Ijumaa iwe siku ya mapumziko: Nini ushauri wako?

Ijumaa iwe siku ya mapumziko: Nini ushauri wako?

Wasabato hawajawekewa siku ya kupumzika Jumamosi haendi kazini,lakini Jumapili yuko mzigoni,sasa ndugu zangu waislamu wanaweza kuiga tu wasabato piga kazi mpaka alhamis jumapili au jumamosi nenda kamalizie siku yako.Kwa kawaidamtu anatakiwa kufanya kazi masaa nane kwa siku na masaa arobaini na tano kwa wiki.Unajiamulia wala usisubiri katiba itakuchelewesha.
 
m.kwere kafanikiwa kuwatoa watu kwenye economic failure yake na kujikita kwenye udini..
 
Kwanini iwe siku ya mapumziko? sisi Waislaam ni siku yetu ya kukutana na kupeana mawaidha kwa yaliyojiri wiki nzima, kujuliana na kupanga mipango yetu mingine ya wiki nzima ijayo. Hatutaki iwe siku ya kupumzika.
 
mbona kwa dar kuanzia saa nane siku hizi ni mapumziko....maana biashara zote zinafungwa kuwapisha wanaondamana baada ya sala
 
[h=1]¡®Ijumaa iwe siku ya mapumziko¡¯[/h]
ico_plus.png
SHARE
ico_bookmark.png
BOOKMARK
ico_print.png
PRINT
ico_email.png
EMAILRATING
Posted Wednesday, October 31 2012 at 22:52IN SUMMARY¡°Mbunge wa chama cha upinzani anatoa mchango wake anaambiwa kaa chini hata kama ana mchango mzuri kiasi gani¡* Spika akiwa kwenye chama fulani inaleta mpasuko¡±alisema. Pia alitaka Katiba Mpya iweke kifungu kitakachoilazimisha Tume ya Uchaguzi (NEC),Hussein Nyari, SihaMKAZI wa Kijiji cha Kikwe wilayani Siha, Halima Munisi ametaka katiba ijayo iitambue siku ya Ijumaa kuwa ni siku ya mapumziko kama zilivyo siku za Jumamosi na Jumapili. Munisi alitoa pendekezo hilo juzi wakati akitoa maoni yake mbele ya kamati ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa ikiongozwa na Profesa Mwesiga Baregu. Kwa mujibu wa mwananchi huyo, Ijumaa kutokuwa ni siku ya mapumziko hasa kwa kuwa ndio siku ya kumuabudu Mola kwa Waislam si sahihi na kutaka siku hiyo iwe ya mapumziko. Mkazi wa Kitongoji cha Nasai, Stanslaus Mallya alitaka katiba ijayo iweke kifungu ili Mawaziri watakaoteuliwa katika Baraza la Mawaziri wasiwe wabunge wa kuchaguliwa wala kuteuliwa. Mallya alisema kitendo cha Mawaziri kushika kofia mbili ya Uwaziri na Ubunge, kinawafanya wasitekeleze majukumu yao ipasavyo hasa pale inapofikia mahali pa kuibana Serikali. Kwa upande wake mkazi wa Ndoroso, Solomon Mmari alitaka Spika wa Bunge asiwe Mbunge na wala kuwa mfuasi wa chama chochote cha siasa ili aweze kutenda wajibu wake kwa haki. Hoja hiyo iliungwa mkono na Radegunda Nyabu, mkazi wa Magadini Bomang¡¯ombe ambaye alisema endapo Spika anatokana na chama cha siasa, kuna kila sababu ya kutoa upendeleo. ¡°Mbunge wa chama cha upinzani anatoa mchango wake anaambiwa kaa chini hata kama ana mchango mzuri kiasi gani¡* Spika akiwa kwenye chama fulani inaleta mpasuko¡±alisema. Pia alitaka Katiba Mpya iweke kifungu kitakachoilazimisha Tume ya Uchaguzi (NEC), kutopanga siku ya uchaguzi kwa siku zile ambazo zinatumika kumwabudu Mungu. Kwa mujibu wa Nyabu, siku hizo ni Ijumaa kwa waumini wa Kiislam na Jumamosi na Jumapili kwa waumini wa Kikristo ili kila mmoja aweze kumwabudu na kumtukuza mola wake.
Hapo "siku ya ijumaa wapumzike!" Amekulupuka tu! Sababu Qurani imewaamrisha kwamba; "Mkisha kuswali tawanyikeni kwenye ardhi mkafanye kazi!" labda aombe hii ayat ifutwe kwanza!
 
Kwanini iwe siku ya mapumziko? sisi Waislaam ni siku yetu ya kukutana na kupeana mawaidha kwa yaliyojiri wiki nzima, kujuliana na kupanga mipango yetu mingine ya wiki nzima ijayo. Hatutaki iwe siku ya kupumzika.
Hizo stori mnapiga mkiwa kazini? Au!
 
Why J.mosi na J.pili mapumziko & not Ijumaa? Kuna jambo limejificha nyuma ya kanisa hapa, Ka-saa ka ukombozi ni sasa
 
hakuna aliyemzuia kupumzika yeye na familia yake hata kwa katiba ya sasa. Cha msingi watumishi wa umma wafanye kazi hadi saa 10.30 jioni halafu warudi nyumbani wakapumzike. Mimi huwa nafanya kazi jumatatu hadi jumapili, lakini pia huwa napumzika jumatatu hadi jumapili.

Mambo ya kufikiria kulala kwenye majamvi misikitini siku nzima ndio yanayotuletea umasikini




shame on you...!
Lione kwanza
 
Haina haja kupumzika ila kazi za serekali na taasisi mbali mbali kwa cku ya ijumaa zianze saa 8 mchana baada ya watu kutoka mckitini asubuhi ni muda kutembelea ndugu na jamaa na kuwahi mapema mckitini
 
Kazi sisi mabota?
daah, Mkuu imekuwa hayo?Si qaraa inakujuza kwamba muumini akikasirika Akatawadhe! Au? NAGHAIRI KUWA MUISLAMU SABABU YA WAISLAMU!
 
daah, Mkuu imekuwa hayo?Si qaraa inakujuza kwamba muumini akikasirika Akatawadhe! Au? NAGHAIRI KUWA MUISLAMU SABABU YA WAISLAMU!

Kazi kwako, mimi inanihusu nini? hata uwe baniani unaeabudu panya, hayo ni yako nami na yangu.
 
Kazi kwako, mimi inanihusu nini? hata uwe baniani unaeabudu panya, hayo ni yako nami na yangu.
Kulingania imani ndio maamrisho ya allah! Umekata tamaa kama mzee mzima!
 
Na hko misikitini mkienda hata hamjiesabu, hadi leo hamjijui mko wangapi

Kwanini iwe siku ya mapumziko? sisi Waislaam ni siku yetu ya kukutana na kupeana mawaidha kwa yaliyojiri wiki nzima, kujuliana na kupanga mipango yetu mingine ya wiki nzima ijayo. Hatutaki iwe siku ya kupumzika.
 
Labda wewe jumapili huwa unalala, wenzako tunaenda kusali na mzigoni unaenda kama kawa

Nie mnaotaka Ijumaa iwe mapumziko nawauliza hivi watangazaji, manesi, madktari, polisi, wanajeshi n.k wao siku yao ya kupumzika ni ipi

QUOTE=mdau wetu;4984351]Ijumaa iwe siku ya mapumziko badala ya Jumapili[/QUOTE]
 
Jumamosi haikuwekwa kupumzika kwa sababu ya Wasabato. Rais mstaafu Mwinyi alisema kwamba siku ya jumamosi na Jumapili wafanyakazi wafanye shughuli za kujitafutia kipato kwani mshahara ulikuwa hautoshi.

To put records right. Ikumbukwe kuwa kazi katika ofisi za Serikali zilikuwa zinaanza saa 1.30 hadi saa 8.30 Jumatatu hadi Ijumaa na Jumamosi ilikuwa saa 1.30 hadi saa 6.30. Sasa hivi watumishi wa Serikali wanaanza kazi saa 1.30 hadi saa 9.30 kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa. Idadi ya masaa ya kazi kwa wiki/juma ni ile ile.
Hii dhana ya kufikiri kila wakati Wakristo wanapendelewa ni chafu na inajenga chuki za kidini. Narudia tena kupumzika Jumamosi kusihusishwe na Siku ya Sabato.
Kwa wakristo siku ya jumapili ni siku ya mapumziko. Sina uhakika kwa waislam kwa mujibu wa imani yao kama Ijumaa ni siku ya mapumziko. Hata hivyo sijawahi kusikia hilo kutoka kwa waislam. Isije ikawa tunahangaika na watu wavivu na wasiotaka kufanya kazi na kuja na visingizio ambavyo ni kinyume cha mafundisho ya dini yao.
 
Back
Top Bottom