Ilitokeaje mpaka makanisa yanaruhusu unywaji pombe wakati inaleta majaribu ya kutenda dhambi zaidi na kukusogeza karibu na ulevi?

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,081
Habari zenu ndugu zangu, naombeni ufafanuzi

Mungu alishakataza pombe agano la kale na hata Yesu katika ile sala ya baba yetu ulie mbinguni kuna sehemu ya kuomba tuepushwe na majaribu ili tuepuke uovu.

Sasa inakuwaje tena kwamba hii pombe inabidi tuwe wanywaji na sio walevi?

Pombe ni dawa ya kulevya iliyohalalishwa kisheria kama ilivyo sigara. dawa zingine za kulevya ni bangi, mirungi, cocaine, n.k. zote hizi zinatumika kumlewesha mtu kwa namna tofauti. Pombe ni depressant drug, Bangi ni stimulant drug, cocaine ni hallucination drug, n.k. tena pombe ni hatari zaidi kuzidi hata bangi, huko makazini wapo wavuta bangi wanastua kabla ya kazi ila wanapiga kazi na ni ngumu hata kugudua, lakini kwa wale wanaokunywa pombe wanagundulika kirahisi kwa matendo na hata harufu kinywani, mlevi wa pombe kufukuzwa kazini ishazoeleka.

Hivi jamani kunywa pombe tu sio majaribu hayo? Maana ukinywa unapata karaha kenye majaribu ya kutaka kuendelea, pia akili inakuwa imeshuka uwezo wa kufanya maamuzi tofauti na ukiwa hujanywa, pombe nyingine hata ukinywa bila hata kulewa zinaanza kukupa ashki ya kufanya ngono.

Walevi nao huwa wanaanza kwa unywaji wa glasi moja tu tena unakuta ni mara 1 kwa mwezi, ila ikianza kumkolea hata hicho kiglasi hakina kazi tena inabidi aanze kupiga chupa mbili hivi na mazoea huanza kujengeka ya kunywa karibu kila baada ya siku kadhaa, hapo ni mnywaji tu, akianza ulevi pombe inakuwa kama dozi ni kila siku ama mara tatu kwa kutwa kama dawa.

Hata wale walevi wa bangi, unga, sigara, kamali, uzinzi, huwa mwanzoni wanaonja kidogo tu lakini ile raha ikianza kuwakolea ni majaribu tosha, wanajikuta tayari kwenye dimbwi zito kuchomoka inakuwa taabu. Hawezi kuvuka hata siku 2 ama 3 bila kustua.

Sasa inakuwaje kwamba tunaomba tuepushwe na majaribu huku tunajiweka kwa majaribu?

Hadi sasa ni wasabato pekee ndio nimekutana nao wao sheria zao zinapiga marufuku hata kuonja tone.
 
Nasubiria wafike🐒

images (74).jpeg
 
Una andiko ambalo MUNGU kakataza pombe?

Kilichokataliwa ni Ulevi na sio pombe.
Kula hakujakatiliwa , ila Ulafi ndio umekataliwa
Chakula na Pombe ni vitu viwili tofauti kabisa.

Huwezi mlinganisha mtu alielewa na mtu alievimbiwa, mtu alielewa hufanya vitendo vya kujishusha heshima, kutukana hovyo, kuvua nguo, kujikojolea, kujiny*a, kubaka, kuwa mgomvi, n.k.

Hata mtu aliekula kawaida na yule aliekunywa pombe ni vitu viwili tofauti, aliekunywa hutokwa na harufu mbaya mdomoni, uwezo wake kiakili unakuwa umeshuka kuliko skiwa kawaida, pombe inakuwa imeanza kumshuka kunako, yupo kwenye majaribu ya kulewa maana akili yake imeshuka maamuzi, n.k.
 
Kunywa kidogo usilewe,tumia mvinyo kidogo kwaqjili ya tumbo lako,mpe masikini kileo asahau shida zake,

Kwenye mvinyo ndio kuna ukweli,acha ulevi kunywa kuchangamsha akili utalijenge taifa.

Pia kumbuka viwanda vya pombe ndio vinalipa kodi kwa kiwango kikubwa kuliko hata hizo dini ambazo kila siku zinalilia kupata msamaha wa kodi.
 
Habari zenu ndugu zangu naombeni ufafanuzi

Mungu alishakataza pombe agano la kale na hata Yesu katika ile sala ya baba yetu ulie mbinguni kuna sehemu ya kuomba tuepushwe na majaribu ili tuepuke uovu.

Sasa inakuwaje tena kwamba hii pombe inabidi tuwe wanywaji na sio walevi ?

hivi jamani kunywa pombe tu sio majaribu hayo ? Maana ukinywa unapata karaha kenye majaribu ya kutaka kuendelea, pia akili inakuwa imeshuka uwezo wa kufanya maamuzi tofauti na ukiwa hujanywa, pombe nyingine hata ukinywa bila hata kulewa zinaanza kukupa ashki ya kufanya ngono.

Walevi nao huwa wanaanza kwa unywaji wa glasi moja tu tena unakuta ni mara 1 kwa mwezi, ila ikianza kumkolea hata hicho kiglasi hakina kazi tena inabidi aanze kupiga chupa mbili hivi na mazoea huanza kujengeka ya kunywa karibu kila baada ya siku kadhaa, hapo ni mnywaji tu, akianza ulevi pombe inakuwa kama dozi ni kila siku ama mara tatu kwa kutwa kama dawa.

Hata wale walevi wa bangi, unga, sigara, kamali, uzinzi, huwa mwanzoni wanaonja kidogo tu lakini ile raha ikianza kuwakolea ni majaribu tosha, wanajikuta tayari kwenye dimbwi zito kuchomoka inakuwa taabu. Hawezi kuvuka hata siku 2 ama 3 bila kustua.

Sasa inakuwaje kwamba tunaomba tuepushwe na majaribu huku tunajiweka kwa majaribu ???

Hadi sasa ni wasabato pekee ndio nimekutana nao wao sheria zao zinapiga marufuku hata kuonja tone.
RC siyo kanisa ni secret society tu kama freemasons. that is why wanaruhusu vitu vyote vibaya
wana mission ya kutawala watu na kunyonya pia
walikuwa ma agent wa wazungu kututawala
 
Sio wasabato pekee ndiyo hawanywi wala kugusa pombe, wapentekoste ndio namba moja kutokunywa na kugusa pombe. Ukinywa utatengwa au kufukuzwa ushirika. Kuna kanisa moja kubwa duniani padri wake alipomaliza misa akaenda klabuni tena klabu cha pombe za kienyeji kijijini. Alipomaliza kunywa kiasi chake akawasha kiko akabugia mdomoni kisha akawasha gari kurudi parokiani.
 
Sio wasabato pekee ndiyo hawanywi wala kugusa pombe, wapentekoste ndio namba moja kutokunywa na kugusa pombe. Ukinywa utatengwa au kufukuzwa ushirika. Kuna kanisa moja kubwa duniani padri wake alipomaliza misa akaenda klabuni tena klabu cha pombe za kienyeji kijijini. Alipomaliza kunywa kiasi chake akawasha kiko akabugia mdomoni kisha akawasha gari kurudi parokiani.
Ikawaje?
 
Pia kumbuka viwanda vya pombe ndio vinalipa kodi kwa kiwango kikubwa kuliko hata hizo dini ambazo kila siku zinalilia kupata msamaha wa kodi.
Ni vilevi ndivyo hushikilia rekodi kubwa ya kuchangia kodi, hapo zamani sigara zilikuwa zinalipa zaidi.

Leo hii hata wakiruhusu vilevi vya ziada kama bangi na mirungi vitachangia zaidi.

Vilevi ni chanzo kikuu cha mapato kwasababu hata kodi ikiongezwa watu wananunua tu maana kuacha ulevi si shughuli ndogo (inelastic demand).

Na ndio maana hata kwenye uhalifu ni wauza madawa ya kulevya ndio wanakinga pesa zaidi.. kina Pablo, El Chapo, n.k.

Kuingia rahisi kutoka ni kitu kingine hicho
 
RC siyo kanisa ni secret society tu kama freemasons. that is why wanaruhusu vitu vyote vibaya
wana mission ya kutawala watu na kunyonya pia
walikuwa ma agent wa wazungu kututawala
Acha uongo na uzushi Bwashee! Roman Catholic Church ni Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume. Kanisa ambalo waumini wake wengi hawajutii kuwemo humo. Pombe tunakunywa kwa kipimo!

Binafsi huniambii kitu kuhusu Roman Catholic church. Tumsifu Yesu Kristu.....🙏
 
Acha uongo na uzushi Bwashee! Roman Catholic Church ni Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume. Kanisa ambalo waumini wake wengi hawajutii kuwemo humo. Pombe tunakunywa kwa kipimo!

Binafsi huniambii kitu kuhusu Roman Catholic church. Tumsifu Yesu Kristu.....🙏
Kwa kipimo kivipi wakati ni Pombe hio hio ilishakatazwa na Mungu mwenyewe.

Maneno ya baadhi ya watu kisa wamo kwenye biblia hayamuwakilishi Mungu, mtu kama Paulo kuwahamasisha watu wanywe pombe hio ilikuwa ni yeye kama yeye kwa mawazo yake, haina uhusiano wowote na Mungu.

Hio pombe inapunguza uwezo wa kiakili tofauti na mtu akiwa hajanywa, pombe inaleta ashki ya kuzini, walevi huanza kama wanywaji na hata mnywaji atalewa ili ajue kipimo chake.
 
Una andiko ambalo MUNGU kakataza pombe?

Kilichokataliwa ni Ulevi na sio pombe.
Kula hakujakatiliwa , ila Ulafi ndio umekataliwa
Mantiki ya kijinga hasa.Unakunywa pombe ili iwe nini?Kwa sababu unakunywa dawa ili upone.Dhumuni hasa la kunywa pombe ni nini?
Hata chakula unakula ili ushibe ndio sababu huli tonge moja ukaacha.
Sawa na uvute sigara halafu useme sija inhale!Sasa dhumuni la kuvuta hiyo sigara ni nini?
 
Kwa kipimo kivipi wakati ni Pombe hio hio ilishakatazwa na Mungu mwenyewe kwenye mistari kibao ya biblia.

Hio pombe inapunguza uwezo wa kiakili tofauti na mtu akiwa hajanywa, pombe inaleta ashki ya kuzini, walevi huanza kama wanywaji na hata mnywaji atalewa ili ajue kipimo chake.
Wengine tunakunywa pombe mara moja moja ili kupunguza mawazo ya marejesho, na ada za watoto mkurugenzi! Huko kwingine sisi hatumo!
 
Chakula na Pombe ni vitu viwili tofauti kabisa.

Huwezi mlinganisha mtu alielewa na mtu alievimbiwa, mtu alielewa hufanya vitendo vya kujishusha heshima, kutukana hovyo, kuvua nguo, kujikojolea, kujiny*a, kubaka, kuwa mgomvi, n.k.

Hata mtu aliekula kawaida na yule aliekunywa pombe ni vitu viwili tofauti, aliekunywa hutokwa na harufu mbaya mdomoni, uwezo wake kiakili unakuwa umeshuka kuliko skiwa kawaida, pombe inakuwa imeanza kumshuka kunako, yupo kwenye majaribu ya kulewa maana akili yake imeshuka maamuzi, n.k.

Acha maneno mengi.

Njoo na andiko la biblia , linalopinga Pombe.
Mimi nina maandiko yanayopinga ulevi tu .

Au wewe , unatokea upande ule wa wanafiki , wanaokata pombe na kusema mbinguni kuna mito ya pombe
 
Back
Top Bottom