IKULU: Kikwete si mmiliki DOWANS!

IKULU: Kikwete si mmiliki DOWANS!

Haya ni matokeo ya kuokota watu mitaani na kuwapa vyeo vikubwa serikalini bila kufanyiwa vetting na kutokuwa na uzoefu wa kufanya kazi za serikali.Ndiyo maana barua iliyoandikwa na ikulu inafanana na mashairi ya taarabu,tutalajie vitu vya ajabu zaidi.Ipo siku inakuja kutokea ikulu inajibu tuhuma zilizotolewa na wanasiasa kwa kusema wananchi achaneni nao hao msisikilize habari za kisen....Ndipo tunapoelekea.

ni kweli tangu ajuane na akina RA wakati wa Rai basi kaonekana mjuaji sana. Kwani kile cheo kinapatikanaje? Kuwa msemaji wa ikulu inapatikanaje kazi iyo?na analipwa na nani?au anateuliwa kishikaji na kiranja mkuu? Je mda wa kukaa pale kwa cheo icho ni muda gani? Nadhani kama muda wake wa kustaafu ukifika asiruhusiwe kupata mkataba mwingne wampe mtu mwenye kuiheshimu ikulu! Kama anapa mafao ya ikulu,hata kunywa chai ya ikulu,ujue kodi yetu inapotea bure. Ikulu ni mahala patakatifu bwn!
 
Kuna kamchezo kanaibuka JF. Watu badala ya kujadili hoja wanajadili maisha ya watu. Yeye kulelewa na nani, si msaada saana kwa maendeleo ya nchi. Tujadili content ya hoja alioyotoa na kuachana na mambo yasiyo na faida.
 
Ndugu wanaJF nimesikitishwa sana na kauli alizotoa msemaji wa ikulu,ndugu Salva Rweyemamu juu ya wanaohoji uhalali wa Dowans Tanzania Ltd,kama dr.Slaa! Salva amechanganyikiwa kwa kuitetea Ikulu kwa kutumia maneno ya kijijini kwao Ijumbi! Uzabinazabina na kuchanganyikiwa anakosema ndugu Salva ndo nini? Mwl.Nyerere alisema Ikulu ni mahali patakatifu! Nashangaa maneno haya yamegongwa muhuli wa Ikulu kumkejeli na kumdhalilisha Mtanzania mzalendo dr.Slaa. Serikali ilitenga sehemu inaitwa Mirembe pale Dodoma ili kuwaweka vichaa na waliochanyikiwa sasa Salva badala ya kumpeleka huko dr.Slaa yeye anakimbia kuwataarifu watanzania kuwa mzee wetu dr.Slaa ame'chizi'! Tukueleweje Salva? Ndugu wanaJF,Salva ndo chizi,tena chizi aswaa! Salva tangu ahitimu pale Rubya Seminari,amelelewa kwa karibu na babake mdogo mzee Francis Kadogo wa Nyamagoma kijijini Katare,Buganguzi karibu kwa Afande A.Tibagaina,ila Salva alipokuja mjini ameitelekeza familia yake,na Mzee Kadogo yupo ktk siku za mwisho wa maisha yake kwa ugumu wa maisha! Mzee Francis Kadogo analaani kitendo cha Salva kumtupa afe kwa dhiki! Mzee amepooza takribani miaka 10 hawezi kunyanyuka wala kutoka alikolala wakati Salva amehamia ikulu kula raha kama vile ni mtoto wa msoga,chalinze. Huyu naona amechanyikiwa zaidi ya mwenzake dr.Slaa aliyetueleza kodi yetu ilipo! Amesahau alikotoka na mola atamlipa! Salva anakula na kulala pale Mango garden kisha kwenye nyumba yake pale pembeni mwa Mango ikingali mzee Kadogo anaishi nyumba ya udongo,mbavu za mbwa! Mzee Kadogo anaishi kwa kuuza Gongo/local brew konyagi na Rubisi,kwa msaada wa mke wake,MA Belena na watoto wao walio na ufukara wa kutupwa! Sasa nani Mzabinazabina na aliyechanganikiwa,dr.Slaa mzalendo au Salva mlinzi wa ikulu?? Dunia hadaa,ulimwengu shujaa,kwa kuwatelekea mzee Kadogo na Ma Belena,mi namuona Salva ndo mzabina zaidi ya wale wazalendo anaowakashifu! JF mshauri uyu mzamiaji aijue familia yake kwanza kabla ya kuwakoromea wenzie. Salva, kwangu ,amechanganyikiwa yeye!

we huna sera majumgu tu yamekujaa,toa hoja
 
Apa tunataka hoja zenye evidency,na rio majungu,ohh kalelewa cjui na nani ohh cjui kamtekeleza nani,inawahusu watu humu jf?
 
Kuna kamchezo kanaibuka JF. Watu badala ya kujadili hoja wanajadili maisha ya watu. Yeye kulelewa na nani, si msaada saana kwa maendeleo ya nchi. Tujadili content ya hoja alioyotoa na kuachana na mambo yasiyo na faida.



Huko alikotoka kumesababisha afanye hivyo. Huwezi kumtenga yeye SR na hoja yake
 
Kuna kamchezo kanaibuka JF. Watu badala ya kujadili hoja wanajadili maisha ya watu. Yeye kulelewa na nani, si msaada saana kwa maendeleo ya nchi. Tujadili content ya hoja alioyotoa na kuachana na mambo yasiyo na faida.

huo ndo mchango wako kwa leo. Inaonekana unajua sana kuchangia masuala ya kitaifa! Ndo nyie wazabinazabina kama mwenzio salva. Kila upuuzi wenu tutauhanika kama ulivo sio tu Jf popote tuendako! Tunataka viongozi bora wanaojielewa sio bora viongozi! Kama hamtaki yenu yajulikane kwa nini mjitokeze kuwakashifu wenzenu?mnasema dr.slaa amechanganyikiwa? Then there is no stone to be left unturned! Tunaendelea!
 
Apa tunataka hoja zenye evidency,na rio majungu,ohh kalelewa cjui na nani ohh cjui kamtekeleza nani,inawahusu watu humu jf?

unataka hoja zenye evidence?ni evidence ipi unaitaka kwenye hoja yangu na haujaipata? I shall always call Spade a spade! Aneke said,"since men learnt to shoot without missing,we/birds learnt to fly without pearching!" you and your brethren salva shall be put to light,don't assume you are upright while others have ability!wath and be ready to appreaciate others,ata msemeje hamtamkashifu dr Slaa nikae kimya! Niko tayari kutumia gharama yangu kufanya research hata na wewe tukakuelewa vizuri ili tuache kusumbuka kwa kuwafikiria wasio timamu! Sitaki kuendelea kumfukuza mweu/salva pindi akikwapua nguo ili tusifukuzane uchi nami nkaonekana kichaa! Ni bora tukuelewe fika ili tujue tunayefikiria kauli zake alizoita uzabinazabina! Literature war is worse than verbal war,that is it!
 
wana jamii naomba mwenye tamko la salvatory rweyemamu kuwalaani chadema kwa kiswahili anipe nasikia aliandika kwa kiswahili fasaha sana sana
 
fasaha? aliandika kwa kiswahili cha mipasho. kiswahili cha kariakoo! limo humu ndani kwenye threads.
 
SALVATORY Rweyemamu, aliyekuwa mkurugenzi na mhariri mtendaji wa Habari Corporation Ltd (HCL), ni mtu wa kuhurumiwa sana. Amepata kazi ngumu.

Kama aliomba, hakujua uzito wake na kama aliteuliwa, basi aliyemteua amemkomoa kwani amempa kazi ya kufunika kwa viganja ikulu. Nia, isibaki uchi.

Kazi aliyopewa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, inasaliti misingi aliyosimamia kwa muda mrefu wa utendaji wake kama mwandishi makini: kufichua uozo badala ya kuuficha.

Alipokuwa mhariri mtendaji wa HCL, magazeti ya Rai na Mtanzania yalikuwa yakiibua uozo serikalini.

Ni magazeti hayo yaliyosababisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Dk. Hassy Kitine ajiuzulu baada ya kudaiwa kuchotewa kifisadi Sh. 60 milioni. Ni mgazeti hayo yaliyofichua rushwa katika ununuzi wa rada na ndege ya rais.

Ni magazeti hayo yaliyolaani mauaji ya watu 21 yaliyofanywa na polisi wakati wa kuzima maandamano ya wanachama wa CUF waliokuwa wanalalamikia kuporwa ushindi wao Zanzibar, Januari 26 na 27 mwaka 2001.

Salva aliongoza harakati za kupinga kusudio la serikali ya CCM kumfukuza nchini aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya HCL, Jenerali Ulimwengu. Labda ile ilikuwa.

Salva wa leo ni tofauti. Anachukia vijana aliowalea wanapomweka peupe Rais Jakaya Kikwete kwamba ana mkono katika kampuni feki ya Dowans.

Salva leo anatetea uozo, tena kwa lugha ya kukirihisha, kufitinisha, kukejeli viongozi wa siasa. Anaunga mkono wafuasi na viongozi wa CHADEMA kudundwa kwa kuandamana kudai haki yao.

Katika kukanusha tuhuma zilizotolewa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, hivi karibuni, Salva alisema Dk. Slaa ni mzushi wa kupuuzwa, na ni mtu hatari.

Akataka wanahabari watafiti kujua mmiliki halali wa Dowans. Siku mbili baadaye, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja akaibuka na majina ya eti wamiliki wa Dowans.

Kinachofichwa

Baada ya Bodi ya HCL kuuza hisa zake, aliyenunua ni Rostam Aziz, mbunge wa Igunga (CCM). Kwa hatua hiyo, Rostam aliamua kuuza hisa zake katika kampuni ya Mwananchi.

Wakurugenzi wote wa HCL walikwenda wapi? Salva na Dk. Gideon Shoo walianzisha kampuni ya ushauri wa mawasiliano ya G&S Media Consultants; Ulimwengu, Johnson Mbwambo na Shaaban Kanua walishirikiana na watu wengine kuanzisha kampuni inayomiliki gazeti la Raia Mwema.

Salva akapewa kibarua, kupitia G&S, kufanya ushawishi magazeti yasiiandike vibaya kampuni ya Richmond. Ndiye aliwapeleka Uwanja wa Ndege wanahabari kushuhudia na kupiga picha mitambo ya Richmond ilipoingia nchini kwa ajili ya kufua umeme wa dharura.

Alipohojiwa na Kamati Teule ya Bunge ya Dk. Harisson Mwakyembe, alivyoifahamu Richmond, Salva alisema alipelekwa na Rostam ambaye ni rafiki wa Rais Kikwete. Hao wote, Salva na Rostam, ni kati ya watu muhimu katika kinachoitwa mtandao wa ushindi wa Kikwete.

Rostam alikuja kuwa mweka hazina wa CCM baada ya uchaguzi mkuu. Kwa vile Richmond ilianzishwa kwa baraka za ikulu na kulikuwa na mipango ya kuigeuza Dowans, Salva akaajiriwa kuwa mpiga filimbi wa Hamelini ili kuhamisha akili za watu kama mapanya.

Ifahamike, kabla ya kuwa waziri, Ngeleja aliwahi kuwa mwanasheria wa Vodacom wakati Rostam alipokuwa mmoja wa wenye hisa. Hawa ndio wanachezea akili za watu kuficha wamiliki wa Richmond/Dowans.

Usanii huo ndio umetumika kuishtaki TANESCO mahakama ya kimataifa ya uluhishi wa migogoro ya kibiashara (ICC) na kushinda kiaina na sasa inataka ilipwe Sh. 185 bilioni. Walipoona wananchi wamechachamaa malipo yamepunguza hadi Sh. 94 bilioni.

Jiulize, kama ICC ilisema fidia ni Sh. 94 bilioni kwa nini walipandisha hadi Sh. 185 bilioni? Kwa nini Rostam amepewa mamlaka ya kisheria – Power of Attorney – kukinga mgawo huo wakati siku zote anadai hahusiki na Dowans? Kwa nini rais anayetuhumiwa yuko kimya wakati hadhi yake inachafuliwa?

Bunge limesema Richmond ni feki na Dowans ni feki, lakini ikulu imeng’ang’ania Dowans walipwe. Hata kama Salva atakejeli watu, ajue wazi Dowans imebeba anguko la kisiasa kwa Kikwete.
 
SALVATORY Rweyemamu, aliyekuwa mkurugenzi na mhariri mtendaji wa Habari Corporation Ltd (HCL), ni mtu wa kuhurumiwa sana. Amepata kazi ngumu.

Kama aliomba, hakujua uzito wake na kama aliteuliwa, basi aliyemteua amemkomoa kwani amempa kazi ya kufunika kwa viganja ikulu. Nia, isibaki uchi.

Kazi aliyopewa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, inasaliti misingi aliyosimamia kwa muda mrefu wa utendaji wake kama mwandishi makini: kufichua uozo badala ya kuuficha.

Alipokuwa mhariri mtendaji wa HCL, magazeti ya Rai na Mtanzania yalikuwa yakiibua uozo serikalini.
source.MWANAHALISI

Ni magazeti hayo yaliyosababisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Dk. Hassy Kitine ajiuzulu baada ya kudaiwa kuchotewa kifisadi Sh. 60 milioni. Ni mgazeti hayo yaliyofichua rushwa katika ununuzi wa rada na ndege ya rais.

Ni magazeti hayo yaliyolaani mauaji ya watu 21 yaliyofanywa na polisi wakati wa kuzima maandamano ya wanachama wa CUF waliokuwa wanalalamikia kuporwa ushindi wao Zanzibar, Januari 26 na 27 mwaka 2001.

Salva aliongoza harakati za kupinga kusudio la serikali ya CCM kumfukuza nchini aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya HCL, Jenerali Ulimwengu. Labda ile ilikuwa.

Salva wa leo ni tofauti. Anachukia vijana aliowalea wanapomweka peupe Rais Jakaya Kikwete kwamba ana mkono katika kampuni feki ya Dowans.

Salva leo anatetea uozo, tena kwa lugha ya kukirihisha, kufitinisha, kukejeli viongozi wa siasa. Anaunga mkono wafuasi na viongozi wa CHADEMA kudundwa kwa kuandamana kudai haki yao.

Katika kukanusha tuhuma zilizotolewa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, hivi karibuni, Salva alisema Dk. Slaa ni mzushi wa kupuuzwa, na ni mtu hatari.

Akataka wanahabari watafiti kujua mmiliki halali wa Dowans. Siku mbili baadaye, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja akaibuka na majina ya eti wamiliki wa Dowans.

Kinachofichwa

Baada ya Bodi ya HCL kuuza hisa zake, aliyenunua ni Rostam Aziz, mbunge wa Igunga (CCM). Kwa hatua hiyo, Rostam aliamua kuuza hisa zake katika kampuni ya Mwananchi.

Wakurugenzi wote wa HCL walikwenda wapi? Salva na Dk. Gideon Shoo walianzisha kampuni ya ushauri wa mawasiliano ya G&S Media Consultants; Ulimwengu, Johnson Mbwambo na Shaaban Kanua walishirikiana na watu wengine kuanzisha kampuni inayomiliki gazeti la Raia Mwema.

Salva akapewa kibarua, kupitia G&S, kufanya ushawishi magazeti yasiiandike vibaya kampuni ya Richmond. Ndiye aliwapeleka Uwanja wa Ndege wanahabari kushuhudia na kupiga picha mitambo ya Richmond ilipoingia nchini kwa ajili ya kufua umeme wa dharura.

Alipohojiwa na Kamati Teule ya Bunge ya Dk. Harisson Mwakyembe, alivyoifahamu Richmond, Salva alisema alipelekwa na Rostam ambaye ni rafiki wa Rais Kikwete. Hao wote, Salva na Rostam, ni kati ya watu muhimu katika kinachoitwa mtandao wa ushindi wa Kikwete.

Rostam alikuja kuwa mweka hazina wa CCM baada ya uchaguzi mkuu. Kwa vile Richmond ilianzishwa kwa baraka za ikulu na kulikuwa na mipango ya kuigeuza Dowans, Salva akaajiriwa kuwa mpiga filimbi wa Hamelini ili kuhamisha akili za watu kama mapanya.

Ifahamike, kabla ya kuwa waziri, Ngeleja aliwahi kuwa mwanasheria wa Vodacom wakati Rostam alipokuwa mmoja wa wenye hisa. Hawa ndio wanachezea akili za watu kuficha wamiliki wa Richmond/Dowans.

Usanii huo ndio umetumika kuishtaki TANESCO mahakama ya kimataifa ya uluhishi wa migogoro ya kibiashara (ICC) na kushinda kiaina na sasa inataka ilipwe Sh. 185 bilioni. Walipoona wananchi wamechachamaa malipo yamepunguza hadi Sh. 94 bilioni.

Jiulize, kama ICC ilisema fidia ni Sh. 94 bilioni kwa nini walipandisha hadi Sh. 185 bilioni? Kwa nini Rostam amepewa mamlaka ya kisheria – Power of Attorney – kukinga mgawo huo wakati siku zote anadai hahusiki na Dowans? Kwa nini rais anayetuhumiwa yuko kimya wakati hadhi yake inachafuliwa?

Bunge limesema Richmond ni feki na Dowans ni feki, lakini ikulu imeng’ang’ania Dowans walipwe. Hata kama Salva atakejeli watu, ajue wazi Dowans imebeba anguko la kisiasa kwa Kikwete.
 
Salva akwepa hoja, akimbilia matusi


Na Mtega Mustapha - Imechapwa 12 January 2011


Na Mtega Mustapha

IKULU ya Dar es Salaam imejiumauma, imejikanyaga na kwa lugha rahisi, imeshindwa kutoa majibu kwa tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na Dk. Willibrod Slaa juu ya uhusika wa Rais Jakaya Kikwete katika kampuni feki ya Dowans.

Hali hii inatokana na wanaomsaidia Rais kushindwa kutambua kuwa ikulu ni taasisi ya umma ambayo inatakiwa kutoa maelezeo ya kina pasipo jazba kila inapotokea haja ya kufanya hivyo.

Wananchi kwa ujumla wao au kupitia wawakilishi na viongozi wao au mtu mmoja kwa upekee, wana haki ya kikatiba kupata maelezo ya kina juu ya utendaji wa viongozi wa ikulu, ambao ndio wasimamizi wa viongozi wengine wote.

Dk. Slaa alipowasilisha tuhuma dhidi ya msimamizi mkuu wa raslimali ya nchi, waliotoa majibu walitakiwa kutafakari; kupima kama fikra za Slaa zinawakilisha mawazo na hisia za wengi wa wapiga kura au ni za kwake na chama chake tu.

Hapo, wangeweza kutoa jibu linalofaa.

Hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) inayotaka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) liilipe kampuni ya Dowans Sh. 185 bilioni au Sh. 94 bilioni si jambo dogo kwa Watanzania ambao wamepandishiwa gharama za umeme katika mazingira ya kutatanisha.

Hukumu hiyo si jambo dogo kwa Watanzania wanaopata huduma duni ya umeme kwa kuwa shirika limeelemewa na madeni huku likibebeshwa mzigo wa kutekeleza mikataba ya kifisadi kama huu uliowaleta Richmond na Dowans. Ikulu haikutoa majibu kuonyesha ukweli ni upi.

Tuliambiwa na Bunge kuwa Richmond ni kampuni hewa, na mrithi wake Dowans naye ni hewa. Sasa nani analipwa pesa katika kampuni ambayo ni hewa! Sielewi ni kiasi gani waliomjibu Dk. Slaa walipima uelewa wa wananchi kuhusu ukweli huu kabla ya kuamua kujibu kwa lugha ya kashfa.

Baada ya kupatikana taarifa kwamba TANESCO inatakiwa kulipa Sh. 185 bilioni (kabla ya kupunguza hadi Sh. 94 bilioni), wananchi wengi weledi walitaka kujua inakuaje?

Walianza kuhoji inawezekanaje shirika ambalo tayari lihoi, kumudu deni wasilolisababisha? Ikumbukwe kuwa aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa TANESCO, Dk. Idris Rashid aliwahi kutaka kujiuzulu ila alibembelezwa na rais arudi.

Kitendo cha Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Salva Rweyemamu kutoa majibu kwa Dk. Slaa yaliyojaa kashfa, kebehi na pengine yanayokaribia kuwa matusi, kwa, kinaonyesha namna watendaji wa taasisi hiyo wasivyojua dhima yao kwa jamii waliowateua kutawala.

Kwa mtazamo wowote ule ambao Ikulu au watendaji wake binafsi wanaweza kuwanao dhidi ya Dk. Slaa, watambue kuwa majibu watakayomtolea hayampatii faida yeye binafsi bali wananchi wote wanaotaka kujua ukweli kuhusu sakata la Dowans.

Walitakiwa kupima ni kwa kiasi gani tuhuma alizotoa Dk. Slaa zinawezekana ni sauti ya wapiga kura.

Katika somo la utoaji wa hoja kwa wanasiasa, tamko hili dhidi ya Dk. Slaa limekosa hoja ya msingi kwani badala ya kujibu hoja, Salva ameamua kutukana- argumentum ad hominem.

Hii ni kasoro katika kujenga hoja - logical fallacy – kwani unadhani kwa kumtukana mjumbe badala ya kujibu hoja zake, unaweza ukamtisha na kumnyamazisha kumbe unajijengea mazingira ya kuwaonyesha watu kuwa umehusika na kwa sababu huna namna ya kujitetea unaamua kumtishia kwa matusi yule anayekushitaki. Pia unatumia kipigo, kashfa au mashataka mahakamani.

Inawezekana Dk. Slaa alikosa, iwapo kweli alikosa, au kushindwa kujenga hoja yenye maelezo na ushahidi wa kutosha kuwaridhisha Watanzania na Ikulu.

Jukumu la Ikulu lilikuwa kutoa maelezo ya kina juu ya sakata la Dowans na kujitahidi kumwonyesha kila Mtanzania kuwa Rais Kikwete hahusiki kama mshirika, lakini kama kiongozi wa nchi, alitakiwa kuwawajibisha wahusika.

Unapokuwa kiongozi, ukatuhumiwa, ukaanza kujibu wapigakura kwa matusi, unatoa msisitizo kuwa ni kweli unahusika na kashfa unayotuhumiwa. Si hivyo, itakuwa unawaogopa wahusika hasa kwa sababu za urafiki nao, uanachama katika chama chenu au ufadhili wa kifedha wanaoutoa kwenu.

Wasaidizi wa Ikulu wajue si mara ya kwanza Dk. Slaa kumtuhumu Kikwete. Alifanya hivyo Septemba 2007 alipomtaja Kikwete katika orodha ya watafuna nchi – List of Shame.

Baada ya Rais kutajwatajwa, kina Salva walipaswa kumsafisha kwa kutoa maelezo ya kina ya namna asivyohusika lakini wakitoa maelezo ya nani wanahusika halisi na hatua gani wamechukuliwa.

Utaona kuwa kwa kukosekana mfumo mzuri wa utoaji taarifa, kila waziri alijisikia kuzungumza na wakazungumza kila mmoja alivyotaka na Rais ambaye ndiye msemaji mkuu wa serikali hakuweza kutoa tamko kuwatoa hofu wananchi.

Tunaambiwa TANESCO inaongeza kodi, katika kipindi ambacho imeamriwa kuilipa Dowans mabilioni ya shilingi na dola 50,000 za Marekani kwa Richmond. Ni nani anawatolea ufafanuzi wa yote haya?

Lakini majibu yale ya Salva pia yanaonyesha taswira halisi ya watu walioikalia ofisi. Kuwa hawana uwezo wa taaluma ya kusimamia mahusiano kati ya serikali na wapiga kura.

Wakati wajibu wa washauri wa rais ni kujenga mahusiano bora na wananchi, wataalamu hawa wanataka kumwona rais kuwa ni mtu asiyefaa kulaumiwa – above reproach!

Si kweli hata kidogo. Katiba inaruhusu au inatoa haki za msingi za kila mwanadamu kuzungumza hisia zake ilimradi kwa kufanya hivyo haathiri amani. Kama mtu anaona anaonewa, basi aombe jukwaa la kuzungumza ili kupinga aliyetuhumu kwa njia ileile isiyovuruga amani.

Haiwezekani kuwa umetuhumiwa kwa lugha ya amani, unaamka kutishia kumfunga, kumtukana mtuhumu, na kumbeza kwa kejeli za namna hiyo. Huko ni mtu kupungukiwa na mantiki.

Kwa lugha hii, Salva amethibitisha kuwa Rais anahusika ndiyo maana amekimbilia kujibu hoja za Dk. Slaa kwa matusi kama kinga. Na huko ni kuidhalilisha ikulu.

SOURCE;MWANAHALISI
 
SALVA ni kama taahira flani hivi ambae hajui anachoongea, siku si nyingi natamtarajia atakuwa kama makamba au tambwe hiza.
 
Kweli ukitupwa kwenye dustbin ujue na wewe ushakuwa takataka. Huitajiki tena na huna thamani.
Salva kashaingia kwenye dustbn hakuna namna ataweza kusema maovu ya ndani wakati na yeye yupo ndani.
Tumeshampoteza huyo kiumbe.
 
Hivi huwa kazi yake, kikatiba, ni nini? Kuna wakati anatoa amri Kama amiri jeshi mkuu!
 
Back
Top Bottom