wana JF ina watu wa makundi tofauti, kuna vilaza, kuna waropokaji lakini kuna great thinker wa ukweli ambao wameshaishauri Serikali hii kwa namna ya kipekee tena bure kabisa, ni suala la kuchambua na kutekeleza, lakini wapi wao wanajua ku-hire ma-consultants ambao hawana lolote zaidi ya kuja na li-document kuubwa lisiloweza kusomwa na viongozi wetu vilaza hawa, na likisomwa halifanyiwi kazi.
Kwa uchache tu,
JF
1.ilijadili mfumo mpya wa kuingiza magari wa TRA na athari zake
2. imejadili misamaha ya kodi na athari zake na nini serikali ifanye
3. ilijadili madhara ya kupanga mipango kwa mazoea
4. Ilijadili athari za mgao wa umeme na mapendekezo yake
5. ilijadili mfumo rafiki wa uwekaji wa viongozi wa kisiasa na athari zake
6. ilijadili ukubwa wa sserikali kwa maana ya mawaziri, manaibu waziri, makatibu wakuu, wakurugenzi, manaibu katibu wakuu, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na madhara yatakayosababishwa na "Diminishing return"
7. ilijadili mfumo mbovu wa uchaguzi wa biashara ya kura badala ya uhalisia wa sera
8. ilijadili madhara ya gharama kubwa za uchaguzi kwa maana ya machapisho ya fulana, kofia, khanga, suruali, magamba, magwanda, chai simple, mikopo ya kina mama lishe isiyozingatia ushindani wa kimikopo, kumbuka pesa zote hizi zina-loose track ya kuwa monitored na mfumo wa mzunguko wa fedha,
9.ilijadili madhara ya tume ya uchaguzi kuwalea viongozi wabovu na kudharau matokeo halali ya wapiga kura,
10. ilijadili madhara ya chama tawala kutozingatia ushauri wa kitaalamu katika maamuzi ya kitaifa
11. ilijadili ubaya wa safari za kwenda nje zinazokuwa-spearheaded na mkuu wa nchi
12. ilijadili madhara ya kutochukua hatua kwa wahujumu wa mali za umma kuwa impact yake ni kila mmoja kuwa mhujumu wa mali za umma
13. ilijadili madhara ya kutokuwa na Reli ya Kati, Kusini, Arusha na madhara yake kwa uchumi kuwa kuleta mahitaji makubwa ya magari makubwa "trucks" kwa ajili ya kusafirisha miziggo na hatimaye kuwa na demand kubwa ya mafuta ya diesel na petrol(madhara yake yapo wazi)
14. imejadili madhara ya kutokuwa na shirika la ndege kuwa kuua hub ya nchi hivyo kuudhoofisha utalii na mengineyo
15. imejadili mishahara midogo ya walimu hivyo kupelekea walimu kutokuwa na moral ya kazi na kuhama fani hivyo kuwa na graduate wabovu
16. imejadili ......kila kitu
17. ilijadili madhara ya wabunge wa kuteuliwa kuwa hawafanyi kazi yoyote zaidi ya kula stahili na kupiga meza kupitisha hoja dhaifu na dhalili za serikali
18. ilijadili matumizi ya serikali katika kununua magari ya GX V8 kwa ajili ya kuchukua wakurugenzi kutoka mbezi beach hadi posta na kuwarudisha
19. ilijadili hata wizi wa vifaa pale bandarini kuwa utafukuza watumiaji wa bandari yetu toka Congo, Zambia, burundi, Uganda, Rwanda
20. ilijadili madhara ya familia za viongozi na watendaji wa serikali nao kuwa viongozi na watendaji wa serikali kwa maana ya matumizi resources za serikali
21...
Orodha ni ndefu mkuu, cha msingi waambie kuwa wachumi wapo, ma-injia wapo, wahasibu wapo, wanasheria wapo lakini nao wako bize kwenye kufisidi mali za umma kama viongozi wao wanavyofanya.
 
Hakuna kitu kinakula hela ya serkali kama magari - haya ma-STK. Bili ya mafuta ni noma, hasa wakati huu wa joto ambapo hayazimwi hata yakipaki ili kibosile akute AC imepooza. Usiseme kuhusu service. Service ya kumwaga mafuta ya STK inaweza kupitiliza hata Shillingi Millioni moja.
 
Merekani wanakopa itakuwa Tanzania? mnanchekesha!
Mkuu FF, sidhani kama kukopa ni tatizo, ni utaratibu wa kawaida tu. tatizo letu hapa ni kuwa (kulingana na taarifa nilizoziona hapa) tunatumia zaidi kuliko tunavyokusanya. Hii inamaanisha kuwa tunalazimika kukopa ili kufidia pale tunaposhindwa kukusanya. isingekuwa vibaya kama tungekuwa tunakopa kwa ajili ya midari ya maendeleo kwa sababu ingekuja kulipa hayo madeni baadaye. hatari ni kuwa tunakopa kwa ajili ya kughramia recurrent expenditure. Ukiona hali kama iyo, basi ujue kuwa tunaelekea kule kwa Greece
 
Mficha ugonjwa kifo humuumbua.! Na masharti mapya ya kukopa ndio hayoo kama yalivyotolewa na Uingereza, serikali inaongozwa na ma poyoyo .! Kutegemea kodi ya sigara na pombe
 
Unakopa ili katika matumizi ya bajeti yako ya trilioni 13.5, over 8 trillioni goes to posho na mishahara and the rest ndio kwenye shughuli za maendeleo ya walipa kodi? Come on now. Angalia Marekani wanapokopa wanafanya nini na matumizi yao. Kukopa kwa serikali yoyote sio tatizo, unakopa kwenda kufanyia nini? na unachokifanya kitasaidia kuweza rudisha mkopo au atleast punguza mkopo in the future parallel to lifting the rural mass?
Brother kila siku nawaambia watu wa humu JF kuwa achaneni na wehu wa humu, wamo wengi tu. Unapoteza nguvu nyingi kumfafanulia jambo la msingi asiyestahili. Kumbukeni kila soko lina mwehu wake!
 
Mkuu, umeongea point sana, ila kuna mahali umepiga msituni kidogo. Unaposema kuwa asilimia 60 ya bajeti imekwenda kwenye mishahara na Posho, na kiasi kilichosalia kikaenda kwenye maendeleo siyo kweli. Kwa heasabu nyepesi kabisa, unachotaka kuwaambia watanzania ni kwamba Bajeti ya Tanzania= Posho+ Mishahara+ Maendeleo. Kama hiyo ndiyo tafsiri yako ya Bajeti, utakuwa umepotoka. Tafsisi sahihi ni hii:

bajeti ya Tanzania= Mishahara+Posho+ Matumizi ya kawaida ( mafuta, vitabu, madawa, ukarabati nk)+ maendeleo. Kwa tafsiri halisi ya serikali( kwa mujibu wa vitabu vya bajeti) bajeti yetu = Personal Emoluments ( Mshahara na mafao)+ Other charges ( ghrama za uendeshaji) + developement Expenditure( Maendeleo). Kwa miaka mingi sasa, bajeti ya maendeleo imekuwa ni kama asilmia 20 tu ya bajeti nzima.

Kwenye tafsiri yako, utakuwa umesahau fedha za uendeshaji ( other charges ) ambazo ni karibia asilimia 40 ya pesa pesa zote za matumizi ya kwaida yaani ( recurrent Expenditure)

Viginevyo, point zako ni za msingi sana.

Kwani mishahara siyo matumizi ya kawaida?
 
Serikali ya Ugiriki imeanguka jana tu kwa mambo ya hivihivi, matumizi makubwa kuliko mapato. Na huko ni Ulaya. Mimi kwakweli naogopa.
 
hapa nakukubali mkuu maana Mzee Mwnakijiji alitoa hapa (bureeeeeeeeeeee) draft ya katiba. Pia alitoa structure ya Bodi ya Mikopo ambapo ilikuwa wazi tu! Lakini kaulize kiasi ambacho Werema na Celine Kombani wamespend katika kupindisha sheria ya katiba. Angalia wanafunzi masikini ambao wangeliweza kuliondoa taifa hili hapa lilipo walivyokosa nafasi za kusoma vyuo!
Mkuu, kama Serikali ingelianzisha kitu kinachoitwa "Dawati la JF" kwa maana ya kutumia michango mbalimbali inayotolewa na wanaJF na kuifuatilia na hatimaye kuitekeleza, nadhani swali hili usingeliuliza. Wana JF ina watu wa makundi tofauti, kuna vilaza, kuna waropokaji lakini kuna great thinker wa ukweli ambao wameshaishauri Serikali hii kwa namna ya kipekee tena bure kabisa, ni suala la kuchambua na kutekeleza, lakini wapi wao wanajua ku-hire ma-consultants ambao hawana lolote zaidi ya kuja na li-document kuubwa lisiloweza kusomwa na viongozi wetu vilaza hawa, na likisomwa halifanyiwi kazi.
Kwa uchache tu,
JF....
.......
.........
......
Orodha ni ndefu mkuu, cha msingi waambie kuwa wachumi wapo, ma-injia wapo, wahasibu wapo, wanasheria wapo lakini nao wako bize kwenye kufisidi mali za umma kama viongozi wao wanavyofanya.
 
"Year","Tanzania"
"2004","2175000064"
"2005","2074000000"
"2006","2375000064"
"2007","2910000128"
"2008","2915000064"
"2009","3206000128"
"2010","3687000064"

Semeni, semeni. In US$.

Tazama ongezeko toka Kikwete aliposhika na tazama alivyokuta. Mnataka na za nyuma? Hiyo Tanzania foreign Reserves.
source: Tanzania - Reserves of foreign exchange and gold - Historical Data Graphs per Year
Yea, this is impressive, but the way we are doing now, by obtaining loans to foot recurent expenditure, we are going to erode our impressive reswerves soon, and that is not health for our economy
 
Hapo panaopoonekana aid as total % of budget kuwa inashuka haina maana kuwa wanakopa less,bali ni kwamba mapato ya ndani yameongezeka lakini bila kuchukua hatu yoyote ya kupunguza aid money.

Ama kweli, onyesha na kabla ya kuchukuwa nchi Kikwete ilikuaje? hiyo ulioonesha tu haina haja ya kuelezewa inakusuta

JF Premium Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png



Join Date : 2nd November 2007
Posts : 8,553
Rep Power : 83


[h=2]
icon1.png
Re: IMF wathibitisha, Serikali imeishiwa![/h] [TABLE="class: cms_table_cms_table"]
[TR]
[TD]Period[/TD]
[TD]Domestic Revenue (Tsh)[/TD]
[TD]Foreign Aid (Tsh)[/TD]
[TD]Overall Budget (Tsh)[/TD]
[TD]AID (Ushoga) as % of total budget[/TD]
[TD]Domestic Revenue as % of total budget[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2007 – 2008[/TD]
[TD]3.5 trillion[/TD]
[TD]2.5 trillion[/TD]
[TD]6.1 trillion[/TD]
[TD]41 %[/TD]
[TD]57 %[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2008 – 2009[/TD]
[TD]4.8 trillion[/TD]
[TD]2.4 trillion[/TD]
[TD]7.2 trillion[/TD]
[TD]33 %[/TD]
[TD]66 %[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2009 – 2010[/TD]
[TD]6.3 trillion[/TD]
[TD]3.1 trillion[/TD]
[TD]9.5 trillion[/TD]
[TD]33 %[/TD]
[TD]66 %[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2010 – 2011[/TD]
[TD]8.3 trillion[/TD]
[TD]3.2 trillion[/TD]
[TD]11.6trillion[/TD]
[TD]28 %[/TD]
[TD]72 %[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]2011 - 2012[/TD]
[TD]6.7 trillion[/TD]
[TD]3.9 trillion[/TD]
[TD]13.5 trillion[/TD]
[TD]28 %[/TD]
[TD]49 %[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Unakopa ili katika matumizi ya bajeti yako ya trilioni 13.5, over 8 trillioni goes to posho na mishahara and the rest ndio kwenye shughuli za maendeleo ya walipa kodi? Come on now. Angalia Marekani wanapokopa wanafanya nini na matumizi yao. Kukopa kwa serikali yoyote sio tatizo, unakopa kwenda kufanyia nini? na unachokifanya kitasaidia kuweza rudisha mkopo au atleast punguza mkopo in the future parallel to lifting the rural mass?

Marekani wanakopa na pesa nyingi zinaishia kwenye vita visivyo na tija..Afghanistan, Iraq na Libya.
 
Nilikuja na hii hapa mmeshindwa kuijibu mpaka sasa:
Mkishindwa hoja huwa mnaanza fujo, hata hapa unaanzisha hayohayo, hamna cha kusema;

Weka idadi ya barabara za lami kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Shule kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Waalimu kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Zahanati kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Viwanda kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Utalii kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Umeme kabla ya Kikwete
Weka idadi ya Maji kabla ya Kikwete
Weka idadi ya kazi kabla ya Kikwete
Weka idadi ya biashara kabla ya Kikwete
Weka idadi ya umaskini kabla ya Kikwete
Weka idadi ya kilimo kabla ya Kikwete
Weka idadi ya bidhaa zinazopita bandari zetu kabla ya Kikwete
Weka akiba ya fedha tulokuwa nayo kabla ya Kikwete


Ukimaliza weka na idadi ya wakati huu wa Kikwete, itayokuwa zaidi ya leo hii wakati wa Kikwete, mimi naihama CCM leo hii.

Ili kuwasaidia, nikaweka data hizi hapa ambazo zinafuta swali la 14 hapo chini (Akiba ya nje (foreign reserve), nawapa fursa tena tuendelee na mengine 13 yakiyobaki, msilete hadithi ndefu zisizokuwa na "data", leteni hoja yakinifu sio ubunifu:
quote_icon.png
By FaizaFoxy
"Year","Tanzania"
"2004","2175000064"
"2005","2074000000"
"2006","2375000064"
"2007","2910000128"
"2008","2915000064"
"2009","3206000128"
"2010","3687000064"

Semeni, semeni. In US$.

Tazama ongezeko toka Kikwete aliposhika na tazama alivyokuta. Mnataka na za nyuma? Hiyo Tanzania foreign Reserves.
source: Tanzania - Reserves of foreign exchange and gold - Historical Data Graphs per Year



  1. Weka idadi ya barabara za lami kabla ya Kikwete
  2. Weka idadi ya Shule kabla ya Kikwete
  3. Weka idadi ya Waalimu kabla ya Kikwete
  4. Weka idadi ya Zahanati kabla ya Kikwete
  5. Weka idadi ya Viwanda kabla ya Kikwete
  6. Weka idadi ya Utalii kabla ya Kikwete
  7. Weka idadi ya Umeme kabla ya Kikwete
  8. Weka idadi ya Maji kabla ya Kikwete
  9. Weka idadi ya kazi kabla ya Kikwete
  10. Weka idadi ya biashara kabla ya Kikwete
  11. Weka idadi ya umaskini kabla ya Kikwete
  12. Weka idadi ya kilimo kabla ya Kikwete
  13. Weka idadi ya bidhaa zinazopita bandari zetu kabla ya Kikwete
  14. Weka akiba ya fedha tulokuwa nayo kabla ya Kikwete
 
Sawa sawa mkuu. Ebu tusaidiane kuchambua hili:

Mkullo June 2011


Mheshimiwa Spika, kwa upande wa matumizi, katika mwaka 2011/12 Serikali imepanga kutumia jumla ya shilingi
bilioni 13,525.9 kwa matumizi ya kawaida na maendeleo. Kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi bilioni 8,600.3 kimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida, ikijumuisha shilingi bilioni 3,270.3 kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa Serikali, taasisi na wakala za Serikali na shilingi bilioni 1,910.4 kwa ajili ya Mfuko Mkuu wa Serikali.

Aidha, jumla ya shilingi bilioni 4,925.6 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, ambapo shilingi bilioni 1,871.5 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 3,054.1 ni fedha za nje.

Mapato:
A: Mapato ya Ndani 6,775,952
(i) Mapato ya Kodi (TRA) 6,228,836
(ii) Mapato Yasiyo ya Kodi 547,116
B: Mapato ya Halmashauri 350,496
C: Mikopo na Misaada ya Nje 3,923,551
D: Mikopo ya Ndani 1,204,262
E: Mikopo ya Masharti ya Kibiashara 1,271,634
JUMLA YA MAPATO YOTE 13,525,895

F: Matumizi ya Kawaida 8,600,287
(i) Mfuko Mkuu wa Serikali 1,910,376
(ii) Mishahara 3,270,292
(iii)Matumizi Mengineyo 3,419,619
Wizara 2,727,472
Mikoa 49,981
Halmashauri 642,166

G: Matumizi ya Maendeleo 4,924,608
(i) Fedha za Ndani 1,871,471
(ii)Fedha za Nje 3,054,137
JUMLA YA MATUMIZI YOTE 13,525,895

---
Ukisoma katika ufunguzi utaona kuna takwimu zimefinywa finywa, hazielezwi zimeenda wapi na mantiki yake ni matumizi ya kawaida in the form of posho, mishahara, repairs za majengo haya na yale, dhfa za kitaifa n.k - kwa ufupi i still hold kwamba 60% of the budget goes to other things than maendeleo ya Mtanzania. Thats the bottomo line.

gmosha48 said:
Mkuu, umeongea point sana, ila kuna mahali umepiga msituni kidogo. Unaposema kuwa asilimia 60 ya bajeti imekwenda kwenye mishahara na Posho, na kiasi kilichosalia kikaenda kwenye maendeleo siyo kweli. Kwa heasabu nyepesi kabisa, unachotaka kuwaambia watanzania ni kwamba Bajeti ya Tanzania= Posho+ Mishahara+ Maendeleo. Kama hiyo ndiyo tafsiri yako ya Bajeti, utakuwa umepotoka. Tafsisi sahihi ni hii:

bajeti ya Tanzania= Mishahara+Posho+ Matumizi ya kawaida ( mafuta, vitabu, madawa, ukarabati nk)+ maendeleo. Kwa tafsiri halisi ya serikali( kwa mujibu wa vitabu vya bajeti) bajeti yetu = Personal Emoluments ( Mshahara na mafao)+ Other charges ( ghrama za uendeshaji) + developement Expenditure( Maendeleo). Kwa miaka mingi sasa, bajeti ya maendeleo imekuwa ni kama asilmia 20 tu ya bajeti nzima.

Kwenye tafsiri yako, utakuwa umesahau fedha za uendeshaji ( other charges ) ambazo ni karibia asilimia 40 ya pesa pesa zote za matumizi ya kwaida yaani ( recurrent Expenditure)

Viginevyo, point zako ni za msingi sana.

Msilumbane waungwana, mnachozungumza ni kimoja. tofauti yenu, wakati gmosha matumizi ya stionary, fuel, ukarabati nk umeyaweka kwenye posho na mishahara na kubaki na takribani 20% kwa miradi ya maendeleo; mwenzio hizo other charges kazijumuisha kuwa ziko kwenye maendeleo na hivyo kukamilisha takriban 40% ya total bdget.

My note. Pesa for other charges, zinaweza kupunguzwa kuondoa misafara ya viongozi inayotumia magari mengi, kupunguza/kuondoa matumiz ya magari ya kifahari yanayokunywa mafuta mengi, wakachukua gari simple ndo zikawa kwa matumizi ya office. na kuepuka kila mkuu wa idara kuwa na gari lake na bajeti yake, zikatafutwa costa/isuzu za kuwafuata wafanyakazi na kuwarudisha nyumbani,
 
"Year","Tanzania"
"2004","2175000064"
"2005","2074000000"
"2006","2375000064"
"2007","2910000128"
"2008","2915000064"
"2009","3206000128"
"2010","3687000064"

Semeni, semeni. In US$.

Tazama ongezeko toka Kikwete aliposhika na tazama alivyokuta. Mnataka na za nyuma? Hiyo Tanzania foreign Reserves.
source: Tanzania - Reserves of foreign exchange and gold - Historical Data Graphs per Year

Tunaongelea hali ya sasa ya kiuchumi na muelekeo wake, Wakuu wamejaribu kuchambua bila ya kuingiza siasa ndani wacha tubakie kwenye mkondo huo tafadhali...
 
Back
Top Bottom