IKULU: Kikwete si mmiliki DOWANS!

IKULU: Kikwete si mmiliki DOWANS!

NARUDIA KUSEMA KWA SAUTI KUU MMILIKI WA DOWANS NI JAKAYA MRISHO KIKWETE sababu yeye ndio final say ktk baraza la mawaziri waliopitisha mikataba LAGHAI DHIDI YA TAIFA.
 
Kama kweli Kikwete siyo mmiliki wa Dowans basi wamiliki wake ni maswahiba wake au ana mahusiano ya kimasilahi binafsi na wamiliki wake. Tunaomba serikali yake iwataje
 
NARUDIA KUSEMA KWA SAUTI KUU MMILIKI WA DOWANS NI JAKAYA MRISHO KIKWETE sababu yeye ndio final say ktk baraza la mawaziri waliopitisha mikataba LAGHAI DHIDI YA TAIFA.
 
Kikwete ndiyo mmiliki wa dowans kama alivyoainisha Dr wa Ukweli. Otherwise, aje public, na siyo hizi loudspeakers, atueleze kinagaubaga ni ya akina nani!!
 
Jamani mbona kila baya awe anasukuwa tu JK, tatizo ni nini hasa ndugu zetu?

Hii sasa inafika mahali mpaka inaudhi kweli. Ndiyo maana tangu sasa bora ikulu iwekiwaporomosheeni matusi ya nguoni hivyo ndiyo mkome na umbeambea wenu huo.

Kujishebedua huko siyo dawa mbona inakuuma ni kweli siyo? Halafu hiyo lugha yako ni lazima inafanana na sura yako
 
siamini kauri kama hizi kutokaikuru amaa kweri ukitakaubaya udai chako hatudanganyiki nawewekanawe uso usidanganyike
 
Sometimes I wonder wana-jf, the right path to straighten our course towards a corrupt free society is by using a corrupt mind in a disorganized way like the way we're doing now or by elimination of the corruptive sources from the base to the top. I like politics as means of leading people (good governance), yet I hate lies! Now, if Slaa is a lier may God forgive him, but if the state house is lying (God forbid) may the souls of those perpetrators rest in peace! Wake up call to you all, disregarding whether your a left winger or a modern rightist!
 
Mabaya yote yatakwenda kwake kwani kama angeliyachukulia hatua kwanza angeonekana ni jasiri, sasa yeye kila jambo ana cheka tu wala umakini haupo kwa swala la Taifa kama yeye ndio mkubwa wa nchi unafikili haya yataenda kwa nani????

Baba mwenye familia yake ikikosa adabu lawama zote zitakwenda kwake na sio kwa watoto kwani yeye ndio ameshindwa kukuza Familia kwa maadili.

Jamani mbona kila baya awe anasukuwa tu JK, tatizo ni nini hasa ndugu zetu?

Hii sasa inafika mahali mpaka inaudhi kweli. Ndiyo maana tangu sasa bora ikulu iwekiwaporomosheeni matusi ya nguoni hivyo ndiyo mkome na umbeambea wenu huo.
 
Kama kweli serikali inawafahamu wamiliki wa Dowans haitoshi tu kusema kuwa JK siyo mmiliki wa Dowans na kwamba Dr. Slaa ni mwongo.

Je kutuambia wamiliki wa Dowans kutaigharimu nini serikali? kuna siri gani katika kuwataja hao wamilki?

Dk. Slaa aishika pabaya Ikulu

• Yatumia maneno ya kejeli, mtaani kujibu hoja zake

na Edward Kinabo

KURUGENZI ya Mawasiliano Ikulu imeelezea kukerwa kwake na hatua ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kumtaja rais Jakaya Kikwete kuwa alihusika katika uzembe uliosababisha taifa kutakiwa kuilipa kampuni ya Dowans sh bilioni 185 kama fidia.

Taarifa kali ya Ikulu iliyobeba ujumbe wenye maneno ya kebehi na ya mitaani ya kumwita Dk. Slaa mtu ‘aliyechanganyikiwa’ na ‘mzabinazabina’ ilisainiwa na Salvatory Rweyemamu ambaye kabla ya kwenda Ikulu alikuwa mmoja wa wahariri watendaji aliyekuwa akiheshimika kwa kutumia lugha fasaha na ya staha.

Rweyemamu katika taarifa yake hiyo iliyoonyesha waziwazi kuandikwa na mtu mwenye hasira, chuki na dharau ama kwa Dk. Slaa, CHADEMA na Tanzania Daima alikwenda mbele na kumwita kiongozi huyo wa kisiasa kuwa ni mtu hatari.

Sehemu ya maneno makali ya Rweyemamu kwa Dk. Slaa ni kama yale aliyosema, “Na kama kweli Dk. Slaa ametoa kauli hii na kusema maneno ya namna hii basi sasa Watanzania wanayo kila sababu na haki ya kuamini kuliko wakati mwingine wowote kuwa mzee huyu (Slaa) sasa amechanganyikiwa na ni mtu wa hatari sana kwa utulivu wa nchi hii.”

Rweyemamu aliendelea kueleza, ”Kama Dk. Slaa anataka kweli kujua wamiliki wa Kampuni ya Dowans, basi atafute ukweli huo na aachane na tabia ya kutapatapa na uzabinazabina yenye lengo la kuwapaka watu watope.”

Ikulu ambayo katika mazingira ambayo si rahisi kuyaeleza imekuwa na desturi ya kukanusha kwa nguvu kubwa kila wakati jina la Rais Kikwete linapohusishwa na sakata la kashfa ya Richmond/Dowans.

Hii ni mara ya pili kwa Ikulu kufanya hivyo baada ya mara ya kwanza kuchukua hatua kama hiyo wakati Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, alipokanusha hoja zilizokuwa zikijaribu kumhusisha Rais Kikwete na uhusiano wake na mkataba wa Richmond.

Wakati Ikulu ikikanusha mara kwa mara kuhusishwa kwa Kikwete katika sakata la Richmond/Dowans kwa namna yoyote ile, upo ushahidi wa kibunge (rejea ripoti ya Kamati Teule ya Mwakyembe) unaoonyesha kwamba, maamuzi kuhusu mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura ulioipa ushindi Richmond ulijadiliwa na Baraza la Mawaziri lililokuwa chini ya uenyekiti wa rais mwenyewe.

Kama hiyo haitoshi, gazeti moja la kila wiki linalomilikiwa na kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambalo Rweyemamu amepata kuwa mmiliki wake, limepata kuchapisha katika ukurasa wake wa mbele barua ikionyesha barua aliyoandika aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kwenda kwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini kuhusu suala la Richmond ambayo nakala yake ilikwenda pia kwa Rais Kikwete.

Uamuzi wa jana wa Rweyemamu kuandika taarifa kali dhidi ya Dk. Slaa unakuja siku chache baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa migogoro ya kibiashara hivi karibuni kuamuru Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO) kuilipa Dowans fidia kubwa baada ya kuvunja mkataba nayo kinyume cha taratibu.

Katika mahojiano maalum na gazeti Tanzania Daima Jumapili, la juzi Dk. Slaa alikaririwa akisema chanzo cha suala zima lililopelekea Dowans kutakiwa kulipwa fidia hiyo ni uzembe wa serikali na Rais Kikwete mwenyewe kwani ndio waliohusika katika kuileta kampuni ya Richmond ambayo baada ya kuonekana ya kitapeli iliamua kurithisha kazi zake kwa Dowans.

Ikulu katika taarifa yake hiyo kwa sababu zisizojulikana ilijikuta ikipotoka ama kwa makusudi au kwa kutojua ilipoeleza kuwa gazeti la Tanzania Daima lililonukuu maelezo ya Dk. Slaa, linamilikiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakati taarifa zilizopo kwa msajili wa magazeti zinaeleza bayana kwamba, gazeti hilo ni la watu binafsi.

Ikipinga maelezo ya Dk. Slaa kuhusu uhusiano wa rais Kikwete na Dowans, taarifa hiyo ya Ikulu ilisema, “Huu ni uongo wa mchana, ni uzushi wa karne na propaganda ya hatari. Kwa hakika na kwa namna isiyoweza kuelezeka kwa ufasaha, tumeshtushwa sana na kauli hii ya Dk. Slaa

“Mheshimiwa Rais Kikwete siyo mmiliki wa Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya Dowans. Hakupata kuwa mmiliki, siyo mmiliki na wala hatakuwa, hata siku moja, mmiliki wa kampuni hii.” Ikitumia lugha kali dhidi yake Ikulu iliwataka wananchi wampuuze Dk. Slaa ikidai kuwa ni mzushi na amechanginyikiwa.

Hata hivyo, hii si mara ya kwanza kwa Dk.Slaa kuitwa mzushi na vigogo wa serikali kwani mara kwa mara anapoibua maovu amekuwa akipingwa kwa kuitwa jina hilo ingawa anayoibua huthibitika kuwa na ukweli ndani yake.

BARUA YA SALVA KWA VYOMBO VYA HABARI HII HAPA
As long as Kikwete/Ikulu doesn't want to tell the wananch who is the owner of Dowans, Dr. Slaa is right.
 
Hiyo wala si lugha kali kama watu wanavyotaka kusema. Lakini kama mtu angesoma ila Tz Daima between lines, hakuna sehem ambayo ilimuhusisha Kikwete kwamba ndiye mmliki zaidi ya Title.

Habari ilikuwa by implications na ile ilikuwa ni politics. Kwa bahati mbaya Ikulu nao wameingia na sasa watakuwa wanafanya kazi ya kukanusha. Wangekaa kimya na wakaishughulikia DOWANS kivingine wangepata heshma zaidi kuliko kuhangaika kukanusha.

Kiuhalisia Kikwete hawezi kuwa mmiliki ila by implications.

Chanzo cha matatizo ya umeme nchi hii ni Jakaya Mrisho Kikwete,ever since he signed the IPTL contract in 90's the umeme has never been stable and perfect in the country and yet again he and his fellow culprits bring in Richmond-Dowans deals,the guy knows what he is doing brother!
 
Siku Mkwere atakapovunja ukimya,na kutangaza kuwa ni shareholder wa Dowans, Salva Rweyemamu atasema alikuwa anatoa maoni yake binafsi kuhusu suala la Dowans lol. Kama Werema tu.... Hii ndo serikali ya Dr Kikwete. Ari zaidi,kasi zaidi,na nguzu zaidi katika ufisadi.
 
That's very obvious!! Unafikiri "puppet group" ya JK ingejibu vingine mbali na walivyojibu??? Cha muhimu huyo Salva ajue hakuna alichokifanya ku-counter check tamko la Dr. Slaa.
 
ha haha hahahahahahaha Kikwete; kamanda wa mafisadi. Huyu rwemamu anajifanya kuwa brela. atuambie na vingine anavyomiliki.
 
Halafu hii hasira inamfanya hata ashindwe kuandika waraka wa kiswahili vizuri.....Hakuna Kidhabidhabina ni kizabizabina...na hakuna stori ni Hadithi.Nimefuatilia matangazo mengi yanayoandikwa na Idara ya Mawasiliano Ikulu nimekugundua kuwa Idara hiyo haina watu makini,ni genge la Wahuni.Inapaswa watu hawa wawajibishwe.......huwezi kushindwa kuandika waraka mdogo kwa lugha fasaha inakuwaje mambo makubwa yanayohitaji uandishi makini?
 
salva ,mteteeeeeee we JK, ipo siku kila kitu kitakuwa MWAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
 
Dowans ni mwiba na ipo siku utamtoboa na kumsabibishia tende la mguu mtu anayefanya masihala na mambo yake.Ngoja tuone! Nachojua jana sio leo wala haitakuwa kesho.
 
Back
Top Bottom