Binti mdogo anayemfungia ndani Mama yake mgonjwa aliyepooza kutwa nzima na kwenda kutafuta pesa za kumuhudumia inaumiza wengi mtaani

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,253
Ni Binti mdogo mwenye umri wa miaka 23,na mwenye mtoto mmoja Familia hii haina Baba kwani baba yao alishafariki Miaka mingi iliyopita na kijana aliyempa mimba binti alimtelekeza tangu mtoto akiwa ana miezi 6.

Mama wa huyu binti ana umri wa miaka 63 alikuwa mzima kabisa tangu kuzaliwa huku akifanya vibarua vya hapa na pale lakini miaka sita iliyopita ghafla alipata tatizo hili la kupooza viungo vya mwili, ulimi kuwa mzito na hivyo kushindwa kuongea vizuri, pamoja na kuzimia mara kadhaa kila wiki tatizo linalooendelea hadi sasa.

Kutokana na uwezo duni wa hii familia walishindwa kumpeleka Hospital kubwa kwa uchunguzi zaidi

Binti huyu amepangisha chumba kimoja kidogo akiwa yeye, mtoto wake wa kiume na mama yake huyo huku pembeni kukiwa na Ndoo yenye mfuniko wake ambae mama huyo hutumia kama choo usiku na mchana.

Alfajiri binti hujihimu kuandaa chai kwa ajili ya mama na mtoto wake ambae nae huenda shule na kumfungia mama yake ndani huku ufunguo akiacha kwa jirani hadi mwanae huyo ambae yuko la kwanza atakaporudi mchana na kumpa bibi yake chakula kilichopikwa usiku wa jana yake kwa ajili ya mlo wa mchana, hapo watajifungia ndani wote hadi binti atakaporudi saa moja usiku toka kibaruani.

Mara kadhaa bibi huyo amekuwa akizimia humo ndani na mjukuu huyo humwacha hivyo hivyo hadi fahamu zitakaporejea. Binti hiyo nilipata nafasi ya kumuuliza anagunduaje kama mama yake alizimia mchana na kunijibu kuwa hugundua hilo kutokana na kinyesi kutapakaa kitandani au chini au majeraha atakayomkuta nayo pindi arudipo jioni..

Kama kuna Umuhimu wa kuweka picha ya huyo Bibi mgonjwa basi ntaweka hapa.

Na hata kama kitapatikana wheelchair ♿ kwa ajili ya kumtoa nje wakati wa kuota jua pia itakuwa msaada mkubwa kwenye familia hii.

Wito wangu kwa Serikali iangalie Namna ya kusaidia aina hii ya wagonjwa kwani wapo wengi wanaopitia tabu na inatesa sana familia kwa kuwaletea umaskini na usongo mkubwa wa Mawazo.

Update :
Wengi naona wametaka namba ya binti na kabla sijafanya hivyo niliomba ridhaa ya binti kwanza na Amekubali.
Namba yake hii pia ipo whatsapp unaweza piga video call au picha kwa ajili ya kumuona mamake na huyo binti. 0685 52 86 30
 
Dah mpaka nimeumia. Sasa mkuu wewe ndio umefika hapo mpaka kufanya mahojiano na huyo binti anayemlea mama ake katika hali hiyo, so far umechukua hatua gani kuhakikisha anapata msaada zaidi ya kuleta hii habari hapa JF kama vile kuchukua number ya binti na vielelezo vingine kwaajili ya kupata mchango au kwenda taasisi yoyote ya umma ambayo inaweza ikachukua hatua kubwa zaidi katika kuhakikisha hiyo familia inapata msaada?
 
Haya maisha haya😥😥😥
Mama D maisha ni jinsi vile kila mtu anavyoyachukulia. Inaumiza kujua kuwa kuna watu wanaishi maisha ya aina haya na serikali ipo inayopaswa kutoa huduma kwa watu wenye matatizo kama haya. inapaswa kuwekwa mfuko wa kijamii kama ilivyo katika nchi za wenzetu kwaajili ya kushugurikia wazee na wenye matatizo.
Mbona wenzetu wameweza na wananchi wanakatwa kodi?
 
Mama D maisha ni jinsi vile kila mtu anavyoyachukulia. Inaumiza kujua kuwa kuna watu wanaishi maisha ya aina haya na serikali ipo inayopaswa kutoa huduma kwa watu wenye matatizo kama haya. inapaswa kuwekwa mfuko wa kijamii kama ilivyo katika nchi za wenzetu kwaajili ya kushugurikia wazee na wenye matatizo.
Mbona wenzetu wameweza na wananchi wanakatwa kodi?
Mchakato wa kiserikali ni mzuri Ila unachukua muda mrefu.Jamii yenyewe kuanzia mtaa husika ianze na hili.
 
Mama D maisha ni jinsi vile kila mtu anavyoyachukulia. Inaumiza kujua kuwa kuna watu wanaishi maisha ya aina haya na serikali ipo inayopaswa kutoa huduma kwa watu wenye matatizo kama haya. inapaswa kuwekwa mfuko wa kijamii kama ilivyo katika nchi za wenzetu kwaajili ya kushugurikia wazee na wenye matatizo.
Mbona wenzetu wameweza na wananchi wanakatwa kodi?

Inaumiza sana


Ni Binti mdogo mwenye umri wa miaka 23,na mwenye mtoto mmoja Familia hii haina Baba kwani baba yao alishafariki Miaka mingi iliyopita na kijana aliyempa mimba binti alimtelekeza tangu mtoto akiwa ana miezi 6.

Mama wa huyu binti ana umri wa miaka 63 alikuwa mzima kabisa tangu kuzaliwa huku akifanya vibarua vya hapa na pale lakini miaka sita iliyopita ghafla alipata tatizo hili la kupooza viungo vya mwili, ulimi kuwa mzito na hivyo kushindwa kuongea vizuri, pamoja na kuzimia mara kadhaa kila wiki tatizo linalooendelea hadi sasa.

Kutokana na uwezo duni wa hii familia walishindwa kumpeleka Hospital kubwa kwa uchunguzi zaidi

Binti huyu amepangisha chumba kimoja kidogo akiwa yeye, mtoto wake wa kiume na mama yake huyo huku pembeni kukiwa na Ndoo yenye mfuniko wake ambae mama huyo hutumia kama choo usiku na mchana.

Alfajiri binti hujihimu kuandaa chai kwa ajili ya mama na mtoto wake ambae nae huenda shule na kumfungia mama yake ndani huku ufunguo akiacha kwa jirani hadi mwanae huyo ambae yuko la kwanza atakaporudi mchana na kumpa bibi yake chakula kilichopikwa usiku wa jana yake kwa ajili ya mlo wa mchana, hapo watajifungia ndani wote hadi binti atakaporudi saa moja usiku toka kibaruani.

Mara kadhaa bibi huyo amekuwa akizimia humo ndani na mjukuu huyo humwacha hivyo hivyo hadi fahamu zitakaporejea. Binti hiyo nilipata nafasi ya kumuuliza anagunduaje kama mama yake alizimia mchana na kunijibu kuwa hugundua hilo kutokana na kinyesi kutapakaa kitandani au chini au majeraha atakayomkuta nayo pindi arudipo jioni..

Kama kuna Umuhimu wa kuweka picha ya huyo Bibi mgonjwa basi ntaweka hapa.

Wito wangu kwa Serikali iangalie Namna ya kusaidia aina hii ya wagonjwa kwani wapo wengi wanaopitia tabu na inatesa sana familia kwa kuwaletea umaskini na usongo mkubwa wa Mawazo.

Bushmamy Hawa watu wanaishi wapi?
 
Mchakato wa kiserikali ni mzuri Ila unachukua muda mrefu.Jamii yenyewe kuanzia mtaa husika ianze na hili.
Sawasawa. Naomba kuuliza hivi TASAF tukiacha na kuimpower poor families economically je inawafikia watu wenye matatizo kama hawa? Au kuna haja ya kutanua majukumu yake na kuanzisha hili la kulea wazee kwakuanzisha facilities maalumu kila mkoa zitakazozokusanya vikongwe watakaothibitika familia zao hazina uwezo?
 
Sawasawa. Naomba kuuliza hivi TASAF tukiacha na kuimpower poor families economically je inawafikia watu wenye matatizo kama hawa? Au kuna haja ya kutanua majukumu yake na kuanzisha hili la kulea wazee kwakuanzisha facilities maalumu kila mkoa zitakazozokusanya vikongwe watakaothibitika familia zao hazina uwezo?
TASAF hii phase 5 inawafikia wenye uhitaji kama hawa kabisa.Sasa,hapo inategemea wepesi wa familia husika kuwa wawazi,majirani kulisemea hilo na uongozi wa kitongoji,Kijiji,mtaa au eneo husika kuibua changamoto hiyo hadi ngazi ya halmashauri husika.Pamoja na mambo mengi wanayotuhabarisha watu wetu wa media,ni vema sana na mambo haya wakatupatia.Wakati ni sasa!
 
Ni Binti mdogo mwenye umri wa miaka 23,na mwenye mtoto mmoja Familia hii haina Baba kwani baba yao alishafariki Miaka mingi iliyopita na kijana aliyempa mimba binti alimtelekeza tangu mtoto akiwa ana miezi 6.

Mama wa huyu binti ana umri wa miaka 63 alikuwa mzima kabisa tangu kuzaliwa huku akifanya vibarua vya hapa na pale lakini miaka sita iliyopita ghafla alipata tatizo hili la kupooza viungo vya mwili, ulimi kuwa mzito na hivyo kushindwa kuongea vizuri, pamoja na kuzimia mara kadhaa kila wiki tatizo linalooendelea hadi sasa.

Kutokana na uwezo duni wa hii familia walishindwa kumpeleka Hospital kubwa kwa uchunguzi zaidi

Binti huyu amepangisha chumba kimoja kidogo akiwa yeye, mtoto wake wa kiume na mama yake huyo huku pembeni kukiwa na Ndoo yenye mfuniko wake ambae mama huyo hutumia kama choo usiku na mchana.

Alfajiri binti hujihimu kuandaa chai kwa ajili ya mama na mtoto wake ambae nae huenda shule na kumfungia mama yake ndani huku ufunguo akiacha kwa jirani hadi mwanae huyo ambae yuko la kwanza atakaporudi mchana na kumpa bibi yake chakula kilichopikwa usiku wa jana yake kwa ajili ya mlo wa mchana, hapo watajifungia ndani wote hadi binti atakaporudi saa moja usiku toka kibaruani.

Mara kadhaa bibi huyo amekuwa akizimia humo ndani na mjukuu huyo humwacha hivyo hivyo hadi fahamu zitakaporejea. Binti hiyo nilipata nafasi ya kumuuliza anagunduaje kama mama yake alizimia mchana na kunijibu kuwa hugundua hilo kutokana na kinyesi kutapakaa kitandani au chini au majeraha atakayomkuta nayo pindi arudipo jioni..

Kama kuna Umuhimu wa kuweka picha ya huyo Bibi mgonjwa basi ntaweka hapa.

Na hata kama kitapatikana wheelchair ♿ kwa ajili ya kumtoa nje wakati wa kuota jua pia itakuwa msaada mkubwa kwenye familia hii.

Wito wangu kwa Serikali iangalie Namna ya kusaidia aina hii ya wagonjwa kwani wapo wengi wanaopitia tabu na inatesa sana familia kwa kuwaletea umaskini na usongo mkubwa wa Mawazo.
Jaribu kuwassiliana na gazeti la mwananchi wataiweka vizuri hii habari na wasamalia wema watajitokeza kwa msaada
 
Bushmamy hii habari ni wewe ulienda kuwaona hiyo familia au umeikuta mahali?

Akipata kiti Cha kumtoa nje, nani atamwangalia wakati wa mchana mjukuu na Binti wanapokua hawapo nyumbani?

Hapa Kuna msaada unatakiwa ila Kuna vitu vingi vya kuangalia na kutafakari ili chochote kitakachofanyika kilete tija.

Inaumiza sana, na pia kutukumbusha kuwa na shukrani Kwa kile tunachokipata, Kuna watu wanapitia nyakati ngumu sana kwenye haya maisha.
 
Bushmamy hii habari ni wewe uluenda kuwaona hiyo familia au umeikuta mahali?

Akipata kitu Cha kumtoa nje, nani atamwangalia wakati wa mchana mjukuu na Binti wanapokya hawapo nyumbani?

Hapa Kuna msaada unatakiwa ila Kuna vitu vingi vya kuangalia na kutafakari ili chochote kitakachofanyika kilete tija.

Inaumiza sana, na pia kutukumbusha kuwa na shukrani Kwa kile tunachokipata, Kuna watu wanapitia nyakati ngumu sana kwenye haya maisha.
Nilienda kuiona Hiyo familia na matatizo ya huyo Binti yamenifanya niwe nae karibu kiasi fulani. Na ninatoaga kidogo kilichopo ndani ya uwezo wangu hata kama Mboga basi maisha yanaenda.
 
Back
Top Bottom