ITEGAMATWI
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 5,310
- 4,040
Wadau huwa najiuliza kila siku bila kupata jawabu!Hv ilikuwaje Portugal ikaitwa Ureno kwa kiswahili jina ambalo haliendani hata kidogo na jinsi wao wenyewe wanavyoiita nchi yao? Nimekuwa nikiangalia mfano wa nchi nyingine zinavoitwa kwa Kiingereza au wao wenyewe nimeona kwa kiasi fulani majina yanashabihiana na sisi tunavyoyaita;Mfano:- England - Uingereza. America - Marekani. Spain - Uhispania. Egypt -(Masr) wenyewe wanavyoiita!Misri kwa kiswahili! etc Hebu naomba mnisaidie wadau hii ilikuwaje? Nawasilisha!!!