WanaJF
Wakati nchi nzima ikizizima na kumuunga mkono mgombea Urais wa Chadema Tundu Lissu kutokana na kauli Mbiu ya Uhuru,Haki na Maendeleo ya watu tayari Ilani ya uchaguzi ya Chama hicho imekuwa gumzo kila mahali.
-----------------------------------
BAADHI YA TOFAUTI YA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM NA CHADEMA MWAKA 2020
1.Ilani ya CCM haizungumzii kupunguza Kodi wakati ilani ya CDM inalenga kupunguza Kodi ya ongezeko la thamani ili iendane na nchi jirani na kuondoa utitiri wa kodi (multiple taxation)
2. Ilani ya CCM haizungumzii kuongeza mishahara wala kufidia nyongeza ambazo watumishi walipunjwa miaka mitano iliyopita wakati CDM inategemea kuleta bajeti za ziada kufidia nyongeza mishahara ya miaka mitano ambayo watumishi hawakupata nyongeza ya mishahara wala kupanda madaraja.
3. Ilani CCM haizungumzii kupunguza marejesho ya mikopo ya elimu ya juu(HELSB) wakati CDM inategemea kuweka marejesho ya asulimia 3 kwa wahitimu wa vyuo vikuu badala ya asilimia 15 ya Sasa ambayo iliongezwa kinyume na mkataba wa mkopo kwa kufanya marekebisho ya sheria ya Sasa na kwamba mhitimu alipe baada ya kupata kazi.
4.Ilani ya CCM haizungumzii agenda ya Katiba Mpya wakati ile ya CDM inazungumzia kurudisha mchakato wa katiba mpya ulioasisiwa na jaji Warioba ndani ya siku mia za Kwanza.
5. CCM inaamini kwenye maendeleo ya vitu wakati CDM inaamini katika maendeleo ya watu zaidi. Yaani maisha yawatu ndio yawe bora zaidi badala ya vitu Kama ndege.
6. Ilani ya CCM haizungumzii kulinda uhuru wa habari Kama kipau mbele wakati ilani ya CDM inaweka kipaumbele mojawapo ni kurejesha Uhuru wa habari.
7. Ilani ya CCM haizungumzii kugatua madaraka na kufanya wananchi wawe na nguvu zaidi ya kuamua mambo yao wakati ilani ya CDM inapendekeza kupeleka nguvu zaidi kwa wananchi.
8. Ilani ya CCM haitoi mkazo wa uchumi kumilikiwa na sekta binafsi( wananchi) bali serikali wakati ilani ya CDM inaweka kipaumbele uchumi wa watu( sekta binafsi)
9. Ilani ya CCM haizungumzii bima ya afya kwa watu wote wakati ilani ya CDM inataka watu wote wawe na bima ya afya.
10. Ilani ya CCM inazungumzia kudumisha Muungano was serikali mbili wakati Ilani ya CDM inazungumzia Muungano wa serikali tatu zilizopendekezwa na wananchi kwenye tume ya Jaji Warioba.
11. Ilani ya CCM haizungumzii kuondoa Kodi kwenye maduka ya majeshi ya Polisi, jeshi la wananchi, magereza na Zimamoto Kama hapo awali ili kuwapa wanajeshi unafuu wa maisha wakati CDM inapendekeza kurejesha unafuu huo.
12. Ilani ya CCM haizungumzii marudhiano ya kitaifa wakati ilani ya CDM inapendekeza kuleta maridhiano ya kitaifa ndani ya siku mia za Kwanza.
13. Ilani ya CCM haizungumzii kufuta sheria kandamizi wakati ilani ya CDM inapendekeza kufuta sheria zote kandamizi.
---------------------------------------
Ifuatavyo ndiyo ILANI ya Chadema 2020 - 2025