Kama tunamuomba Mungu atuepushe na majaribu ni kwanini aliruhusu unywaji wa pombe ambao umefanya wengi kuwa walevi?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
bottles-and-glasses-of-alcohol-drinks.jpg


Wasabato mkae pembeni hili haliwahusu

Sijawahi kuelewa hata kidog haya mambo ya unywaji na ulevi, huwa naonaga ni kama tiketi tu ya kuhalalisha ulevi.

Kama ni mlevi ama uliwahi kuwa mlevi wa sigara, bangi, pombe, ngono zembe, kamali, n.k. basi unajua fika kwamba siku ya kwanza huwa ni kujaribu kidogo tu lakini ukianza kadri siku zinavyoenda kukumbuka ile raha yake unajikuta tayari umeingia kwenye shimo la ulevi.

Sasa nachojiuliza ni kwamba, katika sala ile ya Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, kuna kipengere tunamuomba Mungu pia atuepushe na majaribu... ni vipi aliweza kuruhusu unywaji wakati ni wanzo wa kuwa mlevi ?
 
Mathayo 6:9-13

Basi ninyi salini hivi;
Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe,
hapa duniani kama huko mbinguni.
Utupe leo riziki yetu. Utusamehe deni zetu,
kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu.
 
Ulevi siku zote huwa unaanza kwa kutumia kipimo kidogo tu

Mlevi wa bangi huwa anaanza na pafu mbili, mwishowe ni msokoto mzima kila asubuhi na usiku

Mlevi wa kamari huwa anaanza kwa kuweka pesa ndogo, mweishowe anatumia haya sehemu kubwa ya kipato chake

Mlevi wa madawa nae huwa anatumia kidogo tu ila mwishowe gari inakolea
 
Back
Top Bottom