Ijumaa Kuu na katazo la kula nyama

Siku ya huzuni unaanzaje kula vinono?Anateswa,kutwezwa,kutokwa damu na kusulubiwa msalabani hadi kufa.Kula nyama ni kiashiria cha furaha na ufahari.Kwa nini ulie huku unacheka?Halafu ni siku moja tu/masaa machache nini kinakushinda?Kwani kila siku huwa unakula nyama?
Imeandikwa wapi?
 
Wewe ndio unachanganya madema.
Ushindi wa imani ya kikristo ulipatikana msalabani (wakati Yesu anakufa) na sio kaburini (wakati anafufuka). Ndio maana makanisa yanatundika misalaba kama alama ya ushindi na sio kutundika makaburi.

Kufufuka kwa Yesu ni matokeo ya kufa kwake, asingekufa na kufufuka kusingekuwepo. Hivyo msingi upo kwenye kufa kwa Yesu.
Ingekuwa hivyo uwazavyo tungeanza kufurahi siku anatundikwa msalabani.Siku ya kufurahi zaidi ni anapofufuka.Hata hivyo,msalaba ni alama "chungu" ya ukombozi wetu tumuaminio,sikatai.Unaelewa kwa nini hatusemi Hallelujah siku ya ijumaa,jumamosi ila jumapili anapofufuka?Fuatilia.
 
Siku ya huzuni unaanzaje kula vinono?Anateswa,kutwezwa,kutokwa damu na kusulubiwa msalabani hadi kufa.Kula nyama ni kiashiria cha furaha na ufahari.Kwa nini ulie huku unacheka?Halafu ni siku moja tu/masaa machache nini kinakushinda?Kwani kila siku huwa unakula nyama?
Hayo yote ni Sawa mkuu,lakini kinachotatiza ni andiko katika Biblia takatifu.Na pia ukumbuke Yesu aliteswa ili neno litimie na sio kwamba alionewa hapana.
 
Kufa kwa Yesu kristo msalabani ni jambo la furaha, shangwe na ushindi katika imani ya Kikristo maana ndio lilizaaa ukombozi, sasa kwanini watu wakae na huzuni, unyonge na kujinyima?

Wakristo kuleni vinono leo.
Umenena ukweli kiongozi.
 
Hayo yote ni Sawa mkuu,lakini kinachotatiza ni andiko katika Biblia takatifu.Na pia ukumbuke Yesu aliteswa ili neno litimie na sio kwamba alionewa hapana.
Sijapinga.Tupo pamoja.Tunasikitika na kujitafakari kwa dhambi zetu.Mwokozi alipitia mateso,uchungu,kipigo, kutwezwa na kifo.Hapo ndipo nasi tunapata(kukumbuka)wasaa wa kujipima.Huwezi kujipima huku unachekekelea hovyohovyo.Unatulia.Unajinyima.Unajitesa kidogo.Unajinyenyekeza hasa!Wigwa mwanamayu?
 
Ingekuwa hivyo uwazavyo tungeanza kufurahi siku anatundikwa msalabani.Siku ya kufurahi zaidi ni anapofufuka.Hata hivyo,msalaba ni alama "chungu" ya ukombozi wetu tumuaminio,sikatai.Unaelewa kwa nini hatusemi Hallelujah siku ya ijumaa,jumamosi ila jumapili anapofufuka?Fuatilia.
Mimi nimekupa facts za kiimani na sio hisia za kiimani. Ukombozi wa wakristo uko kwa kufa kwa Yesu kristo. Kwanini? Yesu hakustahili kufa, lakini kwa sababu ya dhambi zetu ilimpasa kufa yeye ili sisi tupone. Huo ndio ushindi wa imani ya kikristo. Hakukuwa na mtu mwingine ambaye angeweza kulipa hiyo gharama lakini Yesu akailipa kwa gharama ya kifo chake pale msalabani. Kwanini tusifurahi kwa hilo?

Kufufuka kwa Yesu ni chapter ingine kabisa katika imani ya Kikristo, kufufuka kwake ni udhihirisho wa kuwa kufa kwake kulifanikiwa kulipa deni letu la dhambi msalabani kikamilifu na akashuka kuzimu kumnyang'anya shetani mamlaka yote. Ufufuo wa Yesu haifuti dhambi zetu bali unatupa mamlaka ya kumshinda shetani kwenye nyanza zote.
 
Naombeni anaelijua andiko linalokataza wakristo Kula nyama siku ya Ijumaa kuu.Najua ni suala la kiimani,lakini msingi wa Imani ya kikristo,ni Biblia,hivyo tujuzane hilo andiko liko kitabu gani ndani ya Biblia
Ni kama wewe upite somewhere ukute watu wamempiga mtuhumiwa na kumkatakata mapanga na kumtawanya utumbo, then muda kidogo uingie banda la supu uagize utumbo ndizi, ile memory ya kuona tukio litakufanya ujisikie vibaya hata kuagiza hiyo supu yenyewe.

Ijumaa kuu ni siku ambayo Bwana Yetu Yesu Kristu alisulubiwa vibaya mnooo, ni siku ambayo tunatafakari matendo ya uchungu aliyopitia.

Kwa kifupi kwenye Biblia sidhani kama kuna maandiko juu ya hilo, ila ni sehemu ya Kanisa Katoliki kuliishi kwa imani.

Kama itakuumiza kutokula nyama its your fault. Sie tunakula sato wa kuchoma.
 
Mimi nimekupa facts za kiimani na sio hisia za kiimani. Ukombozi wa wakristo uko kwa kufa kwa Yesu kristo. Kwanini? Yesu hakustahili kufa, lakini kwa sababu ya dhambi zetu ilimpasa kufa yeye ili sisi tupone. Huo ndio ushindi wa imani ya kikristo. Hakukuwa na mtu mwingine ambaye angeweza kulipa hiyo gharama lakini Yesu akailipa kwa gharama ya kifo chake pale msalabani. Kwanini tusifurahi kwa hilo?

Kufufuka kwa Yesu ni chapter ingine kabisa katika imani ya Kikristo, kufufuka kwake ni udhihirisho wa kuwa kufa kwake kulifanikiwa kulipa deni letu la dhambi msalabani kikamilifu na akashuka kuzimu kumnyang'anya shetani mamlaka yote. Ufufuo wa Yesu haifuti dhambi zetu bali unatupa mamlaka ya kumshinda shetani kwenye nyanza zote.
Mkuu,changamoto yako unaanza kuulewa mwisho kabla ya kuuona mwanzo.Tupo pamoja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom