Infinite_Kiumeni
JF-Expert Member
- Jan 23, 2023
- 382
- 686
Asilimia kubwa ya wanaume hufikiri hivyo, hata mimi kuna kipindi nilikua naamini hivyo lakini sikupata matokeo ninayotaka. Japo vingine ni muhimu lakini ili kudumisha mahusiano, usivitegemee hivyo pekee.
Kama unaamini hivyo, na matokeo unayopata kwenye mahusiano yako hayakuridhishi, badilisha imani.
Anza na kujenga utu na tabia zitakazokusaidia kudumisha mahusiano hasa na mwanamke ambaye ana thamani unazozitaka. Usije kuishia kumvutia tu lakini ukashindwa kuwa naye kwenye mahusiano sababu ya imani hizi.
Ukiwa na hela
~ Nikipata hela tu, ntapata mwanamke wa kujenga naye maisha.
~ Nikipata hela tu, wanawake watakua wanavutiwa na mimi.
~ Nikipata hela tu, naanza kumfuatilia yule demu.
~ Nikipata hela tu, ndo namuoa huyu mwanamke.
~ Nikipata gari tu, wanawake hawachomoki.
Hela inachukuliwa kama ndio nguvu za kiume. Kwa kiwango fulani ni kweli ukiwa na hela au gari unaongeza thamani yako, lakini utu wako ndo wa muhimu katika kufurahia na kudumisha mapenzi na mwanamke unayetaka kujenga naye maisha.
Nilikua naamini hivyo, lakini nilipoanza kung’aa mtaani nilikua navutia wanawake wanaowaza kuhusu pesa zangu tu. Nilipogundua hilo nikaamua kubadilika ili kuwa na mwanamke ambaye unanijali mimi pia ukiachana na masuala kwamba nina hela.
Ukweli ni kwamba mwanamke kuvutiwa na wewe haihitaji kuwa na “hela” vile unavyohisi inabidi iwe. Kuvutiwa hakuchagui, inatokea tu.
Ni muhimu kuwa na hela ya kujikimu kimaisha, pia upendeze, lakini usiweke kuwa utapata upendo unaouhitaji sababu ya hela zako.
Ila jiwekee utapata upendo unaouhitaji kwa kuwa na tabia zinazovutia na kukusaidia kumtunza mwanawake mwenye hadhi unayoitaka. Usije kuishia kushangaa kwanini una hela lakini bado hupati mwanamke unayemtaka.
Ukimtimizia au ukimfurahisha mwanamke kila kitu/usimkasirishe mwanamke
Kujishusha na kutaka kumfurahisha mwanamke kila muda. Unaogopa kumkwaza ili asikuache, labda kuna mipaka unataka kuweka lakini kila ukitaka kuiweka, unaona utazua ugomvi unaamua kuacha.
Au unamtongoza mwanamke na unajitahidi kumfanyia kila kitu anachoomba ili upate penzi, au kutokuwa na maamuzi, leo unataka ule nini, unataka mkeo avaaje, kushindwa kuamua umpeleke wapi mkeo mkafurahi unaishia kumwambia chagua tu wewe ntakupeleka popote.
Vyote hivyo ni imani ambazo hazisaidiii kujenga mahusiano yanayodumu sababu mwanamke anakuona sio jasiri. La sivyo mtaishia kukaa ndani tu sababu jamii/kanisa/msikiti unajua nyie ni wapenzi lakini hamfanyi vitu wafanyavyo wapenzi.
Ukiwa rafiki yake kwa muda mrefu
~ Huu ndio ushauri tunaopewa na wazee wetu.
~ Huu ndo ushauri tunao uona kwenye muvi.
~ Huu ndo ushauri ambao mara nyingine akili zetu zinatuambia. Anza na urafiki usije ukakataliwa.
Inawezekana umetongoza wanawake kadhaa na wamekukatalia mpaka akili yako inakuambia “Saivi usitongoze, kuwa rafiki yake kwanza”. Usifanye hivyo. Na hata ukipata mpenzi kwa njia hiyo, mahusiano yenu yanakua hayana mapenzi sana (sexless).
Kwanini?
Sababu ili mwanamke akuone unafaa kimapenzi lazima alijue hilo tangu mwanzo. Bila kuogopa kukataliwa (we sio wa kwanza kukataliwa), na akiwa na wewe ajue kwamba kuna uwezekano wa kufanya mapenzi muda wowote na mambo mengi wafanyayo wapenzi.
Hata kama alikua anakutaka kimapenzi, ukijiweka kirafiki ndo basi tena. Hauhitaji kuwa rafiki yake kwanza ili baadaye uwe mpenzi wake ila nenda naye taratibu.
Sasa kwanini bado tunapewa imani hizo kila kona? Sababu wengi hawajui njia nzuri ya kumvutia na kumtunza mwanamke kimapenzi. Hivyo ni muhimu kuhakikisha unapata ushauri kutoka sehemu sahihi au kwa mtu ambaye unaona ana furaha kwenye mahusiano yake au kwa mtu ambaye ungependa kuwa na mahusiano kama ya kwake. Sio kwa kila mtu.
Jiulize kwanza, je, ningependa niwe na mahusiano kama ya huyu mtu anayenishauri? Kama ndio chukua kama hapana usichukue ushauri.
Kama unaamini hivyo, na matokeo unayopata kwenye mahusiano yako hayakuridhishi, badilisha imani.
Anza na kujenga utu na tabia zitakazokusaidia kudumisha mahusiano hasa na mwanamke ambaye ana thamani unazozitaka. Usije kuishia kumvutia tu lakini ukashindwa kuwa naye kwenye mahusiano sababu ya imani hizi.
Ukiwa na hela
~ Nikipata hela tu, ntapata mwanamke wa kujenga naye maisha.
~ Nikipata hela tu, wanawake watakua wanavutiwa na mimi.
~ Nikipata hela tu, naanza kumfuatilia yule demu.
~ Nikipata hela tu, ndo namuoa huyu mwanamke.
~ Nikipata gari tu, wanawake hawachomoki.
Hela inachukuliwa kama ndio nguvu za kiume. Kwa kiwango fulani ni kweli ukiwa na hela au gari unaongeza thamani yako, lakini utu wako ndo wa muhimu katika kufurahia na kudumisha mapenzi na mwanamke unayetaka kujenga naye maisha.
Nilikua naamini hivyo, lakini nilipoanza kung’aa mtaani nilikua navutia wanawake wanaowaza kuhusu pesa zangu tu. Nilipogundua hilo nikaamua kubadilika ili kuwa na mwanamke ambaye unanijali mimi pia ukiachana na masuala kwamba nina hela.
Ukweli ni kwamba mwanamke kuvutiwa na wewe haihitaji kuwa na “hela” vile unavyohisi inabidi iwe. Kuvutiwa hakuchagui, inatokea tu.
Ni muhimu kuwa na hela ya kujikimu kimaisha, pia upendeze, lakini usiweke kuwa utapata upendo unaouhitaji sababu ya hela zako.
Ila jiwekee utapata upendo unaouhitaji kwa kuwa na tabia zinazovutia na kukusaidia kumtunza mwanawake mwenye hadhi unayoitaka. Usije kuishia kushangaa kwanini una hela lakini bado hupati mwanamke unayemtaka.
Ukimtimizia au ukimfurahisha mwanamke kila kitu/usimkasirishe mwanamke
Kujishusha na kutaka kumfurahisha mwanamke kila muda. Unaogopa kumkwaza ili asikuache, labda kuna mipaka unataka kuweka lakini kila ukitaka kuiweka, unaona utazua ugomvi unaamua kuacha.
Au unamtongoza mwanamke na unajitahidi kumfanyia kila kitu anachoomba ili upate penzi, au kutokuwa na maamuzi, leo unataka ule nini, unataka mkeo avaaje, kushindwa kuamua umpeleke wapi mkeo mkafurahi unaishia kumwambia chagua tu wewe ntakupeleka popote.
Vyote hivyo ni imani ambazo hazisaidiii kujenga mahusiano yanayodumu sababu mwanamke anakuona sio jasiri. La sivyo mtaishia kukaa ndani tu sababu jamii/kanisa/msikiti unajua nyie ni wapenzi lakini hamfanyi vitu wafanyavyo wapenzi.
Ukiwa rafiki yake kwa muda mrefu
~ Huu ndio ushauri tunaopewa na wazee wetu.
~ Huu ndo ushauri tunao uona kwenye muvi.
~ Huu ndo ushauri ambao mara nyingine akili zetu zinatuambia. Anza na urafiki usije ukakataliwa.
Inawezekana umetongoza wanawake kadhaa na wamekukatalia mpaka akili yako inakuambia “Saivi usitongoze, kuwa rafiki yake kwanza”. Usifanye hivyo. Na hata ukipata mpenzi kwa njia hiyo, mahusiano yenu yanakua hayana mapenzi sana (sexless).
Kwanini?
Sababu ili mwanamke akuone unafaa kimapenzi lazima alijue hilo tangu mwanzo. Bila kuogopa kukataliwa (we sio wa kwanza kukataliwa), na akiwa na wewe ajue kwamba kuna uwezekano wa kufanya mapenzi muda wowote na mambo mengi wafanyayo wapenzi.
Hata kama alikua anakutaka kimapenzi, ukijiweka kirafiki ndo basi tena. Hauhitaji kuwa rafiki yake kwanza ili baadaye uwe mpenzi wake ila nenda naye taratibu.
Sasa kwanini bado tunapewa imani hizo kila kona? Sababu wengi hawajui njia nzuri ya kumvutia na kumtunza mwanamke kimapenzi. Hivyo ni muhimu kuhakikisha unapata ushauri kutoka sehemu sahihi au kwa mtu ambaye unaona ana furaha kwenye mahusiano yake au kwa mtu ambaye ungependa kuwa na mahusiano kama ya kwake. Sio kwa kila mtu.
Jiulize kwanza, je, ningependa niwe na mahusiano kama ya huyu mtu anayenishauri? Kama ndio chukua kama hapana usichukue ushauri.