Maboso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 5,164
- 5,761
Nikiri wazi sikuwa nimeisoma ilani ya Chadema hasa baada ya kuona mgombea wao hana mwelekeo mnzuri na kuisadia nchi hii. Leo baada ya kumsikia ndugu Polepole nilishtushwa na kipengere kinachohusu madini wakati anafanya mrejeo wa ilani ya Chadema. Baada ya kuitafuta hiyo ilani na kukisoma hicho kipengere, nimejikuta napatwa na ukakasi kujua kama kweli Chadema wana nia nzuri na nchi yetu. Nisiwe msemaji sana, naomba wadau tusome hiki kipengele halafu sote tutoe michango ya mitazamo yetu kama kitakuwa na manufaa kwa nchi au hakitakuwa na manufaa. Nimeaattach ilani yote (.pdf) kwa wale ambao watapenda kuipitia waone manzuri na mapungufu yake.
12.1 Nishati
Chadema inatambua kwamba nishati ni nguzo muhimu katika kuboresha maisha ya watanzania na ujenzi wa taifa kiuchumi.
Kumekuwa na changamoto kubwa ya kupata nishati ambayo inaendana na ulinzi wa mazingira kutokana na chanzo kikuu cha nishati inayotumika nchini ni mkaa na ambao kwa kiasi kikubwa sio rafiki kwa mazingira.
Katika kukabiliana na changamoto hizi serikali ya Chadema itafanya yafuatayo;
a. Serikali ya Chadema itaingia ubia na sekta binafsi katika kuzalisha, kusafirisha na kusambaza nishati ya umeme nchini
b. Serikali ya Chadema itatumia madini kama dhamana katika kujenga miundombinu ya umeme nchini
12.2 Madini
Chadema inatambua kwamba raslimali za madini zilizopo Tanzania ni utajiri usioendelevu na urithi wa wote ndani ya vizazi vyote vya Tanzania.Hivyo hatuna budi kuitumia rasilimali hii kwa uangalifu ili vizazi vijavyo viweze kunufaika na rasilimali hii hata kama itakuwa imeshaisha.
Hivyo basi ili kuhakikisha kuwa madini yananufaisha kizazi cha sasa na kijacho , Serikali ya Chadema itachukua hatua zifuatazao;
12.1 Nishati
Chadema inatambua kwamba nishati ni nguzo muhimu katika kuboresha maisha ya watanzania na ujenzi wa taifa kiuchumi.
Kumekuwa na changamoto kubwa ya kupata nishati ambayo inaendana na ulinzi wa mazingira kutokana na chanzo kikuu cha nishati inayotumika nchini ni mkaa na ambao kwa kiasi kikubwa sio rafiki kwa mazingira.
Katika kukabiliana na changamoto hizi serikali ya Chadema itafanya yafuatayo;
a. Serikali ya Chadema itaingia ubia na sekta binafsi katika kuzalisha, kusafirisha na kusambaza nishati ya umeme nchini
b. Serikali ya Chadema itatumia madini kama dhamana katika kujenga miundombinu ya umeme nchini
12.2 Madini
Chadema inatambua kwamba raslimali za madini zilizopo Tanzania ni utajiri usioendelevu na urithi wa wote ndani ya vizazi vyote vya Tanzania.Hivyo hatuna budi kuitumia rasilimali hii kwa uangalifu ili vizazi vijavyo viweze kunufaika na rasilimali hii hata kama itakuwa imeshaisha.
Hivyo basi ili kuhakikisha kuwa madini yananufaisha kizazi cha sasa na kijacho , Serikali ya Chadema itachukua hatua zifuatazao;
- Kuhakikisha madini yanatumika kama dhamana ya mtaji kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali kama vile maji, barabara,reli na nishati
- Uvunaji wa madini utakuwa maalumu kwa ajili ya mitaji ya; Nishati, hasa umeme na maji, Ujenzi wa viwanda , kujenga na kuboresha miundombinu ya uchukuzi
- Serikali ya Chadema itaweka utaratibu wa ubia katika uchimbaji wa madini baina ya raia na wageni kwa ajili ya kuwawezesha watanzania ambao mitaji na teknolojia yao sio kubwa kuweza kunufaika kutokana na ubia na Makampuni ambayo yataingiza mitaji mikubwa na teknolojia ya kisasa katika uchimbaji wa Madini
- Serikali ya Chadema itaweka utaratibu wa kisheria juu ya misamaha ya kodi katika sekta hii ili kulipunguzia taifa hasara itokanayo na baadhi ya misamaha kwenye sekta hii
- Serikali ya Chadema kwa kushirikiana na sekta binafsi itaboresha sekta ya madini na kuwezesha wachimbaji wadogo kushiriki na kumiliki uchumi wa madini
- Serikali ya Chadema itapitia na kuboresha sheria za madini zilizopo ili ziendane na viwango vya kimataifa ili taifa liweze kunufaika na madini bila kuathiri uwekezaji