. Pamoja na yote hayo mke wangu anatambua kuwa ni wajibu wake kufanya kazi za nyumani, namimi ni wajibu wangu kutafuta chakula na mahitaji muhimu kwa ajili ya familia yangu japo mke wangu hunisaidia pia katika hayo pale ninapokwama kifedha.
Mke wangu ni Mwalimu. Pamoja na kuwa housegirl.
Hapa ndo mimi nashangaa.
Umesema wewe hufanya kazi za nyumbani.
Lakini kumbe pia mkeo ni mwajiriwa.
Sasa unaposema anajua ni jukumu lake kufanya kazi za nyumbani na unajua jukumu lako la kuleta mkate, wakati wote wawili mnafanya vyote, SIELEWI.
Ni kwamba ndani yako bado kuna conflict, unataka kujulikana kama the main breadwinner wakati wote wawili ni maBread winner.
Wengine hujipa moyo kwa kusema "ananisadia nikikwama" wakati inajulikana kabisa kila budget wote mnachangia.
au hela zake zinafanya nini kama si kuhudumia watu wake ?
Hili ndo tatizo la kisaikolojia walilonalo wanaume wengi huku.
Ndomana hata mwanamke akitengeneza pesa nyingi kuliko mwanaume, mwanaume atatafuta njia za ajabu kuboost ego, ikiwemo kutomsaidia HATA kipindi anahitaji msaada.
Kuna thread mmama alianzisha, mume wake kapoteza kazi basi mke akirudi jioni mume hajafanya kitu, ni tv tu, hata mtoto akilia, mke anatolewa jikoni ambembeleze!!
Imefika muda mkubali tu dunia imebadilika.
Kama mkeo sio housewife, ukubali wote wawili ni mabreadwinner na wote mna jukumu la kutunza nyumba. Wala uanaume wako haupungui.
Uanaume wako utajihidhirisha in everyday life. Akitokea nyoka utaitwa. Zisikisikika kelele usiku utatoka peke yako. Ndege wakisogeza dish utapanda kutengeneza. Mtaongoza misiba. Men are physically stronger and more daring no? Lol