Ilikuwa mwaka 1981

Na umeliweka kwenye wanga... mgongoni kuna malinda ya mraba, na mabegani pia....

Kuna wakati BLUEE ILIKUWA INAHUSIKA
Usisahau na Buibui!! Ila sisi wa mjini tulikuwa tunatumia karatasi flani hivi za kupasia!! Basi unakuta ina picha ya kijimaua,unanyunyiza maji kidogo kwenye shati Kisha unabandikia kipicha chako na kukipasi!! Oow! Those good old days!
 
Dah... Ulisalimika na kichapo siku hiyo??
Ilibidi nirudi home mbio huku nikiwa nahema kwanguvu, nilipo ulizwa tatizo, nikasema nimeijia tochi nikatafute pesa imeanguka. Tena nikajifanya nina haraka isije tokea mpintanjia akaiokota....

Ndipo mama akanipa pesa nyingine na akasema sio rahisi kuipata pesa ilio anguka usiku ule....
 
Mm unitoe nilikuwa na miaka saba!!
Ahaa! Wewe ndiyo ulikuwa unanipiga makwenzi nikinyoa kipara eh? Halafu nikivaa safari buti zangu unanifanyia Wow wow kama mbwa! Nimeshakujua!! Sasa hivi mi msoja,njoo tena!
 
Pale tabora tulikuwa na KAUTA, wengine walikuwa na Kagera Retco, Kauma, Shinyanga Retco, Kaudo, Mbeya Retco, sijui nchi hii tulijikwaa wapi tu
Arusha-Moshi nilipanda kilimanjaro bus service! Nauli sh 75
 
Shikamoo mzee!
 
Hapana mwaka huo hao walikuwa hawajaja. Alikuwapo mtu anaitwa Belesa Kakere. Hao walikuja kunako 1984

Mkuu Belesa Kakere wakati huo yuko na Marehemu Marijani Rajab namkumbuka kwenye kipande hiki cha wimbo nadhani unajua,
"Shangazi yakooo nae kakusihi sanaaaaaa, uje kumuona mama Magreti ukapuuza ". Aaah acha tu nyimbo zilikuwa zamani siku hizi kelele tu Mkuu!
 


Hiyo ilikuwa DAR INTERNATIONAL wana SUPER BOMBOKA na sio BIMA LEE. Hapo walikuwa pia na Cosmas na Fresh Jumbe...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…