Imeniuma nikishuhudia mjukuu wangu akikata roho

JAMANI NIPELEKE WAPI HAYA MALALAMIKO?
Naandika hii post nikiwa na uchungu mkubwa sana kwani ndionimetokea West Kilimanjaro kumzika mjukuu wangu aliekuwa na umri wa miezi sita. Hakika huyu malaika hakustahili kutoweka mapema hivi ila ni kwasababu tu ya uzembe wa manesi na madaktari.
Mnamo saa saba na robo hivi usiku nilishuhudia malaika huyu (Dorris) akikata roho hodini katika hospitali ya Levolosi Arusha ambako ndio ward ya watoto wa Mt Meru ilipo. Dorris alifikishwa hospitalini hapo mnamo saa 5 kamili usiku na alipopimwa aligundulika kuwa anaumwa na Pnewmonia which also triggered her sugar mpaka kufikia 19. Alichomwa sindano, akawekewa oxygen na wauguzi wakaendelea na shughuli zao. Dorris alijatahidi sana kutetea uhai wake kwa takribani masaa mawili tukiwa mimi na mama yake (mkwe wangu) tunamkodolea macho kwani hatukuwa na la kufanya. Basi ilipotimia saa saba na robo mjukuu wangu alivuta pumpzi yake ya mwisho akiwa mikononi mwa mama yake namimi nikiwa pembeni. Hakukuwa na Nurse wala Daktari.
THE WHOLE SCENARIO:
1. Dorris alianza kuugua nyumbani mnamo majira ya saa 1 usiku na kupelekwa private hospital maeneo ya kaloleni (Arusha) inayoitwa Eben Hospital. Daktari aliyekuwepo zamu alimpima na akasema hana ugonjwa wowote. Lakini cha kushangaza akampa vichupa vitatu vya dawa alivyowatoza shs 30,000 halafu akamwambia mama yake Dorris ampeleke mtoto kwa Dr Mohamed Hospital iliyopo tank la maji. Kama hana ugonjwa kwanini ampe dawa na kum refer kwenda hospitali nyingine?
2. Mama Dorris na mototo walifika kwa Dr Mohamed majira ya saa nne usiku hivi. Walivyofika hospitalini hapo, wauguzi hawakujali kuwapokea wala kuwasikiliza isipokuwa walimwambia mama Dorris ampeleke mototo Mt Meru Hospital kwasababu wao wana wangonjwa wengi sana. Mama Dorris aliondoka na mototo wake kuelekea Mt Meru Hospital.
3. Walifika Mt Meru Hospital mnamo saa nne na nusu na kupokelewa na Dr Longdare ambaye ndio alikuwa Daktari wa zamu. Dr Longdare hakuwapatia huduma yoyote zidi ya kumwambia mama Dorris kwamba idara ya watoto imehamishiwa Levolosi hivyo ammpeleke mototo huko. Mama Dorris ndo akanipigia simu na tukakutana Levolosi. N.B. Baba yake Dorris ni mototo wangu anaefanya kazi mbuga za wanyama hivyo siku hiyo alikuwa mbugani.

MALALAMIKO
1. Kwanini Daktari wa Eben akasema Dorris hana matatizo yoyote na kisha kum refer kwenye hospitali nyingine huku akiwa amemcharge shs 30,000?
2. Kwanini Dr Longdare wa Mt Meru hospital haku treat issue ya Dorris kama emergency na ampe matibabu pale pale Mt Meru badala ya kupoteza muda na motto kukimbia kwenye idara ya watoto?
3. Kwanini ma nurse wa Levolosi hawakuendelea na jitahada za kuokoa maisha ya Dorris ila walichofanya ni ushahidi tu wakumchoma sindano na kumuwekea oxygen na kisha kwenda kukaa zao ofisi. Nilitegemea mgonjwa mahututi kama huyu angefariki manasi wakiwa wanhangaika huku na kule lakini kwa Dorris ni kinyume kwani kafariki akiwa mikononi mwa mama yake na mimi peke yangu nikiwa pembeni.
4. Baada ya mototo kufariki nikaomba kama naweza pewa mwili ili niupeleke mortuary. Waliniambia kuna gari ya hospitali ndio itakao upeleka mwili wa mototo. Nilisubiri kuanzia saa saba ile mpaka saa 10 za usiku gari haikutokea ndio mwishowe wakaamua kuniruhusu niuchukue mwili wa mjukuu wangu.
5. Tukiwa Levolosi baada ya mototo kufariki mama Dorris alipatwa na uchungu sana na ilimpelekea kuzirai mara tatu. Cha ajabu mama Dorris alipozirai alikuwa anahudumiwa na wagonjwa wenzake na siyo ma Nurse.

SAFARI YA MT MERU HOSPITAL/MORTUARY
1. Tulifika mortuary saa kumi na nusu, tuligonga mpaka saa kumi na moja kasorobo lakini hapakufungukiwa. Wakati huo mkwe wangu mama Dorris yuko kwenye gari amezimia tena.
2. Ilibidi nitoke kuelekea main building ya Mt Meru na nilipofika mapokezi nikamkuta Dr Longdare akiwa amekaa so relaxed pale reception ni kikombe chake cha chai. Nikamwambia nina shida mbili kama ifuatavyo.
Ø Nina motto amefariki hivyo nataka kumpeleka mortuary, hii alinipa maelekezo na nikasaidiwa
Ø Pili mama wa marehemu yuko kwenye amezimia hivyo ninaomba apatiwe matibabu. Dr Longdare huku akiwa pale pale mapokezi na kikombe chake cha chai akasema “aaaaaaaaaaaaaaaa huyu mpeleke tu nyumabi bwana”. Nikamwambia hapana amesha zimia mara tatu akasema “ aaaaaaaaaaaaa kwani kuzimia ni nini bwana? Kweli at that stage I had to lose temper and I asked him what the hell he was doing there. Cha kushangaza aka charge na kuniambia “You must be mother ****er” – imagine loudly. Infact I didn’t know what he meant. Basi baada ya kucharge sana akaniambia mchukue mgonjwa wako mpeleke kule (waliko manesi)
3. Mama Dorris alikuwa amezimia hivyo nilikuwa nahitaji msaada, nilipoenda kwenye chumba cha ma Nurse kuwaomba msaada wakanielekeza sehemu ilipo wheelchair ili nikamlete mgonjwa. Muda wote huo mkwe wangu alikuwa kwenye gari. Nikaendesha wheelchair mwenyewe nikaenda kwenye gari na kuanza kumbeba mama Dorris. Mungu saidia kukatokea watu walioleta wagonjwa wao hivyo walinisaidia kumteremsha mama Dorris na kumpeleka ndani. Note for all that time Dr Longdare was in the same place enjoying his cup of tea.
4. Wakati nampeleka mama Dorris ndani napishana na Nurse mwingine. Nikijua angenisaidia ila aliishia kunikejeli na kusema “Hivi ni nini tena? Nyie hamkwenda Loliondo? Sikumjibu nikaendelea kumsukuma mama Dorris kwenye wheelchair
5. Finally Dr Longdare akaja, akampima mama Dorris na kumuwekea drip mbili mpaka saa moja asubuhi? Je kama hakuwa mgonjwa kwanini alimuwekea drip? Yeye alisema nimpeleke nyumbani?

Bye: Blue Balaa.
Mkubwa usiiache ipite
Tuma barua kwa waziri, director wa hospital service, mganga mkuu wa Mount Meru na RMO lakini pia hakikisha unapata mwanasheria mzuri

Pole sana lakini hii ndio hali halisi ya Tanzania kwa sasa... kila mtu kwenye idara karibia zote ni rais, waziri, mbunge, afisa utawala na spika... wachache sana wameamua kuendelea kujitolea

Kibaya zaidi ni kwamba tunamalizia hasira zetu kwa ndugu zetu wapendwa na kuacha wahusika wa chuki zetu wakiwa wamelalia vyumba vya mamia ya mamilioni ya pesa

Nadhani Dr. Longdare anafahamika na kuna watu walio karibu nae, hakikisha anapata hizi complaints katika family level na pia offcially

USIACHE LIPITE KWANI HAKI HAIPOTEI IWE NZURI AU MBAYA, UKIIACHA IPOTEE, ROHO YA MALAIKA DORRIS ITAKUSUTA
 
pole sana tumepoteza mjukuu kizembe nchi hii kwa sasa kila sekta imeharibika wanakula pesa na wanatoa huduma feki mungu amlaze mahala pema peponi mjukuu
JAMANI NIPELEKE WAPI HAYA MALALAMIKO?
Naandika hii post nikiwa na uchungu mkubwa sana kwani ndionimetokea West Kilimanjaro kumzika mjukuu wangu aliekuwa na umri wa miezi sita. Hakika huyu malaika hakustahili kutoweka mapema hivi ila ni kwasababu tu ya uzembe wa manesi na madaktari.
Mnamo saa saba na robo hivi usiku nilishuhudia malaika huyu (Dorris) akikata roho hodini katika hospitali ya Levolosi Arusha ambako ndio ward ya watoto wa Mt Meru ilipo. Dorris alifikishwa hospitalini hapo mnamo saa 5 kamili usiku na alipopimwa aligundulika kuwa anaumwa na Pnewmonia which also triggered her sugar mpaka kufikia 19. Alichomwa sindano, akawekewa oxygen na wauguzi wakaendelea na shughuli zao. Dorris alijatahidi sana kutetea uhai wake kwa takribani masaa mawili tukiwa mimi na mama yake (mkwe wangu) tunamkodolea macho kwani hatukuwa na la kufanya. Basi ilipotimia saa saba na robo mjukuu wangu alivuta pumpzi yake ya mwisho akiwa mikononi mwa mama yake namimi nikiwa pembeni. Hakukuwa na Nurse wala Daktari.
THE WHOLE SCENARIO:
1. Dorris alianza kuugua nyumbani mnamo majira ya saa 1 usiku na kupelekwa private hospital maeneo ya kaloleni (Arusha) inayoitwa Eben Hospital. Daktari aliyekuwepo zamu alimpima na akasema hana ugonjwa wowote. Lakini cha kushangaza akampa vichupa vitatu vya dawa alivyowatoza shs 30,000 halafu akamwambia mama yake Dorris ampeleke mtoto kwa Dr Mohamed Hospital iliyopo tank la maji. Kama hana ugonjwa kwanini ampe dawa na kum refer kwenda hospitali nyingine?
2. Mama Dorris na mototo walifika kwa Dr Mohamed majira ya saa nne usiku hivi. Walivyofika hospitalini hapo, wauguzi hawakujali kuwapokea wala kuwasikiliza isipokuwa walimwambia mama Dorris ampeleke mototo Mt Meru Hospital kwasababu wao wana wangonjwa wengi sana. Mama Dorris aliondoka na mototo wake kuelekea Mt Meru Hospital.
3. Walifika Mt Meru Hospital mnamo saa nne na nusu na kupokelewa na Dr Longdare ambaye ndio alikuwa Daktari wa zamu. Dr Longdare hakuwapatia huduma yoyote zidi ya kumwambia mama Dorris kwamba idara ya watoto imehamishiwa Levolosi hivyo ammpeleke mototo huko. Mama Dorris ndo akanipigia simu na tukakutana Levolosi. N.B. Baba yake Dorris ni mototo wangu anaefanya kazi mbuga za wanyama hivyo siku hiyo alikuwa mbugani.

MALALAMIKO
1. Kwanini Daktari wa Eben akasema Dorris hana matatizo yoyote na kisha kum refer kwenye hospitali nyingine huku akiwa amemcharge shs 30,000?
2. Kwanini Dr Longdare wa Mt Meru hospital haku treat issue ya Dorris kama emergency na ampe matibabu pale pale Mt Meru badala ya kupoteza muda na motto kukimbia kwenye idara ya watoto?
3. Kwanini ma nurse wa Levolosi hawakuendelea na jitahada za kuokoa maisha ya Dorris ila walichofanya ni ushahidi tu wakumchoma sindano na kumuwekea oxygen na kisha kwenda kukaa zao ofisi. Nilitegemea mgonjwa mahututi kama huyu angefariki manasi wakiwa wanhangaika huku na kule lakini kwa Dorris ni kinyume kwani kafariki akiwa mikononi mwa mama yake na mimi peke yangu nikiwa pembeni.
4. Baada ya mototo kufariki nikaomba kama naweza pewa mwili ili niupeleke mortuary. Waliniambia kuna gari ya hospitali ndio itakao upeleka mwili wa mototo. Nilisubiri kuanzia saa saba ile mpaka saa 10 za usiku gari haikutokea ndio mwishowe wakaamua kuniruhusu niuchukue mwili wa mjukuu wangu.
5. Tukiwa Levolosi baada ya mototo kufariki mama Dorris alipatwa na uchungu sana na ilimpelekea kuzirai mara tatu. Cha ajabu mama Dorris alipozirai alikuwa anahudumiwa na wagonjwa wenzake na siyo ma Nurse.

SAFARI YA MT MERU HOSPITAL/MORTUARY
1. Tulifika mortuary saa kumi na nusu, tuligonga mpaka saa kumi na moja kasorobo lakini hapakufungukiwa. Wakati huo mkwe wangu mama Dorris yuko kwenye gari amezimia tena.
2. Ilibidi nitoke kuelekea main building ya Mt Meru na nilipofika mapokezi nikamkuta Dr Longdare akiwa amekaa so relaxed pale reception ni kikombe chake cha chai. Nikamwambia nina shida mbili kama ifuatavyo.
Ø Nina motto amefariki hivyo nataka kumpeleka mortuary, hii alinipa maelekezo na nikasaidiwa
Ø Pili mama wa marehemu yuko kwenye amezimia hivyo ninaomba apatiwe matibabu. Dr Longdare huku akiwa pale pale mapokezi na kikombe chake cha chai akasema “aaaaaaaaaaaaaaaa huyu mpeleke tu nyumabi bwana”. Nikamwambia hapana amesha zimia mara tatu akasema “ aaaaaaaaaaaaa kwani kuzimia ni nini bwana? Kweli at that stage I had to lose temper and I asked him what the hell he was doing there. Cha kushangaza aka charge na kuniambia “You must be mother ****er” – imagine loudly. Infact I didn’t know what he meant. Basi baada ya kucharge sana akaniambia mchukue mgonjwa wako mpeleke kule (waliko manesi)
3. Mama Dorris alikuwa amezimia hivyo nilikuwa nahitaji msaada, nilipoenda kwenye chumba cha ma Nurse kuwaomba msaada wakanielekeza sehemu ilipo wheelchair ili nikamlete mgonjwa. Muda wote huo mkwe wangu alikuwa kwenye gari. Nikaendesha wheelchair mwenyewe nikaenda kwenye gari na kuanza kumbeba mama Dorris. Mungu saidia kukatokea watu walioleta wagonjwa wao hivyo walinisaidia kumteremsha mama Dorris na kumpeleka ndani. Note for all that time Dr Longdare was in the same place enjoying his cup of tea.
4. Wakati nampeleka mama Dorris ndani napishana na Nurse mwingine. Nikijua angenisaidia ila aliishia kunikejeli na kusema “Hivi ni nini tena? Nyie hamkwenda Loliondo? Sikumjibu nikaendelea kumsukuma mama Dorris kwenye wheelchair
5. Finally Dr Longdare akaja, akampima mama Dorris na kumuwekea drip mbili mpaka saa moja asubuhi? Je kama hakuwa mgonjwa kwanini alimuwekea drip? Yeye alisema nimpeleke nyumbani?

Bye: Blue Balaa.
 
madaktari na manerse wa leo hawana wito wa kazi zao kabisa, pole sana kwa yaliokukuta mkuu
 
mkuu nitapingana na hatua yoyote unayotaka kuwachukulia hawa watu zaidi tu ya kwenda kuwashauri.kwa sababu i hope wapo wachache pale so mkiwafukuza huduma haitakuwepo tena , but kawa madokta wapo wengi ,ok hamna shida
Acha utoto wewe, Kwa vile wapo wachache waendelee na kuwaua wagonjwa na sote tukae pembeni tukiwashangilia? Mbona huna huruma hivi? Nimesoma majibu ya wana JF bado sijapata lililonikuna. Mimi naamini anachotitaji mwasilisha mada ni ushauri wa nini kifanyike au afanye ili upuuzi huu usirudiwe tena. Naamini humu ndani wapo wenzetu waliobobea katika fani ya sheria wanaoweza kutufungua macho.
Uoza wa namna hii upo karibu katika kila pembe ya nchi. Ni lazima hatua za kuukomesha zianze sasa. Tutafakari,Tuchukue hatua kama Great Thinkers.
 
POLENI SANA blue balaa na family yako........INASIKITISHA mazingira ya kifo cha mjukuu wako kimetokana na uzembe wa ma DR na manesi wa hosp zote ulizopitia....japo tunajua kifo ni lazima kwa kila Bin Adam lakin huduma mbovu zinachangia vifo vya kizembe. Hao wakichuliwa hatua za kinidhamu itasaidia kuzuia vifo vya kizembe kwa wagonjwa wengine. Huyo aliyesema u PM na kumpa detail nyingne nyingi mpe anaweza kutoa msaada wa kuwa adabisha hao ma DR na manesi wengine....POLE SANA, BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE MILELE.......
 
Mkuu Pole sana, nimeumia sana tena sana inanikumbusha kifo cha mama yangu wakati niko mdogo sana, alifariki eti kwa kukosa maji(drips) maana aliharisha na kutapika sana, kutokana na umasikini wa familia yangu manesi wakakataa kutoa huduma wakitaka hongo....RIP Dorris...
 
Mkuu Pole sana, nimeumia sana tena sana inanikumbusha kifo cha mama yangu wakati niko mdogo sana, alifariki eti kwa kukosa maji(drips) maana aliharisha na kutapika sana, kutokana na umasikini wa familia yangu manesi wakakataa kutoa huduma wakitaka hongo....RIP Dorris...

Asante sana na pole wewe pia
 
POLENI SANA blue balaa na family yako........INASIKITISHA mazingira ya kifo cha mjukuu wako kimetokana na uzembe wa ma DR na manesi wa hosp zote ulizopitia....japo tunajua kifo ni lazima kwa kila Bin Adam lakin huduma mbovu zinachangia vifo vya kizembe. Hao wakichuliwa hatua za kinidhamu itasaidia kuzuia vifo vya kizembe kwa wagonjwa wengine. Huyo aliyesema u PM na kumpa detail nyingne nyingi mpe anaweza kutoa msaada wa kuwa adabisha hao ma DR na manesi wengine....POLE SANA, BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE MILELE.......

Asante sana pole na wewe pia
 
Mkubwa usiiache ipite
Tuma barua kwa waziri, director wa hospital service, mganga mkuu wa Mount Meru na RMO lakini pia hakikisha unapata mwanasheria mzuri

Pole sana lakini hii ndio hali halisi ya Tanzania kwa sasa... kila mtu kwenye idara karibia zote ni rais, waziri, mbunge, afisa utawala na spika... wachache sana wameamua kuendelea kujitolea

Kibaya zaidi ni kwamba tunamalizia hasira zetu kwa ndugu zetu wapendwa na kuacha wahusika wa chuki zetu wakiwa wamelalia vyumba vya mamia ya mamilioni ya pesa

Nadhani Dr. Longdare anafahamika na kuna watu walio karibu nae, hakikisha anapata hizi complaints katika family level na pia offcially

USIACHE LIPITE KWANI HAKI HAIPOTEI IWE NZURI AU MBAYA, UKIIACHA IPOTEE, ROHO YA MALAIKA DORRIS ITAKUSUTA

Asante na nimesha anza move
 
May de Angel's soul rest in peace but is this behaviour acceptable?

It is not only about public hospitals... but also private hospitals...

I lost my Beloved Father 7years ago due to the carelessness and inefficicnecy of Dr. Arab Of Aga Khan Hospital; We had complained to the Patient Support Department to Miss N. Bandali but to our surprise all the documents went missing form their side and suddenly there was no proof... Later on Dr. Arab was sacked from Aga Khan Hospital immediately ( Now the owner of Apollo Hospital- wheer by recently a child was suffering from Pneumonia and he failed to diagnose it and instead gave him Malaria Treatment; The child passed away )

Jamani at that time i was young, had no financial resources at all; i was helpless. I could nothing to give my Late Father Justice but today i know my rights; i have resources and i can fight... so Sir ( you who lost Dorris) i want to assure you i am with you in fighting this battle; just give me a shout out and i shall support you.

I'm doing this for my Beloved father; whose loss i feel till today....!!

Please let us all unite and fight against such behaviour; our family; our beloved's life is priceless will we wait to loose them before we raise our voice??

Where are those doctors who had sworn to save people's life? why do we have a vice versa now??

Please lets wake up; stand unite and fight!!!

BTW does any one of you know any NGO which can help and direct us to fight this?? We should contact them...Please help me..Please help my Father...Please Help Dorris..Please ehlp the lady who lost her mother due to carelessness...Please Help all others...Please Help........

Thanks and will PM you shortly
 
Yaani nimebahatika kusoma kisa hiki cha kusikitisha baada ya Ku google "Eben Hospital Arusha" ambapo kuna ndugu yangu kaniambia kuwa ameenda huko kufanyowa dabo cheki baada ya kutibiwa St Thomas na hali kuendelea kuwa mbaya. Sasa ndo nikapata mshtuko wa habari hii.

BLUE BALAA bado upo humu?
 
Back
Top Bottom