Ijue siri kuu ya mahusiano katika Ulimwengu wa Roho

Jamaaa anawalisha wakristo matango pori
Najaribu kumuangalia CR7, bilionea namba moja, Tiger wood, Jinsi walivyo fanya zinaa sijui uasherati lakini bado wana ukwasi wakutosha...

Naenda mbali kwa bilionea namba tatu ambaye hana imani na uwepo wa Mungu lakini uchumi wake ndio una zidi kupaa,

Sasa swali je haya mafundisho yake yanaengemea upande hupi zaidi...

Condom ukitumia je, ina weza kuwa suluhu? Maana vimiminika havito weza hifadhiwa kwa mwanamama au mwanamke...

Nikaenda mbali kidogo kuuliza kuhusu Elton John, Michael Scofield, na mapadre wa kikatoliki wenye tabia zinazo fanana na mambo jinsi moja

Mungu ampe moyo mzuri wa kutufundisha vizuri zaidi elimu aliyo nayo
 
Najaribu kumuangalia CR7, bilionea namba moja, Tiger wood, Jinsi walivyo fanya zinaa sijui uasherati lakini bado wana ukwasi wakutosha...

Naenda mbali kwa bilionea namba tatu ambaye hana imani na uwepo wa Mungu lakini uchumi wake ndio una zidi kupaa,

Sasa swali je haya mafundisho yake yanaengemea upande hupi zaidi...

Condom ukitumia je, ina weza kuwa suluhu? Maana vimiminika havito weza hifadhiwa kwa mwanamama au mwanamke...

Nikaenda mbali kidogo kuuliza kuhusu Elton John, Michael Scofield, na mapadre wa kikatoliki wenye tabia zinazo fanana na mambo jinsi moja

Mungu ampe moyo mzuri wa kutufundisha vizuri zaidi elimu aliyo nayo
Siwezi kukujibu kwa sababu huna msingi wa Biblia. Hivyo amini utakavyo, lakini yote hayo yameandikwa wazi, hakuna swali jipya hapo
 
Mimi huwa nahoji sana swala la kusubiria kuingia katika ndoa baada ya kumaliza maswala ya elimu na kupata kazi. Hivi watu wanaopendana katika umri wa 19 years ay 20 years hawawezi kufunga ndoa na wakaendelea kufukuzana na maisha, y tunafosi kusubiri matokeo yake madogo wanatumia P2 kwa sana, wanatoa ujauzito, wanazini kwa sana na wengine wanapiga punyeto hadi basi.
Umewaza vema mkuu. Ndio huo utamaduni tangu agano la Kale. Mabinti walichumbiwa mapema kabisa, tazama mfano wa Mariamu mama wa Yesu. Baada ya kubadili mfumo wa Mungu ndipo meza ikapinduliwa. Hii ni sababu leo hii mafundisho ya kweli ya Mungu yanaonekana ni upuuzi na hayawezekani. Lakini kumbuka hili, Mungu ni Yeye yule jana, leo na hata milele. Habadiliki kamwe isipokuwa wanadamu nduo tutabadilika, hajawahi kuanza kumwacha mtu bali mtu ndio atamwacha Mungu kwa kufuata njia zake mwenyewe. Mstari wa Mungu uko pale pale.
 
Interjection

Hebu tuone chanzo cha nguvu za mwanadamu na jinsi gani zimeunganishwa na mafanikio. Wengi walihoji ni kwa vipi utajiri ufungamanishwe na mahusiano. Twende kazi...

Mwanzo 1
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
² Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
³ Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

.........

Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.

.........

Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.

..........

¹¹ Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo.
¹² Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

.........

¹⁴ Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka;
¹⁵ tena iwe ndiyo mianga katika anga la mbingu itie nuru juu ya nchi; ikawa hivyo.



Hizo aya zote hapo juu zinaongelea uumbaji wa Mungu. Angalia kwa makini jinsi gani Mungu alivyoumba KWA KUSEMA TU. Kwa nini iliwezekana? Kwa sababu Yeye pia ni Roho, hana mwili wa nyama. Hivyo kila neno atamkalo ni Roho kamili nalo litatukia kama alivyoagiza.

Waswahili wana msemo, kinywa huumba, unajua kwamba msemo huo umefanana na hiki kilichomo kwenye Biblia? Sio kila kitamkwachp basi kinakuwa, bali ni kile ambacho kina nguvu ya roho. Kwamba mtu akiweka moyo wake katika jambo na akalitamka kwa kukusudia kabisa bila shaka, basi humtokea aliyetamkiwa, hasa akiwa amemtendea ubaya huyo atamkaye.

Kwa hiyo Mungu aliumba kwa kusema tu, na ikawa hivyo. Sasa wengi hupotoka hapa, wakidhani ALIPOTAMKA KUFUMBA NA KUFUMBUA MARA ARDHI INATOKEA, WANYAMA WANATOKEA NK. Haikuwa hivyo, kilichoganyika hapo ni UUMBAJI WA ROHONI, KATIKA ULIMWENGU WA ROHO hayo mambo yalithibitika kwanza kabla ya kudhihirika kwenye ulimwengu wa mwili. Huamini? Tuendelee...[/b][/b]

²⁰ Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.
²¹ Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
²² Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi.


Kumbe Mungu aliwabariki hata wanyama pia, ila baraka zao ziko tofauti na mwanadamu. Wanyama wao walipewa NGUVU ya kuijaza nchi na bahari tu, wala hawakupewa KUITIISHA, YAANI kuwa watawala. Ni kwa kutumia nguvu hiyo wanatambua majira ya mwaka, wanajua wapi wapate maji ama chakula waweze kuendeleza nguvu ya kuijaza dunia. Ukitaza Simba kwa mfano: nguvu yake huthibitika kwa kuyamiliki majike, ndio maana huwezi kukuta madume mawili yakawa ndani ya kundi moja. Hakika mmoja lazima auawe, ndipo zilipo baraka za Mungu,hapo penye kuujaza ulimwengu.

Kwa binadamu ikoje?
.........

²⁶ Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.[/I]

Kwa hiyo kwanza kabisa uumbaji wa mwanadamu ulikuwa tofauti, KWA SURA NA MFANO WETU. Hapo ndipo penye mvurugano mwingine wa kitafsiri, lakini ni rahisi tu. Sura ya Mungu ni HAKI YAKE (righteousness) na mfano wake ni kutawala kwa sababu Yeye ni mtawala wa vyote.

“Bali mimi nikutazame uso wako katika haki, Niamkapo nishibishwe kwa sura yako.”

— Zaburi 17:15
“As for me, I will behold thy face in righteousness: I shall be satisfied, when I awake, with thy likeness.”
— Psalms 17:15 (KJV)


Hapo mzaburi anasema nikutazame uso wako katika haki, kila ninapoamka asubuhi NIRIDHIKE PALE NINAPOFANANA NA SURA YAKO. Ndivyo alivyo mwanadamu siku ya kuumbwa kwake. Tuendelee...

²⁷ Mungu akaumba mtu kwamfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

Kumbe toka siku ya kuumbwa mwanamume, mwanamke pia aliumbwa!! Kwa vipi? Waliumbwa kwenye ulimwengu Wa roho, ni kama mjenzi anapoandaa ramani yake kwanza kisha iakiona ni njema hujenga.

Tena ona hapo inaposema Mungu aliumba MTU kwa mfano wake. Haisemi watu kana kwamba ni wengi, bali MTU!! Halafu inamsema huyo mtu wa mfano wa Mungu kuwa ni mwanamume na mwanamke. Hii inaonyesha wazi kuwa mwanamke na amwanamune walikuwa mwili mmoja toka kuumbwa kwao, hakuumba mwanamumebpeke yake na mwanamke peke yake, ok?

²⁸ Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

Hapa Mungu akambariki huyo MTU aliyemwumba, alimwambia ZAENI.... Iweje wawe wengi? Ni kwa sababu Mungu alimwumba mtu mmoja mwenye sehemu mbili tayari,yaani alikuwa na roho moja yenye sehemu ya mke na mume ili kuwa kamilifu.

Kwa sababumwanadamu ni zaidi ya mnyama, akampa pia KUITIISHA DUNIA. Hapo ndipo nfuvu ya kutawala ilipokuja, kama Yeye alivyo mtawala. Kwa sura na mfano wake. Akampa jimbo la kutawala nalo ndilo dunia yetu.

.........
³¹ Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.

Baada ya kuumba katika roho akaona kila kitu kimekaa sawa kabisa, lakini kumbuka hakuna kitu kilichotokea physically bado. Ndipo tunasema kwa kuwa tu mfano wa Mungu, mambo yetu yanapaswa kuumbwa katika roho kwanza, kisha huja kudhihirika katika mwili.

Hiyo ni kanuni ya maisha ya mwanadamu tangu kuumbwa kwake, atawale kutokea rohoni (kumbuka mpaka hapo bado mwanadamu ni roho, hana mwili bado). Ndivyo alivyoishi Yesu Kristo kwani alisema wazi, hakuna neno alilisema isipokuwa amemsikia Baba akilisema. Kwamba hakuenenda kwa kuangalia mambo ya duniani bali kusikiliza mambo ya rohoni ambayo ndiyo yanayomwongoza kuitawala dunia.

Tuendelee.....[/I]


Maya Angelou, Africa Tanzania, dumbi, LOGARITHM, Sergei Lavrov, LOVE U JF, korino, Mshuza2, park don, Surya, big-diamond, Mwanamena, Tajiri wa Magomeni, dudupori, Bubolwa Chura, Patra31, Depal, alumn, Ed Kawiche, Sexless, The 13, Avriel, Styles
yna2, ngebo, iMind, HoneyBee, Will jr, gbmm, True Believer, Saint Anne[/i][/B][/B], Nature
 
Yesu alitenda kwa kuongozwa na Roho

Yohana 5
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁹ Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile.


Hivyo ndivyo alivyopaswa kuishi mwanadamu, anatenda kile akionacho katika roho. Dhambi ilifungua macho ya nje hata kusababisha tusiweze kuona katika roho. Ndio maana majanga na mabalaa hutukuta tukiwa hatujui, wakati ilitupasa tuyaone kabla.

Kwa hiyo tumeona jinsi gani Baba alifanya uumbaji KATIKA ROHO kwanza kabla ya kutokea wazi wazi. Kisha kila alupotazama akaona kila kitu ni chema. Hapa kumbuka Kristo alisema:

Mathayo 21
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
²¹ Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka.
²² Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.


Huo ndio msingi, unapoomba kuhusu jambo lolote unazitikisa mbingu, sasa ili uweze kupokea AMINI kwanza. Kama una mashaka na jambo unaloomba ni heri usiombe kabisa. Mungu aliumba na alupomaliza hakuwa na shaka yoyote, ALIONA KILA KITU NI CHEMA.

Mwanzo 1
³¹ Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.


Sasa tuje kwenye uhalisia, ni kwa jinsi gani nimeshika kusema huo uumbaji ulikuwa kwa jinsi ya roho pekee? Kwa nini hakuna kitu kilikuwapo tayari katika mwili baada ya hizo siku sita? Je, ni kweli Mungu alipoumba binadamu alimuumba Adamu na Hawa ndani ya MTU MMOJA aliyemwita ADAMU? Kuelewa majibu ya haya maswali ni ufunguo wa kuelewa uhusiano waNDOA NA ULIMWENGU WA ROHO. Utapata elimu ambayo haijachakachuliww na theolojia bali ni PURE WORD OF GOD, kutoka chanzo halisi, BIBLIA TAKATIFU. Tuendelee...

Wahubiri wengi sana wamekuwa wakidai kwamba sura ya kwanza ya kitabu cha Mwanzo inahusu uumbaji kwa ujumla wake na kisha sura ya pili hufafanua kwa kina. Leo utashuhudia mwenyewe kwa nguvu ya Roho wa Mungu jinsi maandiko haya yalivyo wazi na wala hayahitaji elimu ya teolojia kuujua ukweli.

Mwanzo 2
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.


Hapa mbingu na nchi zilikamilikw katika ulimwengu wa roho, lakini mbingu na nchi zilikuwa ukiwa tena utupu. Ni vema kuona kuwa hapa haiongelei uumbaji wa malaika kwani hatukupewa maelezo zaidi. Hii ni jumla ya zile siku sita za uumbaji na vile vyote vilivyoumbwa katika siku hizo.

² Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.
³ Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.


Hii ni mada nyingine hivyo nitaiacha hapa

⁴ Hivyo ndivyo vizazi vya mbingu na nchi zilipoumbwa. Siku ile Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi

Umeona? Mungu anaongelea vile alivyoumba ndani ya siku sita Tu. Habari ya malaika kama wengi wanavyoamini haipo hapa.

⁵ hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;
⁶ ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.


Hapa ndipo tunapata kweli halisi. Licha ya uumbaji wa siku sita, hakukuwa na kitu BADO. Licha ya kuumbwa mawingu mvua ilikuwa haijanyesha bado. Ardhi haikuwa na mimea nk. Sababu? Mtawala hakuwa ameumbwa bado, mwanadamu hakuwapo.

⁷ Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Hapa ndipo Mungu alipomfanya mwanadamu kwa jinsi ya mwili. Mwanzoni alimwumba katika roho tu. Angalia hilo tendo la kumpulizia PUMZI YA UHAI. Tuendelee...

⁸ Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.

Leo jifunze neno moja, Mungu alifanya bustani ya Edeni, lakini ndani ya hiyo Edeni akapanda kijibustani UPANDE WA MASHARIKI wa hiyo Edeni. Kwamba alifanya bustani ndani ya bustani.

⁹ Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Unaona? Kazi ya kuchipusha miti inaendelea hata baada ya siku sita za uumbaji. Tena tunaona mti wa ujuzi wa mema na mabaya ukiwekwa kwenye bustani ya Edeni katikati.

........
¹⁵ Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.
¹⁶ Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,
¹⁷ walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.


Yako mengi ya kueleza lakini naandika kifupi ili kutotoka nje ya mada. Kwa hiyo mtu akawekwa Edeni kama mtawala wake. Kumbuka kuna kijibustani kingine upande wa Mashariki.


Maya Angelou, Africa Tanzania, dumbi, LOGARITHM, Sergei Lavrov, LOVE U JF, korino, Mshuza2, park don, Surya, big-diamond, Mwanamena, Tajiri wa Magomeni, dudupori, Bubolwa Chura, Patra31, Depal, alumn, Ed Kawiche, Sexless, The 13, Avriel, Styles
yna2, ngebo, iMind, HoneyBee, Will jr, gbmm, True Believer, Saint Anne[/i][/B][/B], Nature
 
Yako mengi ya kueleza lakini naandika kifupi ili kutotoka nje ya mada. Kwa hiyo mtu akawekwa Edeni kama mtawala wake. Kumbuka kuna kijibustani kingine upande wa Mashariki.

¹⁸ Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.

Hapo ndipo tunakutana na uumbaji wa mwanamke. Mungu alishawaumba katika Roho tangu siku ya kwanza kisha akawaumba katika mwili mwanamke akiwa sehemu kamili ya Adamu mume. Jiulize ni kwa vipi Mungu aliumba viumbe vyote wawili wawili halafu Adam akawa single? Tayari katika design yake alishamweka Hawa ndaniya Adamu.

¹⁹ Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.
²⁰ Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.


Adamu alikuwa na Hawa ndaniyake lakini HAKUONEKANA katika macho ya nyama. Ingekuwa kwamba Adamu aliumbwa peke yake akiwa mtu mume kamili, basi huenda angewawakia tamaa wanyama. Lakini tayari Mungu alikuwa amemuumba akiwa na nafsi ya mkewe ndani yake, ndio maana hakuna sehemu anaonyesha kusikitika, bali Mungu mwenyewe kwa utaratibu wa uumbaji wake akaona si vema awe peke yake.

²¹ Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
²² na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.[


Itoshe kusema Mungu alimwumba mwanadamu toka udongo, kisha akamtenganisha kupata mwanamke na mwanamume. Alichukua nyama ambayo tayari ilitoka kwenye udongo kisha akaingiza sehemu roho ya Adamu ndani yake. Why? Hakuna mahali ambapo Mungu alimpulizia pumzi ya uhai huyu mwanamke siku ya kuumbwa kwake.

Sasa ona tofauti ya maneno hapa, katika kuumba mwanamume neno lililorumika ni yatsar, lakini kwa mwanamke neno la kuumba ni banah. Kwamba Mungu akamuumba (yatsar) mwanamke ... halafu Mungu akamuumba (banah) mwanamume.. Kwa maana halisi, 'Mungu ALIMFINYANGA MWANAMUME kutoka mavumbini lakini ALIMTENGENEZA (fashion) mwanamke toka ubavuni. Ndio maana mwanamke akatoka na sura na umbo zuri la kuvutia ili Adamu avutwe naye.

Adamu alipozinduka usingizini tayari sehemu ya roho yake ishatolewa, ndio maana hakuhitaji maelezo mengi bali moja kwa moja akamtwaa mwanamke na kumwagia sifa lukuki. Hivyo mwanamke NI SEHEMU HALISI YA MWANAMUME na ndio maana MUUNGANIKO HUTOKEA KATIKA ROHO, KUTENGENEZA NAFSI MOJA kama vile Mungu alivyoumba hapo mwanzo. Inaposemwa na Yesu Kristo kuwa tangu mwanzo haikuwa hivyo, inarejea UUMBAJI. Mwanamke na mwanamume walikuwa NAFSI MOJA na ROHO MOJA tangu kuumbwa kwao. Walitengwa kwa kuwekewa miili tofauti, ili kuendeleza uumbaji. Ndio maana tendo la ndoa ni muunganiko wa kiroho ili kurejea uumbaji wa Mungu, na hivyo linafanywa kwa nafsi moja tu.

²³ Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Baada ya kumwona mwanamke alivyoumbwa ndipo akamtwaa. Hapa ndipo ilipo ASILI YA MAPENZI!! Mungu alipoitoa sehemu ya roho ya Adamu kumfanya Hawa aliacha uwazi, vacuum, ambayo inahitaji kujazwa. Mtu pekee anayeweza kuziba huo uwazi ni mwanamke kwa sababu roho yake ndio iliyotolewa kwa mwanamume, hivyo inarejea kwake. Sexual attraction ilianzia hapo, mapenzi yakawa tendo la rohoni wala si mwili. Roho zinavutana kwanza kisha mnakamilisha kwa kulala pamoja na kuingiliana. MAMBO YOTE HUANZA KATIKA ROHO KISHA HUDHIHIRIKA KATIKA MWILI.

²⁴ Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
²⁵ Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.


Mwanamume atamwacha baba na mama yake, why? Mwanamume tangu kuzaliwa kwake roho yake haikufungamanishwa na wazazi wake. Akibalehe na kuuacha utoto roho yake huliona pengo lililoachwa tangu kuumbwa Hawa, hivyo hutangatanga huku na huko kuitafuta ile sehemu yake iliyoondoka.

Mwanamke yeye alitolewa kwa mwanamume na akawa kiumbe ambaye nguvu zake zimo katika mwanamume. Kwamba yeye anakaa kwa wazazi wake huku akitazamia kwamba kuna nguvu itakuja kumwondoa kwao, nguvu ambayo ndio sehemu yake halisi. Sasa huu ni muunganiko wa kiroho, sio kimwili, kwamba mwanamume atamwacha baba na mama kwa kujitenga nao. Ni roho yake kuungana na roho ya mkewe KWA TENDO LA NDOA, ndio maana ikaandikwa NAO SI WAWILI TENA BALI NI MWILI MMOJA. Kumbe unapofanya tendo la ndoa umejiunganisha na mwenza wako kuwa mwili mmoja. Yaani umemwacha baba na mama yako, sasa umejiona umekuwa mtu mzima, ukajitwalia namna ya mke, ukaambatana naye kwa kufanya naye ngono, kwa hiyo ninyi si wawili tena kwa sababu roho zenu zimerudiana na mmekamilisha ule uumbaji wa mwanzo.

Ndipo Kristo katika Mathayo 19 akaongeza kusema ALICHOKIUNGANISHA MUNGU MWANADAMU ASIKITENGANISHE, ikimaanisha kwamba TENDO LA KWANZA LA NDOA ndilo tendo la agano. Sasa hakuna tena mwanadamu anayeweza kuwatenga waliojiunganisha kwa uzinzi bali ni rehwma ya Mungu mwenyewe. Kama umewaacha wazazi wako ukaambatana na mwenzako katika uzinzi, ninyi tayari ni mwili mmoja, nafsi zenu zimeungana katika roho. Mwanadamu wa jinsi ya mwili hana mamlaka tena, bali Yeye aliyeziumba roho zenu.

Ndipo tunapata MAANA YA HAYO MANENO, alichokiunganisha Mungu - yaani agano la damu, mwanadamu asikitenganishe - yaani asije mwanamume mwingine kumwoa huyu mwanamke mwenye agano la ndoa tayari na mwanamume mwingine!! Hapa haikumaanisha kimwili kama tunavyoamini hivi sasa kwamba mume na mke wakifunga ndoa KANISANI basi mwanadamu asiwatenganishe. Ukiyachunguza hayo maandiko, kesi ilikuwa ni ya talaka. Hapo ndipo tunaelewa zaidi maana ya ISIPOKUWA KWA SABABU YA UASHERATI. Kwamba huyu mwanamke alishatembea na mwanamume mwingine kabla ya ndoa, hivyo tayari ana agano!! Hiyo pekee ndio sababu ya MWANAMUME KUMWACHA MWANAMKE. Tena ni wakati gani? Wakati wa KUFUNGA AGANO!! Wakati wa kuingiliana, kama mwanamke hana bikira, kwa sababu ulupomwingilia ULIFUNGA NDOA, unaruhusiwa kumpa talaka. Hapo kifungo chako hakitakuwapo katika roho.

Ukielewa hivi ndipo unaweA sasa kusoma Kumbukumbu la Torati na kuelewa ni kwa nini waasherati na wazinzi waliuawa. Ni mambo ya kiroho zaidi. Pia ndio maana huwa ninasisitizani kwa nini unapotaka kuoa mnapaswa kujitakasa na kuomba rehema ya Mungu ili ndoa yenu idumu (kama mke si bikira). Itakuwa kama wanaume aliotembea nao wapo hai, agano lao ndanai yake pia litaendelea kuwa hai.. Ndipo inakuwa rahisi sana kwa wao kumteka tena na kusini naye hata akiwa ndani ya ndoa. Dawa pekee ni kujitakasa kwa damu ya Yesu na kuondoa kabisa maagano yote yaluyokuwapo kabla. Hapa ndipo penye mtihani mkubwa na ndoa nyingi za kikristo kuonekana zinayumba mno.

Asili ya nguvu za uumbaji

Nimesema nguvu za mwanamke zimo ndanibya mwanamume, kwa sababu mwanamke ni sehemu ya mwanamume. Mwanamume alalapo na mwanamke huachilia nguvu zake za uumbaji ndani ya mwanamke, naye huzihifadhi nguvu hizo ndani yake, ukizingatia kwamba hawa wawili ni mwili mmoja na roho moja. Kwa hiyo nguvu hizo HAZIPOTEI umpapo mkeo, bali katika roho bado ni zako tu. Hapo unaona kwamba kuna mzunguko wa nguvu na ndio maana mune na mke wakipendana toka moyoni, haya likimpata mmoja, mwenza wake hukosa amani.

Kuzini hovyo ni kutupa nguvu zako, mana yake unabaki mtupu kwa sababu nguvu hizo huisha. Unawapa makahaba nguvu zako ambazo haziwezi kurudi kwako. Hizo ndio nguvu za kujitawala dunia, zimefungwa kwenye viuno vyako. Sasa leo tueleww pake inaposemwa:

1 Petro 3
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁷ Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.


Wanaume kaeni na wake zenu KWA AKILI, tena mkiwapa wake zenu HESHIMA kama chombo kisicho na NGUVU. Mwanamke ni chombo kisicho na nguvu kama nilivyoeleza hapo juu, nguvu zake zimo katika mwanamume. Hivyo unapooa ni lazima umpe mke heshima yake, sio kwamba unamwoa halafu unaendekeza uzinzi. Mwanamke ni dhaifu, kutenda hivyo ni kufungua milango kwake. Hilo lipo kiroho kabisa, ukiwa mzinzi, basi mwanamke naye anaweza kirahisi kabisa kushawishiwa kuchepuka. Ndipo nilisema mwanzoni, kama mkeo ni mzinzi, kwanza jiitazame wewe mwanamume.

Lakini pia imesema sababu ya kukaa kwa akili na kuwapa heshima wake zetu, KUSUDI KUOMBA KWENU KUSIZUILIWE. Hapa iko wazi sasa, NINYI NI NAFSI MOJA. Mmeungana kwa jinsi ya roho na hivyo ni ADAMU MMOJA KATIKA ROHO, maombi pua hufanyika kwa jinsi ya roho. Sasa inapotokea mume hana nia moja na mke katika kuomba, Mungu hawezi kuwasikiliza. Kuomba kwenu kutazuiwa tu. Ndio maana ndoa sio tendo la mchezo mchezo. Wanandoa wengi wameshindwa kuona mkono wa Mungu kwa sababu wao kwa wao wana agenda zao za siri. Ndio maana Paulo ambaye wengi hawamwelewi alisema wazi:

NI HERI MTU ABAKI BILA MKE KABISAAA. LAKINI KWA SABABU YA TAMAA, BASI WATU NA WAOE KULIKO KUANZA KUZINI HOVYO.

Ukikaa bila mke kwa ajili ya Bwana hakika utamwona na utakuwa na nguvu kubwa sana kiroho. Lakini ukiwa na mke, akili yako itakuwa bize kutafakari jinsi gani umpe good time!! Kwamba akili yako itakuwa kidunia zaidi kuliko kumtafakari Mungu. Huo ndio ukweli mchungu.

Mapenzi ya jinsia moja na punyeto

Mwanadamu aliumbwa kumvutia wa opposite sex. Sasa inapotokea roho mbili za jinsia tofauti zinavutana, basi ujue kuna confusion kwenye ulimwengu wa roho. Kuna nguvu iliyobadili mechanism ya roho hata kupoteza mwelekeo. Mtu anayevutiwa na mapenzi kinyume na maumbile ama mwanamume kwa mwanamume ama mwanamke kwa mwanamke, hao wote wanapata hisia zao toka nguvu za giza. Macho yao ya rohoni yametiwa giza hata hawawezi kuona tofauti ya Adamu na Hawa. Tena wapo waliopotea mno hata kulala na wanyama kwa jinsi ya wanadamu. Yote haya ni kwenda kinyume na uumbaji, wala hakuna mwanadamu aliyeumbwa kuwaka tamaa ya kuingiliwa nyuma ama kumwingilia mwingine.

Tena apigaye punyeto na kujichua hujiunganisha moja kwa moja na hayo mapepo yanayovuna nguvu za wanadamu. Ingawa ni rahisi kudhani tunapata hisia kwa njia ya kawaida, lakini hisia zozote zinazokuja tofauti na asili ya mwanadamu zina chanzo tofauti. Ukijisikia hamu ya kujichua, sio wewe, bali uko katika ALTERED STATE!! Akili yako imebadikishwa mfumo wake wa kutazama mambo na hivyo unaongozwa na hisia hasi.

Mtoto akila kinyesi chake tunamkaripia, lakini kwake yeye haoni ubaya. Tena aweza kulalamika kwambaamezakiwa na hisia hizo. Mtu mzima mkijichua tunatetea kwamba amezaliwa hivyo!! Haya ni matatizo ya akili sawasawa na kufirana. Hakuna chenye unafuu kwa sababu yote sio matendo ya asili.

Unapofanya matendo haya unajiua kabisa kiroho, na dalili zake ziko tu. Mtu anayemaliza kupiga punyeto ama kujichua huwa mtupu kabisa kichwani na rohoni (empty). Hili litashuhudiwa na waliowahi kupitia huko, huo ndio ukweli wenyewe. Kufanya hivyo ni kuzielekeza nguvu zako sehemu isiyo sahihi na hivyo zinatumika na mapepo yanayotawala ufahamu wako. Unawapa mapepo wachafu thamani yako nawe unabaki kama msukule tu. Umejiweka namna ya mtumwa.

Itaendelea.........


Maya Angelou, Africa Tanzania, dumbi, LOGARITHM, Sergei Lavrov, LOVE U JF, korino, Mshuza2, park don, Surya, big-diamond, Mwanamena, Tajiri wa Magomeni, dudupori, Bubolwa Chura, Patra31, Depal, alumn, Ed Kawiche, Sexless, The 13, Avriel, Styles
yna2, ngebo, iMind, HoneyBee, Will jr, gbmm, True Believer, Saint Anne[/i][/B][/B], Nature
 
Yako mengi ya kueleza lakini naandika kifupi ili kutotoka nje ya mada. Kwa hiyo mtu akawekwa Edeni kama mtawala wake. Kumbuka kuna kijibustani kingine upande wa Mashariki.

¹⁸ Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.

Hapo ndipo tunakutana na uumbaji wa mwanamke. Mungu alishawaumba katika Roho tangu siku ya kwanza kisha akawaumba katika mwili mwanamke akiwa sehemu kamili ya Adamu mume. Jiulize ni kwa vipi Mungu aliumba viumbe vyote wawili wawili halafu Adam akawa single? Tayari katika design yake alishamweka Hawa ndaniya Adamu.

¹⁹ Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.
²⁰ Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.


Adamu alikuwa na Hawa ndaniyake lakini HAKUONEKANA katika macho ya nyama. Ingekuwa kwamba Adamu aliumbwa peke yake akiwa mtu mume kamili, basi huenda angewawakia tamaa wanyama. Lakini tayari Mungu alikuwa amemuumba akiwa na nafsi ya mkewe ndani yake, ndio maana hakuna sehemu anaonyesha kusikitika, bali Mungu mwenyewe kwa utaratibu wa uumbaji wake akaona si vema awe peke yake.

²¹ Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
²² na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.[


Itoshe kusema Mungu alimwumba mwanadamu toka udongo, kisha akamtenganisha kupata mwanamke na mwanamume. Alichukua nyama ambayo tayari ilitoka kwenye udongo kisha akaingiza sehemu roho ya Adamu ndani yake. Why? Hakuna mahali ambapo Mungu alimpulizia pumzi ya uhai huyu mwanamke siku ya kuumbwa kwake.

Sasa ona tofauti ya maneno hapa, katika kuumba mwanamume neno lililorumika ni yatsar, lakini kwa mwanamke neno la kuumba ni banah. Kwamba Mungu akamuumba (yatsar) mwanamke ... halafu Mungu akamuumba (banah) mwanamume.. Kwa maana halisi, 'Mungu ALIMFINYANGA MWANAMUME kutoka mavumbini lakini ALIMTENGENEZA (fashion) mwanamke toka ubavuni. Ndio maana mwanamke akatoka na sura na umbo zuri la kuvutia ili Adamu avutwe naye.

Adamu alipozinduka usingizini tayari sehemu ya roho yake ishatolewa, ndio maana hakuhitaji maelezo mengi bali moja kwa moja akamtwaa mwanamke na kumwagia sifa lukuki. Hivyo mwanamke NI SEHEMU HALISI YA MWANAMUME na ndio maana MUUNGANIKO HUTOKEA KATIKA ROHO, KUTENGENEZA NAFSI MOJA kama vile Mungu alivyoumba hapo mwanzo. Inaposemwa na Yesu Kristo kuwa tangu mwanzo haikuwa hivyo, inarejea UUMBAJI. Mwanamke na mwanamume walikuwa NAFSI MOJA na ROHO MOJA tangu kuumbwa kwao. Walitengwa kwa kuwekewa miili tofauti, ili kuendeleza uumbaji. Ndio maana tendo la ndoa ni muunganiko wa kiroho ili kurejea uumbaji wa Mungu, na hivyo linafanywa kwa nafsi moja tu.

²³ Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Baada ya kumwona mwanamke alivyoumbwa ndipo akamtwaa. Hapa ndipo ilipo ASILI YA MAPENZI!! Mungu alipoitoa sehemu ya roho ya Adamu kumfanya Hawa aliacha uwazi, vacuum, ambayo inahitaji kujazwa. Mtu pekee anayeweza kuziba huo uwazi ni mwanamke kwa sababu roho yake ndio iliyotolewa kwa mwanamume, hivyo inarejea kwake. Sexual attraction ilianzia hapo, mapenzi yakawa tendo la rohoni wala si mwili. Roho zinavutana kwanza kisha mnakamilisha kwa kulala pamoja na kuingiliana. MAMBO YOTE HUANZA KATIKA ROHO KISHA HUDHIHIRIKA KATIKA MWILI.

²⁴ Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
²⁵ Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.


Mwanamume atamwacha baba na mama yake, why? Mwanamume tangu kuzaliwa kwake roho yake haikufungamanishwa na wazazi wake. Akibalehe na kuuacha utoto roho yake huliona pengo lililoachwa tangu kuumbwa Hawa, hivyo hutangatanga huku na huko kuitafuta ile sehemu yake iliyoondoka.

Mwanamke yeye alitolewa kwa mwanamume na akawa kiumbe ambaye nguvu zake zimo katika mwanamume. Kwamba yeye anakaa kwa wazazi wake huku akitazamia kwamba kuna nguvu itakuja kumwondoa kwao, nguvu ambayo ndio sehemu yake halisi. Sasa huu ni muunganiko wa kiroho, sio kimwili, kwamba mwanamume atamwacha baba na mama kwa kujitenga nao. Ni roho yake kuungana na roho ya mkewe KWA TENDO LA NDOA, ndio maana ikaandikwa NAO SI WAWILI TENA BALI NI MWILI MMOJA. Kumbe unapofanya tendo la ndoa umejiunganisha na mwenza wako kuwa mwili mmoja. Yaani umemwacha baba na mama yako, sasa umejiona umekuwa mtu mzima, ukajitwalia namna ya mke, ukaambatana naye kwa kufanya naye ngono, kwa hiyo ninyi si wawili tena kwa sababu roho zenu zimerudiana na mmekamilisha ule uumbaji wa mwanzo.

Ndipo Kristo katika Mathayo 19 akaongeza kusema ALICHOKIUNGANISHA MUNGU MWANADAMU ASIKITENGANISHE, ikimaanisha kwamba TENDO LA KWANZA LA NDOA ndilo tendo la agano. Sasa hakuna tena mwanadamu anayeweza kuwatenga waliojiunganisha kwa uzinzi bali ni rehwma ya Mungu mwenyewe. Kama umewaacha wazazi wako ukaambatana na mwenzako katika uzinzi, ninyi tayari ni mwili mmoja, nafsi zenu zimeungana katika roho. Mwanadamu wa jinsi ya mwili hana mamlaka tena, bali Yeye aliyeziumba roho zenu.

Ndipo tunapata MAANA YA HAYO MANENO, alichokiunganisha Mungu - yaani agano la damu, mwanadamu asikitenganishe - yaani asije mwanamume mwingine kumwoa huyu mwanamke mwenye agano la ndoa tayari na mwanamume mwingine!! Hapa haikumaanisha kimwili kama tunavyoamini hivi sasa kwamba mume na mke wakifunga ndoa KANISANI basi mwanadamu asiwatenganishe. Ukiyachunguza hayo maandiko, kesi ilikuwa ni ya talaka. Hapo ndipo tunaelewa zaidi maana ya ISIPOKUWA KWA SABABU YA UASHERATI. Kwamba huyu mwanamke alishatembea na mwanamume mwingine kabla ya ndoa, hivyo tayari ana agano!! Hiyo pekee ndio sababu ya MWANAMUME KUMWACHA MWANAMKE. Tena ni wakati gani? Wakati wa KUFUNGA AGANO!! Wakati wa kuingiliana, kama mwanamke hana bikira, kwa sababu ulupomwingilia ULIFUNGA NDOA, unaruhusiwa kumpa talaka. Hapo kifungo chako hakitakuwapo katika roho.

Ukielewa hivi ndipo unaweA sasa kusoma Kumbukumbu la Torati na kuelewa ni kwa nini waasherati na wazinzi waliuawa. Ni mambo ya kiroho zaidi. Pia ndio maana huwa ninasisitizani kwa nini unapotaka kuoa mnapaswa kujitakasa na kuomba rehema ya Mungu ili ndoa yenu idumu (kama mke si bikira). Itakuwa kama wanaume aliotembea nao wapo hai, agano lao ndanai yake pia litaendelea kuwa hai.. Ndipo inakuwa rahisi sana kwa wao kumteka tena na kusini naye hata akiwa ndani ya ndoa. Dawa pekee ni kujitakasa kwa damu ya Yesu na kuondoa kabisa maagano yote yaluyokuwapo kabla. Hapa ndipo penye mtihani mkubwa na ndoa nyingi za kikristo kuonekana zinayumba mno.

Asili ya nguvu za uumbaji

Nimesema nguvu za mwanamke zimo ndanibya mwanamume, kwa sababu mwanamke ni sehemu ya mwanamume. Mwanamume alalapo na mwanamke huachilia nguvu zake za uumbaji ndani ya mwanamke, naye huzihifadhi nguvu hizo ndani yake, ukizingatia kwamba hawa wawili ni mwili mmoja na roho moja. Kwa hiyo nguvu hizo HAZIPOTEI umpapo mkeo, bali katika roho bado ni zako tu. Hapo unaona kwamba kuna mzunguko wa nguvu na ndio maana mune na mke wakipendana toka moyoni, haya likimpata mmoja, mwenza wake hukosa amani.

Kuzini hovyo ni kutupa nguvu zako, mana yake unabaki mtupu kwa sababu nguvu hizo huisha. Unawapa makahaba nguvu zako ambazo haziwezi kurudi kwako. Hizo ndio nguvu za kujitawala dunia, zimefungwa kwenye viuno vyako. Sasa leo tueleww pake inaposemwa:

1 Petro 3
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁷ Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.


Wanaume kaeni na wake zenu KWA AKILI, tena mkiwapa wake zenu HESHIMA kama chombo kisicho na NGUVU. Mwanamke ni chombo kisicho na nguvu kama nilivyoeleza hapo juu, nguvu zake zimo katika mwanamume. Hivyo unapooa ni lazima umpe mke heshima yake, sio kwamba unamwoa halafu unaendekeza uzinzi. Mwanamke ni dhaifu, kutenda hivyo ni kufungua milango kwake. Hilo lipo kiroho kabisa, ukiwa mzinzi, basi mwanamke naye anaweza kirahisi kabisa kushawishiwa kuchepuka. Ndipo nilisema mwanzoni, kama mkeo ni mzinzi, kwanza jiitazame wewe mwanamume.

Lakini pia imesema sababu ya kukaa kwa akili na kuwapa heshima wake zetu, KUSUDI KUOMBA KWENU KUSIZUILIWE. Hapa iko wazi sasa, NINYI NI NAFSI MOJA. Mmeungana kwa jinsi ya roho na hivyo ni ADAMU MMOJA KATIKA ROHO, maombi pua hufanyika kwa jinsi ya roho. Sasa inapotokea mume hana nia moja na mke katika kuomba, Mungu hawezi kuwasikiliza. Kuomba kwenu kutazuiwa tu. Ndio maana ndoa sio tendo la mchezo mchezo. Wanandoa wengi wameshindwa kuona mkono wa Mungu kwa sababu wao kwa wao wana agenda zao za siri. Ndio maana Paulo ambaye wengi hawamwelewi alisema wazi:

NI HERI MTU ABAKI BILA MKE KABISAAA. LAKINI KWA SABABU YA TAMAA, BASI WATU NA WAOE KULIKO KUANZA KUZINI HOVYO.

Ukikaa bila mke kwa ajili ya Bwana hakika utamwona na utakuwa na nguvu kubwa sana kiroho. Lakini ukiwa na mke, akili yako itakuwa bize kutafakari jinsi gani umpe good time!! Kwamba akili yako itakuwa kidunia zaidi kuliko kumtafakari Mungu. Huo ndio ukweli mchungu.

Mapenzi ya jinsia moja na punyeto

Mwanadamu aliumbwa kumvutia wa opposite sex. Sasa inapotokea roho mbili za jinsia tofauti zinavutana, basi ujue kuna confusion kwenye ulimwengu wa roho. Kuna nguvu iliyobadili mechanism ya roho hata kupoteza mwelekeo. Mtu anayevutiwa na mapenzi kinyume na maumbile ama mwanamume kwa mwanamume ama mwanamke kwa mwanamke, hao wote wanapata hisia zao toka nguvu za giza. Macho yao ya rohoni yametiwa giza hata hawawezi kuona tofauti ya Adamu na Hawa. Tena wapo waliopotea mno hata kulala na wanyama kwa jinsi ya wanadamu. Yote haya ni kwenda kinyume na uumbaji, wala hakuna mwanadamu aliyeumbwa kuwaka tamaa ya kuingiliwa nyuma ama kumwingilia mwingine.

Tena apigaye punyeto na kujichua hujiunganisha moja kwa moja na hayo mapepo yanayovuna nguvu za wanadamu. Ingawa ni rahisi kudhani tunapata hisia kwa njia ya kawaida, lakini hisia zozote zinazokuja tofauti na asili ya mwanadamu zina chanzo tofauti. Ukijisikia hamu ya kujichua, sio wewe, bali uko katika ALTERED STATE!! Akili yako imebadikishwa mfumo wake wa kutazama mambo na hivyo unaongozwa na hisia hasi.

Mtoto akila kinyesi chake tunamkaripia, lakini kwake yeye haoni ubaya. Tena aweza kulalamika kwambaamezakiwa na hisia hizo. Mtu mzima mkijichua tunatetea kwamba amezaliwa hivyo!! Haya ni matatizo ya akili sawasawa na kufirana. Hakuna chenye unafuu kwa sababu yote sio matendo ya asili.

Unapofanya matendo haya unajiua kabisa kiroho, na dalili zake ziko tu. Mtu anayemaliza kupiga punyeto ama kujichua huwa mtupu kabisa kichwani na rohoni (empty). Hili litashuhudiwa na waliowahi kupitia huko, huo ndio ukweli wenyewe. Kufanya hivyo ni kuzielekeza nguvu zako sehemu isiyo sahihi na hivyo zinatumika na mapepo yanayotawala ufahamu wako. Unawapa mapepo wachafu thamani yako nawe unabaki kama msukule tu. Umejiweka namna ya mtumwa.

Itaendelea.........
Nitag
 
Nashauri tusome kitabu cha nabii Hosea kwani ni unabii wa pande mbili, kwanza kuhusu ndoa kati ya mume na mke, halafu uhusiano kati ya Mungu na Kanisa. Tunaweza kujifunza jambo KUBWA SANA kuhusu ndoa.

Amani ya Bwana iwe nanyi nyote,
Amina.
 
Nashauri tusome kitabu cha nabii Hosea kwani ni unabii wa pande mbili, kwanza kuhusu ndoa kati ya mume na mke, halafu uhusiano kati ya Mungu na Kanisa. Tunaweza kujifunza jambo KUBWA SANA kuhusu ndoa.

Amani ya Bwana iwe nanyi nyote,
Amina.
Amina Mtumishi. Ninayaelewa sana mada zako. Hongera sana
 
Ndugu yangu nimesoma ujumbe wote na ninashukuru kwa kuyafunua haya ikiwa wewe ni kijana basi nafsi yangu inajisifu maana taifa lenye watu wanao ijua sheria na agano la Mungu Kama wewe hakika limebarikiwa. Kwa pamoja tuzidi kuwakumbuka vijana na kuwaombea Mungu awafunikie maana mashambulizi ya adui ni makali yanahitaji watu shupavu na wenye kufahamu kweli na sheria za ufalme wa Mungu. cariha karibu upate mafundisho ya ufalme uliotimilika ili shetani akuachie
 
Ndugu yangu nimesoma ujumbe wote na ninashukuru kwa kuyafunua haya ikiwa wewe ni kijana basi nafsi yangu inajisifu maana taifa lenye watu wanao ijua sheria na agano la Mungu Kama wewe hakika limebarikiwa. Kwa pamoja tuzidi kuwakumbuka vijana na kuwaombea Mungu awafunikie maana mashambulizi ya adui ni makali yanahitaji watu shupavu na wenye kufahamu kweli na sheria za ufalme wa Mungu. cariha karibu upate mafundisho ya ufalme uliotimilika ili shetani akuachie
Amina
 
Sasa sie ambao hatukuwahi pata mwanamke bikra inakuwaje? Au kama tumeoa mwanamke sio bikra tufanyaje mkuu wetu?

Ila wewe ni mtaalam sana na unajuwa kuzipanga nondo za ukweli.

Salute
 
Sasa sie ambao hatukuwahi pata mwanamke bikra inakuwaje? Au kama tumeoa mwanamke sio bikra tufanyaje mkuu wetu?

Ila wewe ni mtaalam sana na unajuwa kuzipanga nondo za ukweli.

Salute
Asante mkuu. Kuhusu hoja yako, mimi hujibu kwa mujibu wa Biblia. Pale ilipoandikwa "alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe" maana yake ni kuwa, mwanamke na mwanamume wakiungana kwa tendo la ndoa, sio rahisi kuwatenganisha. Ndio maana watu hufikia hatua wakawadhuru wapenzi wao kwa sababu tu hawawezi kutengwa kwa chochote, achia mbali vitisho.

Sasa liko jibu moja tu kwenye Biblia,

Mithali 19 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁴ Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

Sasa mke atokaye kwa Bwana ni yule mwenye uhusiano binafsi na Mungu. Huyu ni mwanamke mwenye hofu ya kweli ya Mungu, ambaye hata kama alianguka hapo kabla, sasa yuko safi kabisa, amejaza neno la Mungu moyoni mwake. Mwanamke anayempenda Mungu kuliko kitu chochote, wala mtu yeyote, huyu afaa kuwa mke.

Kumbuka upendo kwa wanadamu hupoa, lakini upendo wa Mungu hudumu daima. Hakuna sehemu imeandikwa UMPENDE MUME/MKE WAKO KWA MOYO WOTE. Ni Mungu pekee tunayepaswa kumpenda namna hiyo. Sasa wajinga wamepenyeza uongo Makanisani kwamba mke/mume ampende mume/mke kwa moyo wake wote. Kisha baadae utasikia vilio,

"nilimpa moyo wangu akanisaliti."

Mjinga kweli kweli, apewaye moyo si mwanadamu bali ni Mungu pekee. Tafuta mwanamke aliyetoa moyo wake kwa Bwana, maana yake ni kuwa HAKUNA NAFASI YA KUISIKILIZA DUNIA ndani yake. Mambo yote huyapima kwa SHERIA YA BWANA. Wenzake wakimwambia twende club, yeye atasikiliza sauti ya Mungu ndani yake. HUYU NI BIKIRA WA ROHO.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom